Romeu yuko Valencia, anacheza kiungo wa kukaba; lakini tayari tumesajili "mtu mzima" Nemanja Matic na kuna fundi Obi Mikel kwa hiyo ni vigumu dogo kurudi;
Kuhusu nafasi ya Marko Marin anayecheza Sevilla CF ni vigumu pia, kwa sababu tayari yuko majeruhi amekuwa majeruhi mara kwa mara ingawa kwa kweli dogo ni fundi sana. Sasa nafasi yake Chelsea ni ndogo; kwa sababu pembeni kuna watu wengi wa maana; Willian, Schurrle, Hazard, Mata, Ramires; ushindani ni mkubwa:
Ba mchezaji mzuri, lakini Chelsea ni timu kubwa;Ba ni mchezaji mzuri kwa timu za kawaida kama Newcastle, Everton, Westham ambako atapata nafasi ya kucheza kila mechi kama anavyofanya Lukaku.
Chelsea ni timu ya Mataji; hivyo inahitaji wachezaji ambao lengo lao ni kushinda mataji si kucheza ili kujiburudisha; Hua namkumbuka sana Ballack #13, huyu bwana anapenda sana kushinda; Kwa sasa tunahitji kuendelea kuwa na Lampard na Terry hata kama watakuwa wanacheza dakika chache ili vijana wapate busara na akili za hawa mafadha..