Rockcity native
JF-Expert Member
- Dec 31, 2012
- 2,174
- 1,460
Hivi chelsea kuna kocha gan aliyemvumbia mchezaj bora wa dunia? Uliza wenger alipomtoa george opong weah tena alimtoa direct africa.
Hivi chelsea kuna kocha gan aliyemvumbia mchezaj bora wa dunia? Uliza wenger alipomtoa george opong weah tena alimtoa direct africa.
Hivi chelsea kuna kocha gan aliyemvumbia mchezaj bora wa dunia? Uliza wenger alipomtoa george opong weah tena alimtoa direct africa.
George Weah alikuwa mchezaji bora wa dunia mwaka 1995. Wakati George anakuwa mchezaji bora wa Dunia alikuwa mchezaji wa AC Milan. Wenger alimtoa Weah, huku Afrika na kumpeleka As Monaco, hata hivyo miaka kadhaa ilipita ndipo Weah akaja kuwa mchezaji bora wa Dunia, akiwa AC Milan ambayo ilikuwa bingwa wa UEFA CHAMPIONS LEAGUE mwaka 1994. Ili kuweka kumbukumbu sawa sawia; AC MILAN walichukua ubingwa kwa kuifunga Barcelona goli 4.
Sasa ndo maana Wenger anaitwa mwalimu wa watoto!
Kila mwalimu ana jukumu lake; mwalimu wa chekechea anaandaa watoto kuingia shule ya msingi, wa msingi anaandaa watoto kwenda sekondari, wa sekondaari anaandaa vijana kwenda chuoni na hatimaye kujitegemea.
Sasa ndo maana Wenger anaitwa mwalimu wa watoto!
Kila mwalimu ana jukumu lake; mwalimu wa chekechea anaandaa watoto kuingia shule ya msingi, wa msingi anaandaa watoto kwenda sekondari, wa sekondaari anaandaa vijana kwenda chuoni na hatimaye kujitegemea.
Mkuu Rockcity native nimecheka sana hiyo hoja yako inachekesha..ha ha haha.
Sasa turudi kwenye mpira wa kitaalamu kidogo wandugu;
cc. Ntuzu, Mentor, Rockcity native, Siziga, Dully jr, Nzi etc.
Nataka tujadili umuhimu wa "kiungo mkabaji" kwenye timu.
Waingereza wanamwita; Defensive midfielder au holding midfielder. Wazee wa samba; Brazil wanamwita volante.
Arsenal Fc walichukua mara ya mwisho ubingwa wa Uingereza(England) msimu wa 2003-2004.
Kilichochangia Arsenal FC kuchukua ubingwa huo enzi hizo ni kuwa na viungo wazuri, hasa kuwa na huyu "kiungo mkabaji" enzi hizo Patrick Vieira#4, the captain.
Vieira alikuwa anacheza mbele kidogo ya mabeki, jamaa mrefu, alikuwa na nguvu na uwezo wa kupokonya mipira kutoka mguuni mwa adui. Vieira alikuwa pia mbabe, wapinzani walimwogopa mfano; Uadui wake na Roy Kean(man utd).
Pia Arsenal wakampata kiungo mwingine mzuri Gilberto Silva #19. Jamaa pia alikuwa fundi sana wa kucheza jukumu la volante. Ndo maana hata kwenye timu ya taifa ya Brazil kiungo mkabaji alikuwa yeye Gilberto enzi akicheza Arsenal Fc. hata alipohama Arsenal kwend Olympiakos ya Ugiriki bado aliendelea kucheza kwenye timu ya taifa. Tangu wachezaji hao waondoke Arsenal ikashindwa kuchukua mataji. Umuhimu wa Kiungo Mkabaji.
Nini kinafanya Manchester City msimu huu kutisha sana? Je, ni Aguero na Negredo? Jamaa wanafunga sana magoli bila kusahau Dzeko. Hata kiungo fundi Yaya Toure anafunga sana. Lakini msimu huu wamempata "kiungo mkabaji" hatari sana. Jamaa mpira wake hauvutii lakini kazi anaijua,FERNANDINHO #25. Huwa anacheza mbele ya Vicent Kompany na Lescott. Jamaa anazuia mipira mingi isiwakute mabeki wake. Mashambulizi mengi pia huanzia kwake na kwenda ama pembeni kwa Navas na Nasri au mbele kidogo kwa Yaya. Kiungo mkabaji ni muhimu sana kwenye timu hii pia.
Real Madrid Cf chini ya Jose Mourinho jukumu hilo la kiungo mkabaji alikuwa nalo "the engine" Sami Khedira.#6. Mpira wake haueleweki lakini ndo roho ya timu.
Barcelona CF wanaye jamaa yao. Sergio Busquets huyu jamaa pia hufanya vituko vingi uwanjani. lakini vina faida kwa timu.
Sisi CHELSEA FC:
Kiungo mkabaji ndo msingi wa mafanikio yetu: Msimu ule wa 2004-2005, Claude Makelele #4. Alicheza kwa mafanikio katika sehemu hiyo kiasi kwamba hakuna mtu kwenye ligi yeyote Ulaya amewahi kucheza kwa mtindo wake. Viungo wengi wazuri wa ukabaji wametokea Ulaya; lakin hakuna aliyefanya shughuli aliyokuwa anafanya Claude Makelele. Msimu mzima Chelsea ilifungwa magoli 15 tu. Mechi 38 timu ilifungwa magoli 15 tu. Mafanikio yote hayo yalitokana na uimara wa Claude Makelele pale kati kwenye jukumu lake la Defensive Midfielder "the makelele style". Makelele alitoka Real Madrid; Alikuwa ameisaidia sana Real kwenye ubingwa mbalimbali; lakini tangu walipomfukuza Makelele hawajawahi kuchukua UCL. jose Mourinho anajua umuhimu wa "kiungo mkabaji" ndo maana alipofika Real alimtengeneza Sammy Khedira kwenye jukumu hilo, jamaa naye anaweza. REal ilifika nusu fainali 3 za UCL chini ya Mou, kwa sababu ya uimara wa Khedira;
Mkuu Rockcity native nimecheka sana hiyo hoja yako inachekesha..ha ha haha.
Sasa turudi kwenye mpira wa kitaalamu kidogo wandugu;
cc. Ntuzu, Mentor, Rockcity native, Siziga, Dully jr, Nzi etc.
Nataka tujadili umuhimu wa "kiungo mkabaji" kwenye timu.
Waingereza wanamwita; Defensive midfielder au holding midfielder. Wazee wa samba; Brazil wanamwita volante.
Arsenal Fc walichukua mara ya mwisho ubingwa wa Uingereza(England) msimu wa 2003-2004.
Kilichochangia Arsenal FC kuchukua ubingwa huo enzi hizo ni kuwa na viungo wazuri, hasa kuwa na huyu "kiungo mkabaji" enzi hizo Patrick Vieira#4, the captain.
Vieira alikuwa anacheza mbele kidogo ya mabeki, jamaa mrefu, alikuwa na nguvu na uwezo wa kupokonya mipira kutoka mguuni mwa adui. Vieira alikuwa pia mbabe, wapinzani walimwogopa mfano; Uadui wake na Roy Kean(man utd).
Pia Arsenal wakampata kiungo mwingine mzuri Gilberto Silva #19. Jamaa pia alikuwa fundi sana wa kucheza jukumu la volante. Ndo maana hata kwenye timu ya taifa ya Brazil kiungo mkabaji alikuwa yeye Gilberto enzi akicheza Arsenal Fc. hata alipohama Arsenal kwend Olympiakos ya Ugiriki bado aliendelea kucheza kwenye timu ya taifa. Tangu wachezaji hao waondoke Arsenal ikashindwa kuchukua mataji. Umuhimu wa Kiungo Mkabaji.
Nini kinafanya Manchester City msimu huu kutisha sana? Je, ni Aguero na Negredo? Jamaa wanafunga sana magoli bila kusahau Dzeko. Hata kiungo fundi Yaya Toure anafunga sana. Lakini msimu huu wamempata "kiungo mkabaji" hatari sana. Jamaa mpira wake hauvutii lakini kazi anaijua,FERNANDINHO #25. Huwa anacheza mbele ya Vicent Kompany na Lescott. Jamaa anazuia mipira mingi isiwakute mabeki wake. Mashambulizi mengi pia huanzia kwake na kwenda ama pembeni kwa Navas na Nasri au mbele kidogo kwa Yaya. Kiungo mkabaji ni muhimu sana kwenye timu hii pia.
Real Madrid Cf chini ya Jose Mourinho jukumu hilo la kiungo mkabaji alikuwa nalo "the engine" Sami Khedira.#6. Mpira wake haueleweki lakini ndo roho ya timu.
Barcelona CF wanaye jamaa yao. Sergio Busquets huyu jamaa pia hufanya vituko vingi uwanjani. lakini vina faida kwa timu.
Sisi CHELSEA FC:
Kiungo mkabaji ndo msingi wa mafanikio yetu: Msimu ule wa 2004-2005, Claude Makelele #4. Alicheza kwa mafanikio katika sehemu hiyo kiasi kwamba hakuna mtu kwenye ligi yeyote Ulaya amewahi kucheza kwa mtindo wake. Viungo wengi wazuri wa ukabaji wametokea Ulaya; lakin hakuna aliyefanya shughuli aliyokuwa anafanya Claude Makelele. Msimu mzima Chelsea ilifungwa magoli 15 tu. Mechi 38 timu ilifungwa magoli 15 tu. Mafanikio yote hayo yalitokana na uimara wa Claude Makelele pale kati kwenye jukumu lake la Defensive Midfielder "the makelele style". Makelele alitoka Real Madrid; Alikuwa ameisaidia sana Real kwenye ubingwa mbalimbali; lakini tangu walipomfukuza Makelele hawajawahi kuchukua UCL. jose Mourinho anajua umuhimu wa "kiungo mkabaji" ndo maana alipofika Real alimtengeneza Sammy Khedira kwenye jukumu hilo, jamaa naye anaweza. REal ilifika nusu fainali 3 za UCL chini ya Mou, kwa sababu ya uimara wa Khedira;
Essien alijaribu kutaka kufikia kiwango Km cha Makelele lkn majeruhi yakamuandama sn na pia Obi bado hajamfikia Makelele na Ramires yeye anasifa ya wepesi kwa kwenda mbele na kukaba ni mzuri lkn wote hawa bado hawajamfikia Makelele!
Kwa game ya City na Chelsea Ningependa Ramires acheze na kwa uwezo Wa Ramires Fenandinho hawezi kumzibiti. Ningependa kumuona Ramires na Oscar pale Kati wakisaidiwa na kiuongo mmoja mkabaji Km atakua Obi au Luiz au Matic au Essien au Lampard!
Lampard kwenye kukaba anajitahidi sn na ni mhamasishaji sn uwanjani!
kimsingi hakuna nafasi nayo ihusudu kama holding midfilder huku kwetu kitaa tunawaita wakata umeme yani akiamua kukata umeme anakata kweli. Na katika maisha yangu ya soka bila kuficha hakuna mtu naye mkubali ktk eneo hilo kama makelele. Huyu jamaa alikua havuki mstari wa kati alikua hana shobo na shughuli ambazo hazimuhusu kama kushambulia au ku assist kama alex song. Dunia ya sasa w2 hawa wamekua adimu sana dunia ya leo imetuletea box 2 box midfilderz ambao wanachanganya mambo.. Kwa dunia ya sasa kidogo namhusudu lucas leiva wa livepool. Kwanza sifa mojawapo ya mkata umeme hatakiwi sana kuonekana ovyo ovyo had kwnye matukio muhimu.
Ntuzu mimi pia nampenda sana Makelele; hata jana nilimzungumzia huyu "legend" wetu kama unakumbuka; hakuna mtu anayeweza kucheza kama yeye; lakini kwa kweli John Obi Mikel anacheza vizuri sana hapo kati kuliko kiungo yeyote mkabaji kwa timu yetu; Ramires ni box to box midfielder; Lakini Obi yeye ni kati tu; na ndo maana pasi zake nyingi ni square pass kushoto au kulia na pasi za nyuma kwa mabeki ili kutengeneza "shape" ya timu.
Ramires faida yake ni kwamba tukicheza na timu kama City ni kwamba jamaa zetu hawatapumzika; tutakuwa tunapushi muda wote; Lakini kwa sababu Matic amekuja nafikiri pale kati patabadilika; jamaa pia ni fundi sana. Chelsea imeanza kuiva; Nakuambia Ntuzu ubingwa wa msimu huu ni wetu. Mo Salah amekuja kuongeza vitu.
Mkuu nakubaliana na Wewe ktk hoja zako!
Na nikweli Obi pale kati ameanza kumzidi Essien, yupo vizuri sn! Na sijamfatilia sn Matic kule Benfica Kwahiyo uzuri wake sn bado sijaufahamu! Ila Ningependa hiyo game ya City na sisi pale Kati aanze Obi na Ramires na Oscar. Alafu anaweza akapumzishwa Oscar akaingia Luiz au Matic au Lampard!
Kimsingi kuanzia 1998 mpaka 2012 Germany wamekua wanashiriki World cup na Euro bila kuchukua kombe! Na wanakomea hatua za mbali kabisa! Km sio Fainal basi ni nusu Fainal au Robo Fainal! Ila hawana bahati! Kwa ulaya hii ni timu moja ngumu sn! Ila ndo ivyo haina wakata Umeme mahili Km Makelele na Gatuso au Emerson
umenikumbusha huyu mtu emerson. Jamaa alimis wodcup ya 2002 kimasihara. Alikua anajaribu kufanya kazi za magolikipa wakiwa kambini na tim ya taifa matokeo yake akapalamia mlingoti akaumia. Hapo ndo scolari from nowhre akamleta mkata umeme mpya gilberto da silva au pale highbury 2likua 2namuita invisible wall au mchimba kokoto.