Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Wapinzani mnaomba tumfukuze kocha sababu mnamuogopa
Katika kocha wa kuogopwa epl na TT yupo ? ,Umeshindwa kumfunga Brighton then muogopwe ....Bado Moyo unaenda Kasi Kwan mnaenda kukutana na klop ,hivi nyie mko sawa kweli ....

TT kaishiwa mbinu , confidence imepotea Hana uwezo Tena
 
Katika kocha wa kuogopwa epl na TT yupo ? ,Umeshindwa kumfunga Brighton then muogopwe ....Bado Moyo unaenda Kasi Kwan mnaenda kukutana na klop ,hivi nyie mko sawa kweli ....

TT kaishiwa mbinu , confidence imepotea Hana uwezo Tena
Mbona ulikimbia humu ndani kwa miezi kadhaa baada ya huyo TT kukupasua na kubeba ndoo ya UCL mbele yako?

We jamaa mnafiki sana.
 
Hakika LUKAKU Kazingua sana kwa shombo Alizo ongea kama kweli hata simpendi hata kdgo
 
Kwa hiyo leo TT amekuwa mbaya?

Aiseeee...

Katika miaka 10 iliyopita makocha wawili bora wa Chelsea ni Antonio Conte na Thomas Tuchel.
Ndio fans wetu hao ni kama vinyonga tu, leo ataongea hivi kesho kutwa ataongea vile

Mashabiki wa chelsea ni waajabu sana, yani yeye kupoteza game kwake atakuwa kocha hafai or mfumo mbovu mara alikuwa anabahatisha, smh

Tuanalyse mpira based na jinsi tunavyocheza na hali tuliyonayo hapo ndio utajua shida nini,

Mtu anasema tuchel hajui kukuza viwango vya wachezaj je rudiger,james,christiansen,mount etc hawa wakat wa lamps na wakat huu viwango vyao vikoje au ndio tunaendeshwa na hisia kuliko uhalisia
 
Sajili za Marina za miaka ya karibuni za kuunga na soletepu, haswa kule mbele ametuletea wachezaji wa kawaida sana

Timu haina angalau hata mshambualiaji mmoja wa hatari wa kuogopeka wa kujivunia. Tangu aondoke HAZARD hatuna tena mchezaji wa kuamua matokeo.
Nani alikuwa hatari kama Werner, Havertz
Mnyonge mnyongeni haki yake apewe
Marina hadi kajizolea sifa kama gwiji wa kuuza na kununua wachezaji leo unamdhiaki jamani
Najua shida yako kubwa ni kwa sababu alishindwa kumleta Erling Haaland darajani
Najua msimu ujao wa kiangazi msisitizo utaekezwa kwenye kiungo atakayeamua matokeo atakayeshirikiana na Kante
Shida yangu ipo hapo katikati
Pia tukumbuke kuwa demand za makocha inatofautiana. Mimi naona

PEPE anademand kubwa kwa wachezaji na ndio maana karibu wote wanacheza kwa viwango vya juu
KLopp - hawezi kumfikia PEP ana bahati tu foward yake ni kali na anao viungo agressive zaidi ya Chelsea
TT - ana tactics nyingi zimeisaidia timu ila hana demand kubwa kwa wachezaji , wachezaji wengine hasa wale watoto wanahitaji kusukumwa sana
 
Huo mfumo TT ndio best kwake. Amefika mwisho wa mfumo sioni akibadilika au kubadilisha mfumo. Bali namuona akistick na mfumo & style hii hii ya uchezaji wa timu linyeshe mvua liwake jua.

Kiufupi TT ni mwoga wa kupoteza mechi mfulilizo hayuko tayari kujaribu mfumo mpya bali atakomaa na huu huu akiamini majeruhi wakipona mfumo wake utaimarika ( pass fupi fupi, back pass milioni 1, ball position asilimia laki 5)
Kila kocha anao mfumo wake, hata PEP anao wa kwake na ni rigid hapo. Inachotakiwa tu kocha ajue kuwafitisha wachezaji kwenye huo mfumo wake, akitokea mchezaji imeshindikana basi auzwe anunuliwe atakayefit humo
 
Shida ni wachezaj wetu, hata guardiola huwez kuta kabadilisha mfumo sana unakuta anabilisha tactics ila mfumo unakuta ule ule,
Zinchenko alikuwa mid lakin pep kamfanya amekuwa lb na anafanya kazi nzuri,

Klop msim uliopita alitumia hadi fabinho n henderson kama cb hakubadilisha mfumo. Kisa injury,

Issue ya kubadilisha mfumo huwa sio rahis kama tunavyozan kwa hawa makocha wakubwa, kubadilisha mfumo unaanza kuimplement idea zingine na huwa sikaz ndogo
Lakini Klop alikunywa magoli Heanderson na Fab walipokuwa wanacheza kama CB
 
Uko sahihi kabisa Chief. Na ikumbukwe TT alishasema hawezi kubadili mfumo kwa sababu, mfumo wake unatoa performance nzuri ya umiliki mpira uwanjani, kinachokosekana ni umalizaji wa kufunga magoli ndio kitu alichosema ataendelea kukiboresha.
Mfumo ndio specialization ya kocha kama tuanposema Daktari bingwa wa macho, ini, upasuaji, meno nk
Kocha anakuwa specialist kwenye formation fulani

Conte ni bingwa wa 343
PEPE 433
TT 343 ila hamkuti Conte

Tusitegemee kocha abadilishe mfumo hiyo ni sawasawa na daktari wa macho umlazimishe awe daktari wa ini nk
Tunachosema kocha ajue kuwafitisha wachezaji na vipawa vyao kwenye hizo mifumo pendwa
 
Hakuna mchezaji professional anaweza kutoka mbele ya media akafanya hivi.

Harry Kane alivyozinguana na Mmiliki wa timu baada ya kugomewa kuuzwa uliona alivyorudi uwanjani alivyokuwa?

Hakupoteza muda kwenda kwenye media.
Lukaku namuona kama ameshakata tamaa kuwa Chelsea na hata nasikia kawaomba msamaha mashabiki wa Inter na kadai anataka kurudi Inter akiwa bado kwenye form ya juu. Huyo sidhani kama atakaa msimu ujao darajani labda mambo yake yamnyookee, akiendelea kuwa na ukame wa magoli na kuwekwa benchi mara kadhaa, next summer atataka kurudi Inter
 
Kwa hiyo leo TT amekuwa mbaya?

Aiseeee...

Katika miaka 10 iliyopita makocha wawili bora wa Chelsea ni Antonio Conte na Thomas Tuchel.
Ni sawa ila sio mkamilifu, na niko hapo hapo kwenye madhaifu yake ambayo yameshaanza kuonekana. Na kwa kusema hivyo haina maana TT ni mbaya wala hafai kuifundisha Chelsea, NO NO, kama mshabiki tunaexpose hayo madhaifu ili aboreshe
 
Mfumo ndio specialization ya kocha kama tuanposema Daktari bingwa wa macho, ini, upasuaji, meno nk
Kocha anakuwa specialist kwenye formation fulani

Conte ni bingwa wa 343
PEPE 433
TT 343 ila hamkuti Conte

Tusitegemee kocha abadilishe mfumo hiyo ni sawasawa na daktari wa macho umlazimishe awe daktari wa ini nk
Tunachosema kocha ajue kuwafitisha wachezaji na vipawa vyao kwenye hizo mifumo pendwa
343 ya Conte ineshindwa kuwork UEFA.

Angalia misimu yote Conte aliyoshiriki UEFA uone kaishia wapi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom