Yes mkuu.
Ila huyu Thomas Tuchel no kocha mzuri sn Chelsea hatujawahi kupata. Nimekuwa namuelewa sn kwa kila kitu na moja ya kitu ninachompongeza huyu kocha ni kuweza kuwapa nafasi wachezaji wote ya kucheza.
Alafu ana mbinu Fulani kwa kutegemea uwezo wa wachezaji.
Mafano Leo ako na mfumo was 3+4+3 lkn hii ni km 4+3+3 maana anatumia uwezo was Christiansen kucheza kulia anakava mpk beki ya kulia ya pembeni. Kwahiyo Odoi muda wote anashambulia tu.
Wakati huo Emerson anaweza kucheza km cb wa kati upande wa kushoto na anacheza pia beki wa kushoto wa pembeni km Ben Chilwell kapanda mbele sn.
Kwa maana hiyo basi km tunashambuliwa sn ndio utamuona Ben anarudi ktk nafasi yake na Odoi na hawa cb watatu wanarudi kati wote
Lkn Tuchel ni bomba la kocha na atatupeleka mbali sn kwa hiki kikosi kipana tulicho nacho.
Jambo jingine naona Pulisic anachezewa sn rafu yaani kila akigusa mpira wanamla
Kwa namna tulivyo na njaa namna hii makombe haya yanayo zagaa zagaa mbele yetu la FA na UEFA tunayabeba yote