Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea kesho anamfunga City
Hakuna bingwa anayejihangaisha kwa mechi ambazo hazina tija tena kwake
Barca leo anafungwa 2+ nyumbani kwake hawaangaiki ya nini wakati tayari ni mabingwa
Napoli mechi zake baada ya kutangazwa bingwa anafungwa kirahisi tu
Mechi za Newcastle na Man U pia hazina umuhimu mkubwa kwani hizo timu zinahitaji droo tu ili kufuzu top 4
Unaweza ukashangaa kipofu akaokota pts 6 katika 9
 
Tunamaliza ligi kinyonge sana kama ndugu zetu Arsenal. Kuna nafasi 11 tulikaa muda mrefu sana, Potter angejitahidi kipindi kile ninauhakika tungeingia top4.

Yote kheri, tukifanya vibaya msimu huu...msimu ijayo tutafanya vyema.
 
EPL ni mbio za marathon
Bingwa huwa haongozi mwanzoni atachoka
Arteta hakujua hilo, kakaza kuongoza ligi hadi akawachosha vijana.
Sasa city mzoefu anakuja kuovertake dakika za mwisho na kubeba ubingwa akiwa na mechi 3 mkononi
 
Tulipocheza na city safari ya mwisho kwenye ligi
Backline ya 4 ilikuwa na

Cucu -- Kou --- TS ----- Azpilicueta - Tukafungwa 1-0


Kwenye FA 3rd round

Hall --- Kou ---Hump --- Chalo Tukafungwa 4-0

Leo mabeki watano wako kitandani
  1. James
  2. Badiashile
  3. Chilwell
  4. Cucurela
  5. Koulibaly - 25%
Basi kinyonge twende na hawa hapa

Azpilicueta ---Hall ----Fofana ----Chalobah

Au tucheze backline ya 3

Hall -----Fofana -----Chalobah

Full line up ya 4-3-3

Mudryk --------Felix ------- Madueke

Enzo ------ Kovacic--------Galagher

Hall ----Koulibally ---- Fofana ----Chalobah
 
Lampard asema aliambia Chelsea imsajili Haaland ila akapewa Lukaku
 
Fofana alipohojiwa na SkySports kuhusu performance ya Chelsea msimu huu alisema

"it’s the players, it’s the club, it’s everybody. It’s not just the coaches coming and going, it’s not just the [owner], it’s not just the new players. It’s everybody. We are the same team. When it’s bad, everybody is bad"
1684644630585.png
 
Lazima tuangalie tupate burudani sio mechi ya kukosa kuangalia kama shabiki wa mpira na timu.

Hii mechi ya leo Pochetino anatakiwa ahudhurie, aangalie madhaifu ya timu na ajifunze pia mwenzake Pep anafanya nini kimbinu.
Pochettino ni sikio la kufa hakidhi vigezo na hana mbinu zozote za kuifundisha klabu kubwa kama Chelsea FC.

Mashabiki wa Chelsea FC tujiandae kisaikolojia kwa kuwa nafasi ya 7-10 kimsimamo EPL 2023/2024..

Tuombeane uzima, nimekaa pale .

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Sasa tutafanyaje chief na ndio kocha wetu mtarajiwa.

Binafsi naona makocha wengi wa epl ni wabovu wameshindwa kumchallenge Pep.

Poche hana uwezo wa kuchukua epl mbele ya Pep.

Kama ile liverpool moto imechukua ubingwa mara 1 mbele ya Pep sembuse hii the blues ya kuunga unga kwa solotepu.

The blues tungempata kocha kama Morinyo au Conte tukawapa rungu la usajili wanavyotaka wangebeba epl mbele ya Kipara.
Ukweli mchungu sana huu kwa 100%

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Pep ametuonea huruma sana, angepanga full mziki tungefungwa nyingi sana.

Tunacheza ovyo sana, kivivu, legelege, kama vile wachezaji wanalazimishwa kucheza, yaani tunacheza bora liende.
Watu mnapenda sana kujitafutia kufa mapema, unaanzaje kupoteza muda kushuhudia Chelsea FC mbovu namna hiyo ukaacha kuangalia;

Yanga FC.

Kula mziki.

Kuangalia muvi.

Kutembelea mbuga za wanyama.

Kula upepo beach.

Kupiga stories za maisha na Watu mbali mbali.

Kukaa na kuenjoyi na familia yako.

Kula Pisi Kali?

Ebu furahieni uhai mliopewa na Mungu badala ya kujitakia;

BP.

KISUKARI.

VIDONDA VYA TUMBO.

SONONA.

KUGONGWA NA GARI.

Mkajifia bure kabla ya siku zenu

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom