Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

True and facts (Hakuna anayepinga hayo), ila Boehly bado mimi namlaumu kwa kuimpliment vision kwa approach mbaya. Mimi nalia na transition period haikuwa nzuri sana, TT alipaswa kuondoka kabla ya kufanyta matumizi makubwa kama yale.
  1. Auba ni wa TT
  2. Fofana ni wa TT
  3. Sterling ni wa TT
  4. Koulibally ni wa TT
  5. Zakaria ni wa TT
  6. Cucurella ni wa TT japo GP alikuwa naye Brighton kwa hiyo anamfahamu vizuri
Ningekuwa mimi Boehly ningemtoa kafara TT kabla ya usajili ili GP aje kwua mshauri mkuu kwenye usajili
Pia angetafuta mbadala wa Marina na nafasi zote nyeti kabla ya kufanya usajili. Transition ya rebuilding ingekuwa soft, sasa inakuwa hard kwa sababu ya hayo makosa
Hayo yameshafanyika hayawezi kubadilishwa. Tujiandae kwa misimu miwili kuwa wavumilivu kitu ambacho hatujazoea.
 
Wote waliondoka bila kutaka kwa lengo la kuanza na watu wanaounga maono ya bosi na mmiliki mpya.
Tena walitudanganya Marina angeshiriki kwenye usajili hadi dirisha liishe ila hicho kitu hakikutokea.
Ukweli ni kwamba wote tunataka Boehly afanikiwe na maono yake ila pia ukweli unabaki pale pale. Wamarekani huwa wanapapara na wanajifanya wao wajuaji kuliko wengine. Kafanya kazi zote za President wa team, Spoprting Director, Technical Director, Head Coach zote na pande zote kaboronga. An maono mazuri ila approach ya kuitekeleza hayo maono ni hovyo hovyo, ni muda tu whose know when hili janga litatibika. Hayo niliyoyasema yalikuwa yanaepukika ili trasnition period iwe nzuri. Wale akina Marina na wenzake wangewekwa vipora hadi successors wazuri wapatikane, pili TT asingefukuzwa hadi maono yake yaliyowekezwa kwenye usajili yafanikiwe au tusingepotez amil karibia 300 kusajili kwa kocha asiyekaa. That is a big blunder kwenye management hasa ya mpira kwenye ligi kama ya Uingereza. Mashabiki tutaumia hadi tukome. Tuwe karibu tu na mashabikli wa Arsenal na Liverpool ili watupe uzoefu wa kuvumilia kwa sababu Chelsea itachukua misimu mingi kurudi ulingoni
Kwahyo Tajiri kafanya Hadi na kazi ya uheadcoach aisee umetisha Sana mkali
 
Kumbuka maono yaliyopaswa kutekelezwa pale Chelsea ni ya Boehly na siyo Tuchel. Hivyo baada ya kutofautiana mitazamo, ilikuwa ni lazima Tuchel aondoke.

Mashabiki lazima tuujue ukweli kuwa Chelsea ya miaka ya 2011 - 2022 ilikuwa imejengwa on short term success. Hatukuwa na team ya kushindana hata misimu miwili mfululizo.
Mfano tulichukua champions league 2012 tukamaliza nje ya top four EPL.

2015 tukabeba EPL msimu uliofuata tulimaliza nafasi ya 10.

2017 tukabeba EPL msimu uliofuata tukamaliza nje ya top 4.

Inconsistency za namna hii zimekuwa zikiendelea msimu baada ya msimu.

Pia hata tunapoingia top four kuna kuwa na tofauti kubwa sana ya points kati yetu na wale top 2 kwenye ligi (Man City na Liverpool)

Katika kipindi hicho hicho ambacho tumekuwa na inconsistency, tumetumia hela nyingi kuwanunua Lukaku, Morata, Timo Werner, Tiemoe Bakayoko, Barkley, Ziyech, Pulisic, Sterling, Kepa Alizabaraga, Drink Water na wengineo ambao wamekuwa flop.

Kwa maana hiyo kuna ulazima wa kubadili namna ya uendeshaji club. Na suluhisho ni kujenga team ambayo inaweza kudeliver in a long term. Team haiwezi kujengwa ndani ya wiki sita. It takes time.

Graham Potter hajapata hata preseason moja na team.
Hajashiriki transfer window yoyote na Chelsea.
Ameingia clubuni wakati ambapo kuna mechi nyingi na wachezaji muhimu wakiwa injured.

Mimi nadhani tumpe GP transfer window mbili angalau. Hii ya January na ile ya Summer alafu tuone atakavyounda timu. Baada ya hapo angalau itakuwa halali kumhukumu.

Tukumbuke hata Guadiola msimu wake wa kwanza na City mambo hayakuwa marahisi. Kidogo tu timu isiingie top four.
Exactly
 
True and facts (Hakuna anayepinga hayo), ila Boehly bado mimi namlaumu kwa kuimpliment vision kwa approach mbaya. Mimi nalia na transition period haikuwa nzuri sana, TT alipaswa kuondoka kabla ya kufanyta matumizi makubwa kama yale.
  1. Auba ni wa TT
  2. Fofana ni wa TT
  3. Sterling ni wa TT
  4. Koulibally ni wa TT
  5. Zakaria ni wa TT
  6. Cucurella ni wa TT japo GP alikuwa naye Brighton kwa hiyo anamfahamu vizuri
Ningekuwa mimi Boehly ningemtoa kafara TT kabla ya usajili ili GP aje kwua mshauri mkuu kwenye usajili
Pia angetafuta mbadala wa Marina na nafasi zote nyeti kabla ya kufanya usajili. Transition ya rebuilding ingekuwa soft, sasa inakuwa hard kwa sababu ya hayo makosa
Hao mbadala unaowasemea sio rahisi kuwapata Kwa huo muda mfupi mzee
 
New Structure /New look of recruitment team ambao washatangazwa mpk sasa
●Laurence Stewart (Technical Director)
Katokea Monaco
●Joe Shields (Co-Director of Recruitment and Talent ) katokea Southampton
●Paul Winstanley (Director of Global Talent and Transfers) katokea Brighton n Hove Albion.
●Kyle Macauley huyu atakuwa anaact kama link/chanel kati ya Potter Backroom staff na Recruitment team-Huyu alikuja na Potter.


Anayetegemea kutanganzwa mda wowote ni Christopher Vivel pia na yeye ni Technical Director kutoka RB liepzig
 
New Structure /New look of recruitment team ambao washatangazwa mpk sasa
●Laurence Stewart (Technical Director)
Katokea Monaco
●Joe Shields (Co-Director of Recruitment and Talent ) katokea Southampton
●Paul Winstanley (Director of Global Talent and Transfers) katokea Brighton n Hove Albion.
●Kyle Macauley huyu atakuwa anaact kama link/chanel kati ya Potter Backroom staff na Recruitment team-Huyu alikuja na Potter.


Anayetegemea kutanganzwa mda wowote ni Christopher Vivel pia na yeye ni Technical Director kutoka RB liepzig
Mkuuu sorry hii habari umeitoa wap?
 
Mkuuu sorry hii habari umeitoa wap?
Hapo nimejuisha habar zote tangu walipoanza kutangazwa,.



 
New Structure /New look of recruitment team ambao washatangazwa mpk sasa
●Laurence Stewart (Technical Director)
Katokea Monaco
●Joe Shields (Co-Director of Recruitment and Talent ) katokea Southampton
●Paul Winstanley (Director of Global Talent and Transfers) katokea Brighton n Hove Albion.
●Kyle Macauley huyu atakuwa anaact kama link/chanel kati ya Potter Backroom staff na Recruitment team-Huyu alikuja na Potter.


Anayetegemea kutanganzwa mda wowote ni Christopher Vivel pia na yeye ni Technical Director kutoka RB liepzig
Chelsea tupo kwenye mikono salama
 
Neil Bath’s role at Chelsea as academy director has changed to director of football development and operations. Role has an involvement in first team matters.

- @JacobSteinberg
 
Hao mbadala unaowasemea sio rahisi kuwapata Kwa huo muda mfupi mzee
Mistake ya kumuacha Rudiger kuondoka pia inatutafuna , yule mwamba alikuwa nguzo sana kule nyuma akisaidiana na akina babu silva na Azpi ,akiwepo Chillwell na James ,ukuta ilikuwa na stability sasa koulibay ,Chalobah na cucurela bado wana wenge sana ,sijui wanafunza miguuni wanachocheza hakieleweki ,
 
Mistake ya kumuacha Rudiger kuondoka pia inatutafuna , yule mwamba alikuwa nguzo sana kule nyuma akisaidiana na akina babu silva na Azpi ,akiwepo Chillwell na James ,ukuta ilikuwa na stability sasa koulibay ,Chalobah na cucurela bado wana wenge sana ,sijui wanafunza miguuni wanachocheza hakieleweki ,
Kweli aisee kina marina na uongozi uliopita cjui walikwama nn kumuongezea alichokitaka
 
New Structure /New look of recruitment team ambao washatangazwa mpk sasa
●Laurence Stewart (Technical Director)
Katokea Monaco
●Joe Shields (Co-Director of Recruitment and Talent ) katokea Southampton
●Paul Winstanley (Director of Global Talent and Transfers) katokea Brighton n Hove Albion.
●Kyle Macauley huyu atakuwa anaact kama link/chanel kati ya Potter Backroom staff na Recruitment team-Huyu alikuja na Potter.


Anayetegemea kutanganzwa mda wowote ni Christopher Vivel pia na yeye ni Technical Director kutoka RB liepzig
Asante kwa updates, angalau inatupa matumaini kwamba nyuma ya pazia kazi inaendelea kuboreshwa. Impack tutegemee sio chini ya misimu miwili
 
Mistake ya kumuacha Rudiger kuondoka pia inatutafuna , yule mwamba alikuwa nguzo sana kule nyuma akisaidiana na akina babu silva na Azpi ,akiwepo Chillwell na James ,ukuta ilikuwa na stability sasa koulibay ,Chalobah na cucurela bado wana wenge sana ,sijui wanafunza miguuni wanachocheza hakieleweki ,
Mistakes ya Rudiger ni kwa akina Marina kuchelewa kumpa mkataba hadi tukapewa ban
 
CHELSEA FC NA PROJECT UCHWARA

1. Koulibaly - Mzee (Uwezo umeshuka)

2. Azip - Mzee (Uwezo umeshuka)

3. Auba - Mzee (Uwezo umeshuka)

4. Silva - Mzee (tegemezi)

5. Jorgnho - Mzito, Hana kasi, hawezi kukaba wala kupora mipira

6. Cheek - Uwezo wake ni kucheza crystal Palace/ Kubwa jinga

7. Cucurela - Uwezo wake mdogo, ana mawenge, anatia huruma

8. Kante - Majeruhi Yasioisha

9. Kovacic - Majeruhi Yasioisha

10. Sterling - Mchezaji Waruwaru, faida yake uwanjani ni ndogo kuliko hasara

11. Pulisic - Mtumishi hewa

12. Ziyech - Tumeshindwana

13. Harvetz - Tunapotezeana muda

14. Zakaria - Tatizo la kutokuwa na mechi fitness
Nawatetea kwa nguvu zote hawa wachezaji watano
  1. Koulibaly bado hajazoea kwa vile hajawahi kucheza backline ya 3, kwenye backline ya 4 aliyocheza Kou kacheza vizuri japo sio sana lakini kwenye hii ya 343 ndio anaboronga sana
  2. Cucurella ni wale wachezaji wanaochukua muda kuzoea ila pia poor form ya timu imemuadhiri
  3. Sterling style yake ya uchezaji ni ya kimlenda ila anayo vitu vingi vya ku-offer. mfano Sterling ni mzuri kwenye kucreate chances na kufunga ila hapati huduma stahiki, hivyo hivyo kwa Auba.
  4. Havertz ni muadhirika wa poor service providers walio pale katikati. Hata hao washambuliaji wengine kama akina Pulisic (Japo Pulisic hata-offer vitu vingi sana lakini abdo angetupa magoli 10+ kama tungekuwa na muunganiko mzuri wa timu pale katikati)
Wachezaji ambao naamini hawatatufaa tena kwenye first team ni
  1. Azpi
  2. Jorginho
  3. Cheek
  4. Kante - Kwa sababu ya majeruhi - anavyozidi kuzeeka anaku more vulnerable to injuries
  5. Kovacic - Kachoka
  6. Ziyech - Ana uwezo mkubwa ila kaamua kuwa mjeuri
  7. Mendy - sidhani kama atarudi kwenye form yake ya 2020/21 na 2021/22 ( Hajitumi tena)
Na maeneo ya kufanyia replacement ni ameneo ya hao jamaa
 
Tuangalie na upande wa pili wa timu yetu, Chelsea yetu ya sasa haina mchezaji kiongozi au wachezaji viongozi wanaoeshimiwa uwanjani.

Mchezaji anabolonga uwanjani kwa kuto toa pasi kwa mda lakini hapati karipio lolote toka kwa wenzie. Au anang'ang'ana kufunga wakati kuna mchezaji alikuwa kwenye nafasi nzuri zaidi bado hapati karipio lolote sijui ni mpaka wakutane baada ya mechi ndio waelezane hiyo ni too late.

Nakumbuka Chelsea yetu pendwa ilikuwa ukibolonga pale pale uwanjani unapewa makavu na viongozi walio kuwa hawamuonei haya mtu wawapo uwanjani walikuwa Drogba, Tery na Lampad. Hawa watu ilikuwa sio ajabu kumfuata mchezaji aliyebolongo na kumpa makavu huku mechi ikiendelea.

Leo hii hatuna watu mwenye sura ya mbuzi linapokuja suala la matokeo uwanjani. Ni kama wote wanaogopana kuambiana ukweli.

Ili kuwa na Chelsea imara tena ni pale kizazi cha akina James (yaani waliotoka Chelsea academy) watakapojizatiti na kupewa mamlaka kama ukaptain vile ndio wanaweza rudisha nidhamu ya wachezaji uwanjani.

Hayo ni maoni yangu tu,

I stand to be corrected.
 
DREAM TEAM
1668584265991.png
 
Nawatetea kwa nguvu zote hawa wachezaji watano
  1. Koulibaly bado hajazoea kwa vile hajawahi kucheza backline ya 3, kwenye backline ya 4 aliyocheza Kou kacheza vizuri japo sio sana lakini kwenye hii ya 343 ndio anaboronga sana
  2. Cucurella ni wale wachezaji wanaochukua muda kuzoea ila pia poor form ya timu imemuadhiri
  3. Sterling style yake ya uchezaji ni ya kimlenda ila anayo vitu vingi vya ku-offer. mfano Sterling ni mzuri kwenye kucreate chances na kufunga ila hapati huduma stahiki, hivyo hivyo kwa Auba.
  4. Havertz ni muadhirika wa poor service providers walio pale katikati. Hata hao washambuliaji wengine kama akina Pulisic (Japo Pulisic hata-offer vitu vingi sana lakini abdo angetupa magoli 10+ kama tungekuwa na muunganiko mzuri wa timu pale katikati)
Wachezaji ambao naamini hawatatufaa tena kwenye first team ni
  1. Azpi
  2. Jorginho
  3. Cheek
  4. Kante - Kwa sababu ya majeruhi - anavyozidi kuzeeka anaku more vulnerable to injuries
  5. Kovacic - Kachoka
  6. Ziyech - Ana uwezo mkubwa ila kaamua kuwa mjeuri
  7. Mendy - sidhani kama atarudi kwenye form yake ya 2020/21 na 2021/22 ( Hajitumi tena)
Na maeneo ya kufanyia replacement ni ameneo ya hao jamaa
Kwa mendy hapna umeongea nahis bàada ya kepa kutudanganya na vi save vyake ila mendy ni Bora sana
 
Kwa mendy hapna umeongea nahis bàada ya kepa kutudanganya na vi save vyake ila mendy ni Bora sana
I am serious utanielewa baadaye, msimu wa a 2021/22 mwishoni na huu msimu wa 2022/23 Mendy hakuwa yule wa misimu iliyopita. Mapenzi ya mchezaji weka pembeni weka mapenzi ya timu mbele. Mendy kwa sasa anastahili kuwa second golie aidha kwa Kepa au kwa kipa mwingoni hodari zaidi yake
 
Kwa mendy hapna umeongea nahis bàada ya kepa kutudanganya na vi save vyake ila mendy ni Bora sana
Kuanzia mwaka huu January Mendy amefanya makosa mengi lakini pia Mendy hawezi kutumia miguu yake vzuri hasa kwenye kuanzisha mashambulizi. Most of the time miguu ya Mendy imesababisha makosa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom