Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Tuna hali mbaya, je hili mido litatufaa ??

Tottenham and Chelsea target Rayan Cherki has been put up for sale in the January transfer window for just £8.5m by Lyon.
1702390944996.png
 
Baada ya mechi 13, Aston Villa walikuwa pointi 1 kutoka kushuka daraja, wakamfukuza Gerrard, Emery akachukua timu, na wakaishia kuingia michuano ya Ulaya.

Makocha wakubwa huwainua wachezaji atakaowakuta. Hawasubiri hadi wanunue wachezaji wanaoingia kwenye mfumo wao.

Tuchel alishinda UCL na Chelsea bila kusubiri asajiliwe wachezaji wake

Nahisi hata kama Pochettino akipewa wachezaji anaowataka bado mafanikio yake kubwa itakuwa ya manati sana
View attachment 2840698

Naimani kwa aina ya wachezaj tulionao sasa ingekuwa chini ya Tuchel tungekuwa mbali now
Yani nahisi tungekuwa tuko tunakimbizana kule juu
 
Baada ya mechi 13, Aston Villa walikuwa pointi 1 kutoka kushuka daraja, wakamfukuza Gerrard, Emery akachukua timu, na wakaishia kuingia michuano ya Ulaya.

Makocha wakubwa huwainua wachezaji atakaowakuta. Hawasubiri hadi wanunue wachezaji wanaoingia kwenye mfumo wao.

Tuchel alishinda UCL na Chelsea bila kusubiri asajiliwe wachezaji wake

Nahisi hata kama Pochettino akipewa wachezaji anaowataka bado mafanikio yake kubwa itakuwa ya manati sana
View attachment 2840698
Huyu unai si alifeli pale arsenal.
 
Dah unalinganisha usingizi na kifo.

Tuchel alikuwa na Mendy, Christensen, Rudger, Silva, Chilwell, Alonso, Kante, Kovacic, Jorgnho, Mount, Werner, Pulisic, Harvetz, Ziyech, Odoi, Cheek

Haya mpe wachezaji tulionao James na Chilwell injuries, Sanchez pazia, Cucurela kituko, Disasi kituko, Caicedo, Enzo, Gallagher uwezo wao haufiki hata robo ya Kante, Jorginho, Kovacic, Mount.

Pulisic, Werner, Odoi, Kai walikuwa wanastruggle kufunga magoli lakini walikuwa bora kuliko sterling, Mudyk, Jackson, Maduake.

Kwanza Tuchel hawezi kukubali kuja kufundisha hizi mbarara ni kuharibu profile yake.

Jinsi Kante na Kovacic walivyokuwa wanatumika chin ya tuchel na ndio hivyo hivyo
Enzo Caicedo wangetumika

Ukiniambia chini ya Poch eneo lipi tuko bora kuanzia defenc mpk kwenye kushambulia?

Unauhakika Tuchel angempamga Sanchez bila kujua uwezo wa Petrovic ukoje?


Ni vile tu Poch hataki kumpa nafas Petrovic nafasi
 
Matumaini mapya kwa majeruhi wetu...ni kurejea uwanjani Jumamosi hii dhidi ya Sheffield United.

Romeo Lavia​

Belgian midfielder Lavia was described in similar terms to Nkunku when Pochettino provided an update on the pair last week.


A "small delay" has set him back but the summer signing is now "so close" to finally making his debut having suffered an ankle injury after his arrival.
Potential return date: December 16, vs Sheffield United

Christopher Nkunku​

Pochettino has hinted that Nkunku is closing in on his long-awaited comeback from a knee injury suffered in pre-season.

Having returned to full training earlier this month, multiple chances for the French striker's debut have come and gone with the Chelsea manager waiting to be given the green light.

"The last step is always the most difficult thing," the manager said last week, adding that he hopes to have Nkunku ready "soon".
Potential return date: December 16, vs Sheffield United
 
Dah unalinganisha usingizi na kifo.

Tuchel alikuwa na Mendy, Christensen, Rudger, Silva, Chilwell, Alonso, Kante, Kovacic, Jorgnho, Mount, Werner, Pulisic, Harvetz, Ziyech, Odoi, Cheek

Haya mpe wachezaji tulionao James na Chilwell injuries, Sanchez pazia, Cucurela kituko, Disasi kituko, Caicedo, Enzo, Gallagher uwezo wao haufiki hata robo ya Kante, Jorginho, Kovacic, Mount.

Pulisic, Werner, Odoi, Kai walikuwa wanastruggle kufunga magoli lakini walikuwa bora kuliko sterling, Mudyk, Jackson, Maduake.

Kwanza Tuchel hawezi kukubali kuja kufundisha hizi mbarara ni kuharibu profile yake.
Hao wachezaji uliowataja walikuwa wa hovyo sana kwa makocha wengine kumbuka
Aliyewainua viwango hao wachezaji ni TT tu
Mfano, Rudiger alikuwa beki wa hovyo wakati wa Lampard ambaye beki wake wa kutumainiwa alikuwa ni Zouma
Alonso alikuwa mzuri kwa Conte akaja Lampard akashuka kiwango
Kwa ujumla majina makubwa ya hao wachezaji ni Tuchel ndie aliyewainua
 
Jinsi Kante na Kovacic walivyokuwa wanatumika chin ya tuchel na ndio hivyo hivyo
Enzo Caicedo wangetumika

Ukiniambia chini ya Poch eneo lipi tuko bora kuanzia defenc mpk kwenye kushambulia?

Unauhakika Tuchel angempamga Sanchez bila kujua uwezo wa Petrovic ukoje?


Ni vile tu Poch hataki kumpa nafas Petrovic nafasi
Mfano uchezaji wa Caicedo ni kama wa Kante, yeey ni box to box midfielder ambaye alitakiwa acheze offesnively zaidi. Ila sasa anachezeshwa kama DM. Hata Enzo naye ni box to box. Usajili wa Midfield utatakiwa ulenge kwenye DM
Mfumo pia wa 4231 ambao Poche anaung'anmg'ania naona kama hauendani na wachezaji waliopo
Conte alipoichukua timu 2016/17 alianza na 433 na matokeo hayakuwa mazuri akaswitch haraka kwenda 343 na akaanza kupata matokeo mazuri

Pochettinoi ni mfahidhina, mfume ule ule hata kama wachezaji hawafit kwenye mfumo
 
Chini ya Poch hakuna eneo lililo bora kwa sababu kila eneo halina exprienced player ambaye ni uti wa mgongo wa eneo husika.

Ushambuliaji - Hakuna exprienced player mwenye uwezo wa kuibeba hiyo safu na kuamua matokeo. Sterling ni kituko

Kiungo - Hakuna exprienced player wa kubeba hilo eneo

Ulinzi - Silva umri umeshamtupa mkono anachofanya sasa hivi anatupa bonus ya mkono wa kwaheri sio tegemezi tena, James & Chilwell watumishi hewa. Hilo eneo la ulinzi huwezi kujivunia kwamba tunaye mchezaji mwamba wa kulibeba.

Kipa ndio kabisa kimeo

Ndio maana Poche anataka asajiliwe kila eneo mchezaji mmoja mwenye exprienced kubwa, wachezaji waliopo waongezee nyama.
Tatizo kubwa la Chelsea sasa hivi ni mbele na hasa striker, maeneo mengine yako sawa kabisa
Tuchel alipochukua UCL alikuwa hana striker wa maana alimtegemea Havert goigoi kwenye false no. 9 na bado akabebo kombe
Pochettino hawezi kuleta matokea ya maana hata akiletewa wachezaji anaowataka

January uongozi utaingia sokoni kumtafutia wachezaji atakaowataka ila sidhani kama tutabadilisha mbao za matokeo
 
unai si alifeli pale arsenal.
Unai HAKUFELI Arsenal. Labda kama kuna maana nyngine Mnayoizungumzia kuhusu Kufeli. Ila amekuwa na Msimu mmoja na Nusu tu na akaifikisha timu Fainali ya Europa na alikuwa na "Winning %" kubwa kuliko hata Arteta. Mikel yeye ana miaka 5 Arsenal na ana Kombe 1 sasa sijajua kama huku ndo kufaulu ama la!

Mfano uchezaji wa Caicedo ni kama wa Kante,
Hapa huu ufananisho hakufanani kabisa. Caicedo ni DM kiasili na ndo namba yake B2B hafai maana namba zake kwenye ushambuliaji sio kubwa.
KANTE alikuwa anaweza hata simama Mwenyewe kama "Lone DM" Kitu ambacho Caicedo hakiwezi. {Kifupi CAIDEDO ni kuporomoka kiusajili, Ni mzuri lakini sio Daraja la KANTE}

Chelsea ya TT unayosema imesukwa zaidi na Lampard ambae si Mwalimu mzuri lakini ukifuatilia mahojiano yake na taswira aliokuwa nayo kwa Chelsea inaonyesha angeweza kuwa Mkurugenzi Mzuri sana wa Michezo. Yeye anakwambia Bodi ilimletea Timo na Kai kitu ambacho mpaka anaondoka hakuwahi jua Nafasi zao Bora ni zipi!

LAMPARD Alitaka msajili RICE na Haaland akiwa bado Salzburg, ila Bodi ikamletea TIMO na KAI.
 
Daaah timu yangu chelsea inanifanya kila siku nalala na viatu huu mkosi sijui utaisha lini.
 
Majeruhi wetu 10 hawa hapa - pamoja na tarehe za matarajio ya kurudi kwao dimbani.

1. Reece James

Baada ya kurejea katika utimamu kamili mwezi uliopita, matatizo ya James yalizidi kuumia siku ya Jumapili. Nafasi yake ilichukuliwa na Levi Colwill kabla ya kuelekea moja kwa moja kwenye handaki huko Goodison Park.

Ni mapema mno kujua ni muda gani atakabiliana nao, hata hivyo, Chelsea na Pochettino watakuwa na matumaini kuwa utambuzi sio mbaya sana.

2. Robert Sanchez
Kipa huyo alipata jeraha la goti katika mechi ya kichapo dhidi ya Manchester United Jumatano lakini alikuwa sawa kucheza dhidi ya Everton. Hata hivyo, baada ya kuumia katika kipindi cha pili, Sanchez alizidisha jeraha hilo leo.
Nafasi yake ilichukuliwa na Djordje Petrovic.
Alichosema Pochettino: "Alipata tatizo dhidi ya Manchester United, tatizo kwenye goti lake na alihisi kitu katika kipindi cha pili."

3. Christopher Nkunku
Baada ya miezi kadhaa ya ukarabati, Nkunku hatimaye amerejea kwenye mazoezi ya kikosi cha kwanza. Mauricio Pochettino alifichua kuwa safari ya katikati ya wiki kwenda Manchester United ilikuwa mapema sana na alikosa wikendi pia.
Alichokisema Pochettino: "Bado tunatathmini siku baada ya siku, ona kesho. Siamini kwamba atahusika lakini tunatakiwa kutathmini siku baada ya siku."
Akizungumza kabla ya kushindwa na Everton, alisema: "Hatua ya mwisho huwa ni jambo gumu zaidi. Wako karibu sana, lakini wakati huo huo tulikuwa na ucheleweshaji mdogo, lakini tunatumai kwamba wanaweza kuhusika hivi karibuni."
Tarehe inayowezekana ya kurudi: Sheffield United (H) - Jumamosi, Desemba 16.

4. Romeo Lavia
Lavia amekuwa akiuguza tatizo la kifundo cha mguu tangu alipowasili Stamford Bridge na bado hajacheza mechi yake ya kwanza kwa The Blues. Mwezi uliopita, kiungo huyo wa kati alikabiliwa na kikwazo kikubwa katika safari yake ya kupona, na hivyo kusukuma tarehe yake ya kurejea mwezi Desemba.

Alichosema Pochettino: "Romeo anaendelea vizuri pia lakini kama Christopher hatahusika."

"Hatua ya mwisho daima ni jambo gumu zaidi. Wako karibu sana, lakini wakati huo huo tulikuwa na ucheleweshaji mdogo, lakini tunatumai kwamba wanaweza kuhusika hivi karibuni."

Tarehe inayowezekana ya kurudi: Sheffield United (H) - Jumamosi, Desemba 16

5. Malo Gusto
Malo Gusto alijiondoa kwenye kikosi cha Ufaransa chini ya miaka 21 mwezi Novemba kutokana na jeraha la goti. Beki huyo mwenye umri wa miaka 20 alifanyiwa uchunguzi wa MRI na baadaye ikabainika kulikuwa na 'kidonda kidogo' kwenye ligament ya ndani ya upande.

Ingawa hakuingia kwenye kikosi dhidi ya Brighton, alionekana akirejea kwenye mazoezi ya kikosi cha kwanza cha Chelsea kabla ya mechi, na kupendekeza kwamba anaweza kupatikana kwa mchujo hivi karibuni.

Alichosema Pochettino: "Tunaona pia kama Malo Gusto anaweza kupatikana lakini mbali na hayo hakuna
Tarehe inayowezekana ya kurudi: Sheffield United (H) - Jumamosi, Desemba 16

6. Noni Madueke
Madueke aliachwa kwenye benchi kwa pambano dhidi ya Brighton na hakutokea mbadala. Anakaribia kukosa kucheza baada ya kushuka uwanjani kutokana na jeraha dogo akiwa mazoezini.

Jina lake liliondolewa kwenye orodha ya majeruhi mbele ya Everton lakini aliachwa kabisa na kikosi cha Merseyside.
Alichokisema Pochettino: "Noni baada ya mechi, baada ya Brighton pia, matatizo madogo yanatumai kwamba hivi karibuni watapatikana kufanya mazoezi na kupatikana kwa timu."

Tarehe inayowezekana ya kurudi: Sheffield United (H) - Jumamosi, Desemba 16

7. Lesley Ugochukwu
Ugochukwu alikuwa mwingine ambaye hakucheza dhidi ya United baada ya kupata jeraha dogo baada ya mechi ya Brighton. Kinda huyo hakujumuishwa kwenye kikosi kilichokabiliana na Seagulls pia lakini hata hivyo alifutiliwa mbali kwa safari ya kuelekea kaskazini.

Alichosema Pochettino: "Lesley anahisi kitu wiki hii, jeraha dogo. Noni baada ya mechi, baada ya Brighton pia, matatizo madogo yanatumai kwamba hivi karibuni watapatikana kufanya mazoezi na kupatikana kwa timu."

Tarehe inayowezekana ya kurudi: Sheffield United (H) - Jumamosi, Desemba 16

8. Ben Chilwell
Chilwell alipata pigo kuelekea mwisho wa mpambano wa Chelsea na Brighton kwenye Kombe la Carabao mwishoni mwa Septemba. Kwa bahati mbaya kwa beki huyo wa The Blues, klabu iligundua haraka kuwa tatizo la misuli lilikuwa baya kuliko ilivyofikiriwa na, zaidi ya mwezi mmoja baadaye, bado yuko nje ya uwanja.

Alichosema Pochettino: "Siwezi kukuambia [atarejea lini]. Ni vigumu kujua. Yuko mbali na uwanja wa mazoezi sasa na tutamsubiri arudi kuona hali ilivyo. Tunatumai anaweza kupona. haraka iwezekanavyo."

Tarehe inayowezekana ya kurudi: Mwishoni mwa Desemba

9. Trevoh Chalobah
Chalobah amekuwa akiuguza jeraha la paja na bado hajaichezea Chelsea msimu huu. Ameonekana akifanya mazoezi kwenye gym huko Cobham wakati wa mapumziko ya kimataifa lakini kurejea uwanjani kunaonekana kuwa mbaya.

Tarehe inayowezekana ya kurudi: Haijulikani

10. Carney Chukwuemeka
Chukwuemeka alipata goli kabla ya mechi akiwa na Arsenal na kisha akaweka benchi dhidi ya Burnley, lakini kiungo huyo amepata pigo lingine. Amekuwa na tatizo la goti ambalo alikumbana nalo dhidi ya West Ham United mapema kwenye kampeni.

Amechapisha kwa mara nyingine tena kutoka kwa Cobham anapopata nafuu na kazi kwenye gym.

Tarehe inayowezekana ya kurudi: Haijulikani
 
Chini ya Poch hakuna eneo lililo bora kwa sababu kila eneo halina exprienced player ambaye ni uti wa mgongo wa eneo husika.

Ushambuliaji - Hakuna exprienced player mwenye uwezo wa kuibeba hiyo safu na kuamua matokeo. Sterling ni kituko

Kiungo - Hakuna exprienced player wa kubeba hilo eneo

Ulinzi - Silva umri umeshamtupa mkono anachofanya sasa hivi anatupa bonus ya mkono wa kwaheri sio tegemezi tena, James & Chilwell watumishi hewa. Hilo eneo la ulinzi huwezi kujivunia kwamba tunaye mchezaji mwamba wa kulibeba.

Kipa ndio kabisa kimeo

Ndio maana Poche anataka asajiliwe kila eneo mchezaji mmoja mwenye exprienced kubwa, wachezaji waliopo waongezee nyama.

Mnajificha kwenye hicho kivulo cha experience

Simple qn
Hiv mchezaj mpka acheze miaka mingapi o game ngapi ndio useme anaexperience???
 
Unai HAKUFELI Arsenal. Labda kama kuna maana nyngine Mnayoizungumzia kuhusu Kufeli. Ila amekuwa na Msimu mmoja na Nusu tu na akaifikisha timu Fainali ya Europa na alikuwa na "Winning %" kubwa kuliko hata Arteta. Mikel yeye ana miaka 5 Arsenal na ana Kombe 1 sasa sijajua kama huku ndo kufaulu ama la!


Hapa huu ufananisho hakufanani kabisa. Caicedo ni DM kiasili na ndo namba yake B2B hafai maana namba zake kwenye ushambuliaji sio kubwa.
KANTE alikuwa anaweza hata simama Mwenyewe kama "Lone DM" Kitu ambacho Caicedo hakiwezi. {Kifupi CAIDEDO ni kuporomoka kiusajili, Ni mzuri lakini sio Daraja la KANTE}

Chelsea ya TT unayosema imesukwa zaidi na Lampard ambae si Mwalimu mzuri lakini ukifuatilia mahojiano yake na taswira aliokuwa nayo kwa Chelsea inaonyesha angeweza kuwa Mkurugenzi Mzuri sana wa Michezo. Yeye anakwambia Bodi ilimletea Timo na Kai kitu ambacho mpaka anaondoka hakuwahi jua Nafasi zao Bora ni zipi!

LAMPARD Alitaka msajili RICE na Haaland akiwa bado Salzburg, ila Bodi ikamletea TIMO na KAI.
Caicedo hata RB alishacheza vizuri Brighton ilipomfunga Man U 1-0 mwaka jana.
Umemtaja Kante, hawa ni moja wa wachezaji ambao unaweza confuse roles zao uwanjani kwa sababu wanamudu nafasi nyingi. Akiwa Lecester city alichezeshwa kama lone DM na hata wakati wa Conte hivyo hivyo kwenye 3-5-2. Ila alipokuja Sari na baadaye Lampard na hao waliofuata wote walimpa advance role ya namba 8 box to box miedlfielder na sio DM. Na nafasi hiyo hiyo ndio iliyomuwezesha TT akabeba UCL Kante akicheza Advanced roles kwenye kushambulia. Kwanini makocha kama Sari, Lampard, TT, Potter walimchezesha mbele, ni kwa sababu ya uwezo wake mkubwa wa kufanya ball recoveries na kuanzisha mashambulizi ya counter attack. Mechi za Real Madrid, Athletico Madrid, Porto tulishinda kwa urahisi kwa sababu ya hizo roles za Kante.

Back to Caicedo, hadi sasa Caicedo anajulikana hivyo kuwa ni DM wa kwenye double pivot, ni sawa ila tukumbuke ya Kante ambaye alikuwa mzuri kwenye DM kumbe na nafasi zingine anacheza vizuri tu
Caicedo ana uwezo mkubwa wa kunyang'anya mipira, kublock na kufanya strategic passes ambazo hizo zitakuwa na manufaa zaidi kama akicheza advanced roles za namba 8 kuliko akicheza kama DM
Bahati mbaya hata Enzo naye ni box to box midfileder ambaye anafaa kucheza namba 8. Sijui Kama Lavia yeye anakuwa best kwenye position ipi;
 
Unai HAKUFELI Arsenal. Labda kama kuna maana nyngine Mnayoizungumzia kuhusu Kufeli. Ila amekuwa na Msimu mmoja na Nusu tu na akaifikisha timu Fainali ya Europa na alikuwa na "Winning %" kubwa kuliko hata Arteta. Mikel yeye ana miaka 5 Arsenal na ana Kombe 1 sasa sijajua kama huku ndo kufaulu ama la!
Kwa taarifa yako Unai Emery alifukuzwa Arsenal kwa sababu za kufanya vibaya kwenye ligi na kuwa alionekana mbele ya uongozi wa Arsenal kuwa hafai kwenye kandanda la Uingereza. "Incompartible with EPL"

Sorry, Unai Emery wining percentage yake ilikuwa ni 55%, Arteta mwenye 58% na Arsenal Wenga mwenye 57%. Sasa hiyo unayosema wewe ana wining percentage kubwa kuliko Arteta imetoka wapi?

1) Tatizo kubwa la kwanza la Emery ni lugha ya kiingereza, alishindwa kuwasiliana na wachezaji kwa sababu english yake ilikuwa poor

2) Tatizo la pili aliingiza timu kwenye hasara ya kumnunua pepe kwa mil 72 na kuvunja rekodi ya timu na baadaye Pepe akaflop ile mbaya

3) Tatizo la tatu, Arsenal iliangukia pua ile fainali ya Eurpoa dhidi ya Chelsea na kuwaudhi wakubwa wa Emirate

4) Kwenye ligi pamoaj na kwenda mechi 22 bila kufungwa, Arsenal ilikuja kupoteza mechi kijinga jinga mwishoni na kuifanya Arenal ishindwa kuingia top 4

5) Dressing room iliharibiak kwa sababu alikosa ushirikiano na staff wengine na wachezaji. Kwenye Mechi msimu wake wa mwisho alitumia wachezaji 35 na kwenye HT sub alifanya sub 32 ambazo ni kubwa kwenye timu zote za EPL

Hali ya sumu iliendelea kuitafuna dressing room hadi alipofukuzwa hiyo tarehe 29 November 2019 baada ya kucheza mechi 7 mfululizo bila kushinda.

Maisha ya Unai Emery akiwa Arsenal yalikuwa mabaya kuliko tunavyodhani na aliondoka kwa aibu bingwa wa mara nne Europa League, mara 3 kwa Sevilla na mara 1 kwa Villareal

Sasa hapo ukisema Unai Emery hakufeli Arsenal ni kwamba wewe umebase kwenye kuifikisha timu Euroap fainal na wining percentage ya 55%

'Factor singine hukuwaza kama hizo point nilizozitoa hapo juu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom