
Hongereni THE BLUES kwa ushindi wa jana, vijana wa academy wamecheza vizuri sana.

Nusu fainali tunaenda kukutana na CONTE baba wa mfumo wa 3-4-3.

Urejeo wa KANTE & KOVACIC uwanjani, kikosi chetu kitarudi kwenye ubora wake.

Nadhani TT abadili style ya uchezaji wa mfumo wa sasa 3-4-3, tuhame kwenye style ya kushambualia kwenye space ndogo ndogo, twende kwenye kushambulia kwa counter attacks.
Tunao wachezaji wa counter attacks wenye kasi na nguvu Werner, Lukaku, Ziyech, Mount, Pulisic
Kwa ushambualiaji wa sasa wa slow motion kwenye space ndogo ndogo kuna pelekea wapizani wetu kupaki basi na kujazana lundo kwenye lango la mpinzani hapo uhaba wa kupata magoli utazidi kutusumbua.
Juzi nimeangalia mechi ya Liver na Tote, zile counter attacks za tote pale mbele ukimweka Lukaku atafunga magoli mengi sana. Ndio style anayopenda kushambulia, nguvu na kasi kwenye space kubwa.