Tulivyokuwa wapuuzi utakuta huyu mtoto tunamtoa kwa mkopo halafu sterling anabaki Darajani!
Aisee huyu Dogo ni kama siyo 18yrs. Hizi siyo touches za mtu mwenye umri huo.
Mechi ya kwanza tu nilishamuona huyo na ndio maana niliandika sehemu kuwa Pochetino akiruhusu Gabriel, Maatsen, Andrey and Cesare waende loan hawajui walitendalo, na katika hao wanne, Gabriel is the best. Labda kama tutawasajili wazuri zaidi yake.
Angelo hata Madueke haoni ndani, jicho la kijana liko kwenye build up ya goli tu na yuko very clinical kwenye kutoa pasi za uhakika. Kweli ile game ya kwanza kuna mpira alimpa Stereling nikakumbuka majonzi ya msimu uliopita wa kupoteza hovyo chances tunazopata.
Sterling hastahili hata kuwepo Chelsea. Huyo auzwe tu Uharabuni. Goli lile la Chilwell Gabriel alitoa assists kali baada ya kugongeana mpira vizuri.
Mwanzo wakati wanamsajili walimuongelea sana kuwa ni winga mchezeshaji ila sikutil;ia maanani sana kwa sabab kwanza ni kinda wa miaka 18 tu pili hakuoneonekana na timu kubwa kwenye scouting yao.
Sasa tunashuhudia alivyo mjanja kuwachezesha wenzake pale mbele. Naomba Mungu permit ya ke isikataliwe kama ya Andrey Santo januari. Atafikisha miaka 19 December 2023 na hivyo uwezekanoi wa kupewa permit ni hadi January labda factor zingine zimbebe.
Kuna uwezekano wa kwenda kwa mkopo baadaye, labda Brazil, RC Strasbourg, au mahali pengine. Haiwezekani kuhitimu kupata kibali cha kufanya kazi cha Uingereza (labda kwa sababu maalum) kwa wakati huu.
Licha ya umri wake mdogo (hatafikisha miaka 19 hadi mwishoni mwa Desemba mwaka huu), Ângelo tayari ana uzoefu mkubwa wa soka, akiwa amecheza zaidi ya mechi 100. Ndiye mchezaji mwenye umri mdogo zaidi katika historia ya Série A ya Brazil na pia ndiye mfungaji mabao mdogo zaidi katika historia ya Copa Libertadores.
Tunategemea atakuja kufanya wonders pia kwenye EPL na michuano mingine mikubwa ya Uingereza na Ulaya kwa ujumla