Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

£148 Post-Match Reaction
FB_IMG_1692556350339.jpg
 
Kafanya makosa saba na ya mwisho ikawa penalti na goli, kuanguka sio mwisho wa safari, makosa aliyofanya haimuondolei kuwa sio DM mzuri
Issue anao uwezo wa kuhandle price yake kama Declan Rice au hata Enzo?

Kingine mna uhakika atakavyotumika Chelsea ataleta impact aliyoitoa akiwa Brighton?
 
Tatizo la hii timu hata sio wachezaji. Tatizo ni culture ya uchezaji. Timu ni mwendo wa slow buildup na slow transformation kutoka nyuma kwenda mbele (huu ndio mtihani mkubwa kwa pochettino) mpira wa sasa bila identity hata tutengeneze timu ya all stars bado mambo yatakuwa hayahaya. All in all toka mwanzo nilisema tunapambania kuanzia nafasi ya sita kushuka chini na hili halitabadilika hata tukishinda game 5 mfululizo
Liverpool tulicheza vizuri, ila leo sijui wamewadharau Westham, too slow hadi inakinaisha
 
Tumepigwa mzee ndomaana hata makocha tuliokuwa nao hawampi nafasi hajiamini anacheza kwa presha sana
Tumepigwa no, hapewi nafasi kubwa kwa sababu anatakiwa azoee ligi, sio kila mchezaji akienda ligi mpya lazima azoee haraka. Na pia kwa umri wake incosistency ni kawaida. Wengi hadi wafikishe miaka 23 ndio wanatulia. Talent za Mudryk ziko wazi zitadevelop naman gani, hii ni kazi ya kocha. Anahitaji apewe zaidi mechi ndogo nyingi kama za karabao na FA mwanzoni.
 
Issue anao uwezo wa kuhandle price yake kama Declan Rice au hata Enzo?

Kingine mna uhakika atakavyotumika Chelsea ataleta impact aliyoitoa akiwa Brighton?
Yule Di zerbi ni jini, si unaona amebakiwa na takataka lakini bado anayaburuta yalete matokeo. Hii timu angepewa Di zerbi ingekuwa balaa
 
Tatizo la hii timu hata sio wachezaji. Tatizo ni culture ya uchezaji. Timu ni mwendo wa slow buildup na slow transformation kutoka nyuma kwenda mbele (huu ndio mtihani mkubwa kwa pochettino) mpira wa sasa bila identity hata tutengeneze timu ya all stars bado mambo yatakuwa hayahaya. All in all toka mwanzo nilisema tunapambania kuanzia nafasi ya sita kushuka chini na hili halitabadilika hata tukishinda game 5 mfululizo
Well said, build up ya konokono.
 
Well said, build ya konokono.
Chukwuemeka alikuwa anasaidia kuifungua defense ya Westham, ila alipoumia tu, mabeki wakaamua kupasiana mpira wenyewe kwa wenyewe kikonokono halafu eti tunaambiwa Possesion ni 75%
Mpira wa leo baada ya HT ulikuwa mbovu na bado kuna wanachelsea wanausifia sana
 
Timu imetumia karibia £1bn in 1 Year, Lakini bado ukiitazama hii timu kwa jicho la tatu ni kama inahitaji £500ml Extra kwa ajili ya Investment nyingine.
 
Timu imetumia karibia £1bn in 1 Year, Lakini bado ukiitazama hii timu kwa jicho la tatu ni kama inahitaji £500ml Extra kwa ajili ya Investment nyingine.
Hiyo ni ya madirisha matatu tangu akina Boehly wachukue timu
Two summers and one january window
Halafu hiyo bilioni moja ni ya maneno tu, kiasi kilicholipwa cash haifiki hata 400M
 
Timu imetumia karibia £1bn in 1 Year, Lakini bado ukiitazama hii timu kwa jicho la tatu ni kama inahitaji £500ml Extra kwa ajili ya Investment nyingine.
Ulipaji umefanywa kwenye installment ya miaka mingi sio cahs ya mara moja. vinginevyo FFP ya EPL na na UEFA wangeshabisha hodi
 
Yule Di zerbi ni jini, si unaona amebakiwa na takataka lakini bado anayaburuta yalete matokeo. Hii timu angepewa Di zerbi ingekuwa balaa
Nilishawahi kusema humu Brighton ina wachezaji wa kawaida ila inabebwa na mfumo wa kocha sasa huyu Caicedo tuliomchukua tuone uwezo wake pale chelsea isije ikawa tumepigwa tena kama Cucurela
 
Nilishawahi kusema humu Brighton ina wachezaji wa kawaida ila inabebwa na mfumo wa kocha sasa huyu Caicedo tuliomchukua tuone uwezo wake pale chelsea isije ikawa tumepigwa tena kama Cucurela
Brighton wanatuchezea washenzi hao kila siku wanatuuzia garasha
 
Nilishawahi kusema humu Brighton ina wachezaji wa kawaida ila inabebwa na mfumo wa kocha sasa huyu Caicedo tuliomchukua tuone uwezo wake pale chelsea isije ikawa tumepigwa tena kama Cucurela
Ila pia mfumo leo alioutumia Pochettino hauendani na wachezaji tulionao
Angesimama kwenye 4-2-3-1 badal ya kutumia 3-4-3
 
Unajua baada ya Caicedo na Lavia kufanikiwa kujiunga na Chelsea walifanya sherehe kubwa na ndugu na marafiki walioko London. Ndio maana Kocha alikuwa akiwajaribu kuwalinda kuwa walikuwa na hectic week. Sasa ile hangover ya sherehe bado haijaisha. Kocha alitakiwa asingemuweka hata benchi
 
Kitu pekee ambacho Pochettino lazima afanye ili kubaki na kibarua chake Chelsea ni kuweza kugundua kikosi chake cha kwanza haraka iwezekanavyo kabla ya kuchelewa. Ikiwa atachelewa, ninaona kwamba mlango na njia ambayo Potter alipitia inangojea apitie.
1692573121724.png
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom