Sasa hata huo muda hizo dkk 15 anazopewa hakuna cha maana touch zake mbovu anachowaza ni kukimbia tuuh ,
Mudryk hana convidence kwa sababu kocha hakumpa
Kwa mchezaji anayetoka ligi ndogo na umri mdogo anahitaji kuaminiwa, kutiwa moyo na kusukumwa ili afuate maelekeoz ya kocha Dizerbi ndivyo anavyofanya.
Huku Chelsea kuna utamaduni wa kuwatia wachezaji kwenye presure kama kocha mwenye alivyo na presure ya kuogopa kutimuliwa
Hii dhana ya kushindania nafasi haifai kwa kila mchezaji
Mchezaji kama Sterling anatakiwa kushindania nafasi ila wachezaji kama Angelo, Deivid, Mudrk, Maatsen, na wale wote U21 wanatakiwa kuaminiwa na kupewa muda wa kutosha huku wakipewa maelekezo ya kimbinu, kutiwa moyo, kupewa inspiration, kusukumwa bila kuchoka. Hazard alipohamia mwka 2012 alipewa muda wakutosha, alikuwa na miaka 21, baada ya kufanywa hivyo ndipo akaja kuwa mchezaji hatari
Kwa wasiojua Hazard alikuwa mvivu sana kwenye hiyo miaka ya 21
Naomba Mungu Pochettino ampe muda wa kutosha sio chini ya 30mins kila game
Evan Ferguson ana miaka 18 tu na ameshakuwa mwiba pale Brighton, Angekuwa Chelsea angepewa huo muda? au angepelekwa kwenye mkopo chap chap akajinoe huko hata kama kashanoleka
Angalia Angelo, Casadei, Andrey Santos hasa Angelo na Casadei wangefaa kabisa kucheza Chelsea lakini wamepelekwa mkopo
Hata huyui Deivid Washington alikuwa apelekwe tu ni kwa sababu muda uliisha na spots za international loan ziliisha
Chelsea yetu imelaaniwa, kwanza tuiondoe hiyo laana ndipo turudi kucheza mpira