Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

1627326643083.png
 
Hiv game yetu ya leo ya pre-season na Bournemouth ni saa ngapi? Tuambieni mnaojua
 
Nimeipenda hiii....


Kocha wa Atletico Madrid, Diego Simeone kuhusu Chelsea ya Thomas Tuchel; "Tulielewa ubora wao kwenye kucheza na nafasi. Mara zote wanakuwepo watu kwenye nafasi zao." "Nililipenda sana hilo na timu inayoweza kufanya mambo mengi. Walilionyesha hilo kwenye mchezo dhidi ya Man city. Waliwafunga Real Madrid kama walivyotufunga sisi. Tuchel amefanya kazi kubwa sana." "Tuchel ni kocha anayezuia au kushambulia? Ni timu inayozuia vizuri na inakupa presha kubwa kwenye kushambulia. Tulifikiri kwamba ni timu ya kawaida ambayo tumeshaiona hapo kabla." "Lakini walikuwa bora sana. Mechi ya marudiano walikuwa na kasi ya tofauti kabisa, walikuwa wanakufanya utengeneze nafasi. Jambo hilo tulilipenda sana." Unapigwa, unafundishwa na soka.....kuna watu wanaweza kusahau kwamba Suarez na ubora wake wote hakupiga shuti lolote😂 #d1905_updates
 
3-4-3 ndio mfumo bora utakao endelea kutupa mafanikio, kulingana na aina ya wachezaji tulionao kwa sasa.

TT asibadili mfumo bali aboreshe mbinu za uchezaji kule mbele mabao yapatikane kwa wingi.

Mkuu kocha bora lazima awe na mifumo tofauti tofauti ili mpinzani asikariri mfumo wake mmoja. Pia kocha bora ni yule anayebadilisha mfumo kulingana na oponent unayokutana nayo.

Kingine ni rotations ya wachezaji unawapo wote nafasi ili isilete kuwa wengine wanakumbatiwa. Wachezaji wetu wote ni wazuri wakipewa nafasi wanafanya wanda na hii ndiyo ilimsaidia tuchel msimu uliyoisha. #Comeonechelseaawemissedthegameoready#
 
3-4-3 ndio mfumo bora utakao endelea kutupa mafanikio, kulingana na aina ya wachezaji tulionao kwa sasa.

TT asibadili mfumo bali aboreshe mbinu za uchezaji kule mbele mabao yapatikane kwa wingi.
Tutegemee kuona mfumo mwingine ukiwa unatumika
 
Nimeipenda hiii....


Kocha wa Atletico Madrid, Diego Simeone kuhusu Chelsea ya Thomas Tuchel; "Tulielewa ubora wao kwenye kucheza na nafasi. Mara zote wanakuwepo watu kwenye nafasi zao." "Nililipenda sana hilo na timu inayoweza kufanya mambo mengi. Walilionyesha hilo kwenye mchezo dhidi ya Man city. Waliwafunga Real Madrid kama walivyotufunga sisi. Tuchel amefanya kazi kubwa sana." "Tuchel ni kocha anayezuia au kushambulia? Ni timu inayozuia vizuri na inakupa presha kubwa kwenye kushambulia. Tulifikiri kwamba ni timu ya kawaida ambayo tumeshaiona hapo kabla." "Lakini walikuwa bora sana. Mechi ya marudiano walikuwa na kasi ya tofauti kabisa, walikuwa wanakufanya utengeneze nafasi. Jambo hilo tulilipenda sana." Unapigwa, unafundishwa na soka.....kuna watu wanaweza kusahau kwamba Suarez na ubora wake wote hakupiga shuti lolote #d1905_updates

Hii statement nililiona mahala nijikuta kucheka tu. Kumbe Simione aliichukulia Chelsea kawaida afundishwa adabu kabisa na soka pia
 
Kuna ripoti zinasema Mason Mount anabadilishiwa namba na kutoka 19 na kwenda namba 8!

Hilo linaonekana pia kuthibitishiwa na yeye mwenyewe mara baada ya kubadilisha jina kwenye akaunti yake ya Instagram ambapo amefuta namba iliyokuwepo hapo mwanzo kwenye jina lake ambapo ameifuta namba 10.

Ingawa bado hajaweka namba 8, lakini ni moja kati ya ishala kwamba huenda anajiandaa kuweka namba 8!

Na usisahau namba 8 ilikuwa inavaliwa na Ross Barkey ambaye alichukua kutoka kwa Oscar Emboaba ambaye naye pia alichukua mara baada ya Frank Lampard kuondoka.

#updates
 
🔙BACK ON THE DAY:

📆Tarehe kama ya leo 2004, Ricardo Cavalho alisaini ndani ya Club ya Chelsea FC akitokea FC Porto kwa ada ya £19.85M.

🏟Michezo - 210.
🥅Cleansheet - 102.
⚽️Magoli - 11.
🏆Premier League x3.
🏆FA Cup x3.
🏆League Cup x2.
🥉Chelsea players' player of the year.

Ricardo Cavalho mtu na nusu 🙌.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom