Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Pamoja kwamba unasema Kocha ana mapungufu lakini pia wachezaji wengi wana mapungufu (wamekutana pipa na mfuniko).
Ndg, wachezaji ni kama kuku wa kufugwa, ukisema wachezaji wana mapungufu unakosea
Hakuna mchezaji asiye na mapungufu, kocha ndie kazi yake kuwatengeneza, wale wasiotengenezeka anatakiwa kuwatosa ili uongozi uwaingize sokoni. NO EXCUSE. Kocha anatakiwa awe on top ya matatizo yote
 
Kumbuka Wakati wa conte tulikuwa na wachezaji wenye uwezo mkubwa ila mfumo wa mwanzo ndio ulikuwa na matatizo ndio maana akabadilisha mfumo

Haya niambie Poche anaimprove vipi mapungufu ya uwezo mdogo wa Sterling, Jackson, Mudyk, Broja na Madueke kwenye kufunga magoli?

Kwahiyo Poche akibadilisha mfumo ndio wakina Jackson mapungufu ya ufungaji yataisha na wataanza kufunga magoli?
Hii timu akipewa kocha mwenye akili anabeba kombe. Kumbuka Lampard alisota na timu ambayo TT alikuja akabeba nayo UCL.
Mimi naona tuna wachezaji wazuri sana, kocha tu hana ukatili alionao akina Arteta, Kipara, na hao wengineo mnaowajua
 
Kwa kweli binafsi hata silaumu safu ya ulinzi kwa maana kwamba kama unashindwa kufunga magoli basi tegemea wewe ndio utafungwa.

Ishu kuu hapa ni kuongelea mapungufu ya washambuliaji wetu kwanini wanashindwa kutumia nafasi za wazi kufunga magoli?

Kama unataka tuboreshe tuu safu la ulinzi tusifungwe magoli basi kocha abadili mfumo tuwe tunajilinda tuu, tuachane na ushambuliaji hauna maana kwa sasa.


------- Sterling ------ Palmer -----

--- Gallagher - Caicedo - Enzo ----

Cucu - Colwil - Silva - Disasi - James
Mbona kwa City walitumbukiza 4
Mbona kwa Arsenal walitumbukiza 2
Hata hao akina Jackson akija kocha mwenye akili, watafunga hadi ufurahi
 
Game ya Newcastle chance ngapi tumetengeneza???(1st half ngapi n 2nd half ngap)

2nd half mara ngapi tumefika kwenye box la newcastle????

Tangu 1st half unaona kabisa team inahitaj mabadiliko 2nd half inaanza hufanya unakuja fanya mabadliko huku tushafungwa goal 3 unategemea hayo mabadiliko yatakuwa na matokeo chanya?
Game ya NC tuliongoza tangu 2005 kucheza na silly individual mistake nyingi sana. Lile game lilivutugika kwa sababu wachezaji hawakutaka kucheza kabisa. Kama vile hakuna serious push kutoka kwa kocha, Silva sio mchezaji wa kufanya ujinga ule
James sio mchezaji wa kufanya ujinga ule
Mabeki walijikusanya kama nyumbu wa Serengeti upande mmoja na kutoa nafasi za kijinga. Kiufupi hakukuwa na seriousness yeyote kwa wachezaji walioingia uwanjanio siku hiyo. Ni kama walikuwa kwenye mgomo
So hata hiyo game haifai kuchambua na kufananisha na game zingine
lilikuwa ni game la UTUMBO
 
Halaf mtu anakwambia Poch hana makosa
Kocha ni kama dereva
Gari likipata shida yeyeote isiyokuwa ya kiwandani, makosa yote kwa dereva
Kochga anayo mamlaka yote ya nani acheza nani aingisub nani atoke sub kulingana na anavyoasses kuanzia kwenye mazoezi hadi uwanjani. Sasa shida inatokea na meli inaonekana inazama halafu nahodha amekaa tu hafanyi jambo halafu tuje kuwalaumu abiria hakupiga mbizi kujiokoa?
Kocha ni dreva
Kocha ni rubani
Kocha ni kapteni wa meli
Kocha ni kila kitu hakwepi lawama
 
Kingine niwakumbushe kuna aina mbili za makocha

1. Kuna kocha ambaye anakamilisha maandalizi na mipango ya mechi kwenye uwanja wa mazoezi kulingana na mpinzani anayeenda kucheza naye.

Huyu kocha akiingia kwenye mechi hutamuona akibabaika wala kufanya sub za hataka, akiamini kwamba home work alifanya vuzuri uwanja wa mazoezi ni wachezaji tuu waimplement uwanjani.

2. Kuna Kocha ambaye uwanja wa mazoezi anafanya yale mambo basics ila kwenye mechi kila dakika inavyokwenda anabadilisha mbinu na mifumo kulingana na mpinzani anavyocheza, mfano nzuri ni Tuchel

Poche ni kocha anayemaliza kila kitu kwenye uwanja wa mazoezi, Kwahiyo wale wachezaji anaowapa dhamana ya kuimpliment mbinu zake uwanjani ndio wanamuangusha.
kocha hawezi kufuatilia matukio akanusa hatari hili limenishangaza , kabla ya Silva kufanya like kosa tayari alifanya kosa la namna hiyo hiyo bahati nzuri akawa karibu na kibendera ikawa Kona , kisha akafanya hivyo hivyo karibu na goli tukapigwa chuma, Pili Joelinton karuka free header akatukosa na alijilaumu sana ilikuwa ni free kwelikweli , baada ya muda tukafungwa free header Tena na beki wakati sio corner , huu ni ujinga angekuwa morihno au Fergie asingevumilia huu ujinga , TATU Badiashile anakubali kuzungukwa na Gordon akiingia kwenye box badala ya kumbana akimbilie kwenye kibendera nje ya box what a poor defender , kocha ana colwill nje anayeweza kucheza katikati vizuri na kuwin duels, poch Kuna wakati anakuwa na mentality za wanawake kuamka na off mood na kujizima data.
 
Kingine niwakumbushe kuna aina mbili za makocha

1. Kuna kocha ambaye anakamilisha maandalizi na mipango ya mechi kwenye uwanja wa mazoezi kulingana na mpinzani anayeenda kucheza naye.

Huyu kocha akiingia kwenye mechi hutamuona akibabaika wala kufanya sub za hataka, akiamini kwamba home work alifanya vuzuri uwanja wa mazoezi ni wachezaji tuu waimplement uwanjani.

2. Kuna Kocha ambaye uwanja wa mazoezi anafanya yale mambo basics ila kwenye mechi kila dakika inavyokwenda anabadilisha mbinu na mifumo kulingana na mpinzani anavyocheza, mfano nzuri ni Tuchel

Poche ni kocha anayemaliza kila kitu kwenye uwanja wa mazoezi, Kwahiyo wale wachezaji anaowapa dhamana ya kuimpliment mbinu zake uwanjani ndio wanamuangusha.
Mhe kwa taadhima zote, makocha wazuri wanachanganya mbinu kuna mbinu na mikakati ya kwenye mazoezi, na kuna mbinu na mikakati ya uwanjani kama utabiri juu ya mpinzani emeenda tofauti. Kwa ligi za ulaya timu zinabadilika nazo ukitegemea mfumo mmoaj tu utaua timu
Ubovu wa Pochettino yuko kama Potter, hana plan B, anaona kabisa mambo yameenda tofauti halafu kang'ang'ana na first 11 yake tu

TT ubovu wake alitgemea mbinu tu bila kuwa na pattern ya uchezaji

Mimi naona kocha anayechanga zote ndie kocha mzuri unless mfumo wako ni imara na wa kifahidhina kama ya mzee kipara
 
Wakati wa Hazard, Willian, Kante, Kovacic, luiz, n.k performance yao ilivyokuwa chini tulikuwa tunasema wachezaji ni wavivu hawajitumi, mgomo baridi ila walikuwa na uwezo mkubwa sana uwanjani.

Hawa wachezaji tulionao sasa hata wajitume mara 10 ya Gallagher uwanjani, still wengi uwezo wao mdogo uwanjani.

Hata wale wachache angalau wanaojiweza kiuwezo wanamezwa na hao wengi ambao hawana uwezo.

Tunao wachezaji wengi wa midtable teams na sio level ya THE BLUES, uwezo wao ndio umefika mwisho, hawafundishiki zaidi. Atakuja kocha mwingine the same lawama kwa makocha zitaendelea hapa.
Ebu tutajie wachezaji wabovu kwenye hii timu, kama wako wapo benchi au walitakiwa kuwa benchi
Timu imecheza vizuri kabisa na Liverpool mechi ya ufunguzi, imecheza vizuri sana na Arsenal, imecheza vizuri na kuisambaratisha Tottenham, imecheza vizuri kabisa na kipara halafu mnasema wachezaji wabovu. Hao wanatakiwa kuchapwa viboko 12 mbele ya mashabiki na asiyetaka aondoke
 
kocha hawezi kufuatilia matukio akanusa hatari hili limenishangaza , kabla ya Silva kufanya like kosa tayari alifanya kosa la namna hiyo hiyo bahati nzuri akawa karibu na kibendera ikawa Kona , kisha akafanya hivyo hivyo karibu na goli tukapigwa chuma, Pili Joelinton karuka free header akatukosa na alijilaumu sana ilikuwa ni free kwelikweli , baada ya muda tukafungwa free header Tena na beki wakati sio corner , huu ni ujinga angekuwa morihno au Fergie asingevumilia huu ujinga , TATU Badiashile anakubali kuzungukwa na Gordon akiingia kwenye box badala ya kumbana akimbilie kwenye kibendera nje ya box what a poor defender , kocha ana colwill nje anayeweza kucheza katikati vizuri na kuwin duels, poch Kuna wakati anakuwa na mentality za wanawake kuamka na off mood na kujizima data.
Nasikia January tunasajili wachezaji wazoefu watatu

Badiashile, Maatsen, Gallagher na Chalobah watauzwa January ili kuleta beki aliyekomaa na asiye injury prone
Pia striker worldclass nk
 
Hahahaha

Mi nakubaliana na wewe chief kwamba tusilaumu tuu mapungufu ya kocha bila pia kulaumu individuals errors/mistake za wachezaji + uwezo wao

Umeeleza vizuri sana, beki mvivu kwenye kuruka mipira ya kichwa, beki anasahau kufanya marking, mchezaji anapiga pass za ovyo ovyo, mshambuliaji anabaki na kipa anambabua au kupaisha kweli haya nayo ya kumlaumu kocha?

Ile mechi ya juzi ukiiangalia individuals error zilikuwa nyingi sana kuliko mapungufu ya kocha.
Sijaona popote mchezaji analaumiwa huku kocha kakaa pale kama vile hausiki
Hujamuelewa Lukub said: Huyo Pochettino alitakiwa aingilie kati, individual error ni dalili kwamba mchezaji hayupo mchezoni
Alitakiwa kufanya sub imediately ili kupeleka ujumbe kwa wanaobaki
Pochettino ni zinga la kocha mjinga sana hasa ni mgumu kwenye kufanya sub pale inapohiotajika
 
Hamna kocha wakuu.

Mkitaka kujua hilo, hao wachezaji wenu mpeni Ange Postecoglu halafu muone kama hagombanii ubingwa.

Mtafute kocha wa maana.
 
Kwa maoni yangu, timu ikifanya vibaya tena ile ya makusudi kama hilo game na Newcastle watu hawa wanastahili kulamiwa kwa nguvu zote
  1. Kocha mkuu kwa niaba ya benchi lote la ufundi, wanayo mandate ya kubadili hali ya hewa kabla ya mechi na wakati wa mchezo
  2. Kapteni wa timu - kwa hili Reece james hafai kuwa kapteni, fuatilieni makapteni wengine, uwanjani na dressing room anawatia morali wezake wapandishe mzimu hadi washinde kwetu Reece James na kama hawa mawaziri wetu Tanzania, too slender too soft, sio hata akiwa agressive uwanjani
  3. Seniour player - mchezaji kama Silva, Rahim Sterling ni wa kulaumiwa sana kwa kutocheza kwa mfano
 
Hii timu akipewa kocha mwenye akili anabeba kombe. Kumbuka Lampard alisota na timu ambayo TT alikuja akabeba nayo UCL.
Mimi naona tuna wachezaji wazuri sana, kocha tu hana ukatili alionao akina Arteta, Kipara, na hao wengineo mnaowajua
We unaona Arteta kuna kitu mule? tofauti y Arteta na Poch ni mmoja anafundisha chelsea wkt mwingine Arse88.
 
We unaona Arteta kuna kitu mule? tofauti y Arteta na Poch ni mmoja anafundisha chelsea wkt mwingine Arse88.
🤣🤣🤣...umefufuka leo mkuu....Arteta yuko juu ya tawi ananing'inia sasahv....Pochettino anapigana viwiko na kina Fulham huko chinichini...utofauti mkubwa sana
 
Pep au Klop ungempa £1.B ya usajili, nadhani wangechukua makombe ya kila aina, wasingesajili wachezaji ovyo ovyo kama tulivyofanya. View attachment 2827307
Kwani hio billion yote katumia pochetinho.
Mpeni hata miaka miwili muone.
sisi ETH hatumpi pressure yoyote, msimu wa kwanza tumechukua kombe 1, final ya FA, nusu final EUROPA, na nafasi ya tatu EPL
Msimu huu bado ndio unaanza, hatuna wasiwasi nae.
Jifunzeni kuvumilia.
Liverpool walikaa miaka 3 ndio klopp akajipata.
Arsenal na arteta miaka 5 hawana EPL, msimu jana ndio wameonja top 4 na uefa, lakini wakija humu ni kelele.

TRUST THE PROCESS, chelsea timu nzuri
 
Sijaona popote mchezaji analaumiwa huku kocha kakaa pale kama vile hausiki
Hujamuelewa Lukub said: Huyo Pochettino alitakiwa aingilie kati, individual error ni dalili kwamba mchezaji hayupo mchezoni
Alitakiwa kufanya sub imediately ili kupeleka ujumbe kwa wanaobaki
Pochettino ni zinga la kocha mjinga sana hasa ni mgumu kwenye kufanya sub pale inapohiotajika
Exactly kocha ni kama mwanaume mwenye mwanamke mjamzito ,unaona mwanamke anableed unamuangalia TU,analalamika tumbo au kichwa kinauma upo kimnya.Ndio kilichokuwa kinaendelea uwanjani awareness ya wachezaji ilikuwa chini sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom