Dormant Account
JF-Expert Member
- Apr 5, 2022
- 11,307
- 32,791
Cheltako mpo 





Mimi ni mojawapo mkuu nisiemkubal kabsa huyu Bwa PotaKupanga kikosi ni jambo moja
Kikosi kucheza kwa mfumo, mbinu na style za uchezaji kumzidi mpinzani ni jambo lingine.
Pamoja na sajili tulizofanya leo nakiri kusema Potter anategemea UWEZO BINAFSI wa mchezaji mmoja mmoja ashinde mechi
Ukiangalia timu inavyocheza sioni mbinu za kocha, sioni patterns za uchezaji ambazo zinawafanya wachezaji watekeleze vyema uwezo na majukumu yao katika nafasi zao uwanjani.
Mi naona timu yetu inacheza aina ya soka linaloitwa CHANGANYIKENI uwanjani.
Sioni uwezo/mbinu za mwalimu katika uchezaji wa timu.
Timu inaweza isiwe na Wachezaji wenye uwezo mkubwa lakini wakacheza kimfumo na kimbinu zaidi wakashinda Mechi.
THE BLUES kwa sasa tuna wachezaji wakubwa/Uwezo mkubwa lakini mbinu za Kocha hakuna uwanjani.
Hata Potter anavyong'ang'ania kuwapanga Harvetz na Mount, tulitegemea wanapangwa kimbinu zaidi, mchango wao ukaonekana katika kupata matokeo, lakini tunaona kinyume chake wanacheza ovyo zaidi.
Na hapa Tunapiga kelele Jao Felix na Fofana waanze mbele ya Mount na Harvetz.
Je waanze kikosini kuonyesha uwezo wao binafsi uwanjani au watekeleze mbinu za mwalimu uwanjani kupelekea timu kupata matokeo?
MWISHO:- Binafsi naamini mafanikio ya uwezo binafsi wa mchezaji ndani ya Mfumo na mbinu bora za Kocha uwanjani
Potter asijifiche kwenye kivuli cha maingizo mapya ya wachezaji bali tunataka kuona wachezaji wakiingia kwenye mbinu zake.
Bila mfumo mzuri
Bila flow/Patten nzuri za uchezaji
Bila mbinu bora za Kocha
Hawa wakina Mudryk wataingia kwenye mtego ule ule SAME PLAYERS, SAME PROBLEMS.
Huyu akili hana wamuache aondoke
Na mimi naamini juu ya hayo uliyosema,Binafsi naamini mafanikio ya uwezo binafsi wa mchezaji ndani ya Mfumo na mbinu bora za Kocha uwanjani
Bila mfumo mzuri
Bila flow/Patten nzuri za uchezaji
Bila mbinu bora za Kocha
Hawezi kuzid €60 huyuHivi thamani ya Mount sokoni kwa sasa imefika bei gani €?
Wachaze wa kiingereza wana akili za hovyo sana yani huyu mount ni kirusi asiondoka bado tutaeendelea kustruggle tuHuyo Mount auzwe tu, Waingereza wakikosa namba kwenye timu za England wanaanza figisu za chinichini
Sasa yeye anataka mshahara mkubwa wakati kiwango chenyewe cha manati.
Alafu ni bonge la selfish, anataka kung'aa yeye tu hivyo anaweza haribu move uwanjani ili mwenzie asi-shine.
Uyo kai nae apigwe spana tu maana kashapewa muda sana lakini habadilikiHivi Havertz naye ni mwingereza?
Sio wenyeji direct, sheria haisemi wenyeji bali inatumia home grownHivi si kuna ile sheria ya FA kunatakiwa kuwe na idadi flani ya wachezaji wa kiingereza lazima wacheze kwenye kikosini?
Hiyo sheria ni ya first team ya wachezaji 25, sheria haimlazimishi kocha acheze au awepo kwenye bench ila inalazimisha awepo kwenye first teamOky nimekupata, kwahiyo chief hakuna sheria inayolazimisha homegrown waanze 1st eleven au lazima wacheze kwenye kila mechi?
Hapo sawa.
Kwahiyo Potter kumngangania Mount 1st eleven kumbe ana lake jambo.
Mi nilidhani kuna sheria inayolazimisha mchezaji wa kiingereza lazima aanze 1st eleven.