Uko sahihi kabisa Chief.
Ukweli utabaki hatuna kikosi bora cha kukimbia mbio ndefu za EPL.
Ukiangalia wachezaji tulionao ni wa kushinda mechi za mtoano/Chache ndio maana tunafanya vizuri UEFA, ila sio kubeba POINT 3 za EPL mfulilizo.
Tunahitaji kusajili wachezaji haswa Kiungo na ushambualiaji wa mbio ndefu wenye ubinifu wa kila aina, nguvu, kasi, wakatili mbele ya goli.
PULISIC:- Sio mchezaji wa mbio ndefu za EPL ndio maana ukiangalia stats zake za EPL tangu atue darajani ni kama anakula mshahara bure.
ODOI:- Sio mchezaji wa mbio ndefu EPL kuboronga ni kwingi kuliko kukupatia matokeo. Atakufurahisha mechi chache ila nyingi anaboronga sana.
MOUNT:- Kiwango chake kinapanda na kushuka ndani ya msimu. Pale mnapohitaji ubora wake ndio kiwango chake kinashuka.
ZIYECH:- Bado hajatulia kikosini, anahitaji kuimarika na kuaminika.
WERNER:- Binafsi huyu mchezaji nilimpa matumaini makubwa sana, niliona kama tumesajili mtambo wa kufunga magoli.
Ujio wa Lukaku tunasahau madhaifu ya Werner, nilitegemea ujio wa Lukaku, Werner angepata muda wa kujitafakari, kujifunza na kurekebisha makosa yake na kurudisha ubora wake wa bundasliga sioni akifanya hivyo. Time will tell
UHITAJI WA KIUNGO MSHAMBULIAJI MBUNIFU:- No doubt tangu aondoke FABRIGAS, hatujapata kiungo wa aina yake mwenye uwezo wa kupiga pass hatari kwenda mbele. Pass inayoweza kuvuka safu mbili za opponent.
UHITAJI WA KIUNGO MKABAJI:- Joghnho ni mzuri sana ila ana madhaifu yake sio kiungo wa kukaba kwa kujitegemea, bali anahitaji kiungo mwingine ambaye yuko kwenye ubora wa kukaba amsaidie kuficha madhaifu yake.

Rudger, Silva, Chilwell, James, Kante, Kovacic, Harvetz, Lukaku:- Hawa wako tayari kutupatia ubingwa wa EPL, kama wataongezewa wachezaji kama 4 (Wenye uwezo mkubwa)
ALONSO:- For Sale
AZIPI - SUB (Umri)
CHRISTENSEN:- Rotation
CHALOBAH:- Rotation
SARR :- SUB
BARKELY:- For Sale
CHEEK:- For Sale
KAI HARVETZ:- Huyu dogo ana kipaji kikubwa sana, anahitaji kucheza na mafundi wenzake ambao kwa sasa hawapo kikosini.
Angewakuta Fabrigas, Hazard, Willan ange- enjoy sana, Dogo yuko smart kichwani na mguuni. BONGE LA USAJILI