Hakuna nafasi ya B2B Boss, Hizi ni sifa za Mchezaji husika zinazomfanya kupewa Jina hilo kwa kuwa tofauti na wachezaji wengine kwenye nafasi hiyo.
LAMPARD ni Kiungo wa Kati CM na Moja ya Viungo bora kuwahi tokea kama Box to Box, Sifa za B2B ni Stamina, Physical Strength, Pressing Ability, Passing Range na Speed ya Maamuzi Pande zote za Uwanja. Mara nyingi amecheza kwenye Double Pivot.
Majukumu ya Ulinzi si lazima kufanya uliyoorodhesha hapo juu. LAMPARD alikuwa Mnyama haswa kwenye Ku-press na Positioning. Tackling ilikuwa udhaifu wake lakini kuzuia si lazima ufanye tackling kuna kina Busquets na Carrick wamecheza DM kwa ufanisi bila kuwa na namba nzuri kama "Tacklers" Ila LAMPARD Pia alikuwa na % kubwa ya Mafanikio ya Tackles chache alozifanya.
Kifupi Lampard ni CM mwenye sifa zote za Kuitwa Box to Box na anatambulika kama Moja ya B2B bora zaidi wahi tokea katika Soka.
Sifa ya kwanza ya box to box awe na uwezo wa kucheza kokote kwenye uwanja, awe na uwezo wa kusaidia mashabulizi na kuzaidia kukaba,
kuna roles na position, nafasi nyingi za uchezaji uwanjani ambazo sisi tunaziita nafasi inafact ni roles na sio nafasi ikiwemo B2B
Na B2B ya mchezaji huyu haiwezi kufanana na B2B ya mchezaji yule. Kila mchezaji ni unique
Tunaposema Kante na Caicedo wamefana sio kwa sura wala kwa urefu. Hawa ni wachezaji wawili tofauti na wamepitia changamoto tofauti
Wachezaji wanaweza kufananishwa kwa takwimu zinazoendana hata kama hazifanani
Saa nyingine unaweza kuwa rigid wa kumuelewa mwenzako kumbe ni lugha tu zimetofautiana, tunazungumzia kitu kile kile
Changamoto sisi tunazopitia Chelsea ukubwa wake uko kwa kocha na wala sio ugeni wala ukosefu wa uzoefu wa wachezaji kama wengine wanavyosema
Tangu Pochettino aje hajawaelewa wachezaji wake sawasawa na kama anawaelewa basi ni mbishi
Yeye anaona kabisa Enzo alicheza vizuri wakati wa Potter alivyotumika kama Jorgninho kwenye namaba 6 (Regista role), yeye mara ampe namba 8 mara ampe namba 10
Caicedo naye n8i kiungo anayecheza vizuri akipewa uhuru na role pekee inayompa uhuru kiungo mwenye uwezo wa kukaba na kutengeneza mashambulizi ni B2B. Palmer akicheza RW anakuwa huru ila yeye anamlazimisha kwenye namba 10