Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Bansley waliwatoa Liverpool 2-1 na Chelsea 1-0 kwenye FA ya mwaka 2008 tena Chelsea tukiwa ndio bingwa mtetezi wa kombe hilo.

Goli la kichwa la Kayode Odejayi dk ya 66 ilitosha kuiondoa Chelsea kwenye robo fainali ya FA ya mwaka 2008 mbele ya akina John Terry, Michael Ballack, Essien, Malouda, Kalou, Carvalho, Anelka, Joe Cole na wengineo
Wakati huo wanatufanyia hayo maajabu, kule Championship walikuwa nafasi ya 18

Liverpool nao nyumbani kwao Anfield wanabamizwa 2-1 na hawa hawa Bansley ambao waliponea chupuchupu kuteremshwa daraja na pia kutolewa round ya pili tu ya Karabao Cup

Ama kweli saa nyingine mpira wa soka hauna adabu, timu bora kufungwa na timu duni
 
me nafikir tommori anatufaa zaid..!!
Tomori atakuja kuwa CB mzuri ila bado ana safari ndefu. Tukiwategemea watu kama akina Tomori tukubali kuwa kila mwaka tutakuwa tunapigania top 4 tu, huo ndio ukweli
Walichokosea Chelsea tu ni kumuuza, angetolewa mkopo tu ikaishia hapo
 
Update ya majeruhi
Wako wanne
  1. Silva
  2. Havertz
  3. Pulisic - sio majeruhi bali mambo ya kifamilia
  4. Werner
Wote watakuwepo kwenye mchezo na Bansley isipokuwa Silva ambaye atakuwa bado kupona hadi tarehe 20/2
 
Tomori atakuja kuwa CB mzuri ila bado ana safari ndefu. Tukiwategemea watu kama akina Tomori tukubali kuwa kila mwaka tutakuwa tunapigania top 4 tu, huo ndio ukweli
Walichokosea Chelsea tu ni kumuuza, angetolewa mkopo tu ikaishia hapo
Tomori hajauzwa bado yupo kwa mkopo
 
Hii team kwa kucheza na vibonde haijambo [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Hii team kwa kucheza na vibonde haijambo [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Mko na Wagonga nyundo leo. Ngoja tuone. What will Zebra FC do?
 
Hii team kwa kucheza na vibonde haijambo [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
ni msimu huu tuu,maana msimu uliopita nilikutoa wewe...au wewe kibonde?
 
Tutakuwa na wazee wengi kule nyuma kama Crystal Palace
Kwa nini Chelsea wasimsajili beki wa kumpa mkataba wa miaka minne au mitano. CB wa miaka 27 maximum anafaa
Wangemsajili Upecano 22 au Laporte, naona Man city wanamuweka benchi kwa sababu ya Dias ana miaka 26 hao watatufaa
Nathan ake yuwapi sikuhizi
Huyu alikuwa future CB wa Chelsea
 
Tomori atakuja kuwa CB mzuri ila bado ana safari ndefu. Tukiwategemea watu kama akina Tomori tukubali kuwa kila mwaka tutakuwa tunapigania top 4 tu, huo ndio ukweli
Walichokosea Chelsea tu ni kumuuza, angetolewa mkopo tu ikaishia hapo
Sikuelewa kwa nini lampard hakutaka kumpa nafasi tomori kama alivyokuwa anawapa wengine hata wafanye makosa kiasi gani
 
Tutakuwa na wazee wengi kule nyuma kama Crystal Palace
Kwa nini Chelsea wasimsajili beki wa kumpa mkataba wa miaka minne au mitano. CB wa miaka 27 maximum anafaa
Wangemsajili Upecano 22 au Laporte, naona Man city wanamuweka benchi kwa sababu ya Dias ana miaka 26 hao watatufaa
City hawawezi muuza Laporte, ni injury tu za mara kwa mara ndio zinamsumbua
 
City hawawezi muuza Laporte, ni injury tu za mara kwa mara ndio zinamsumbua
Lakini kwa uwepo wa Dias na Form nzuri ya John Stones, Laporte anaweza akalazimisha aende kwenye timu itakayompa muda wa kucheza

Pep Guardiola says Aymeric Laporte can decide own future at Manchester City​

  • Frenchman unable to break partnership of Stones and Dias
  • ‘He has to be focused to come back in the best condition’
Pep Guardiola has said Aymeric Laporte can reclaim his first-choice status for Manchester City, despite the impressive central defensive partnership of John Stones and Rúben Dias.
Source: The Guardian
 
Kovacic anacheza vizuri sana na tena siku hizi ameimprove kwenye defensive phase sio kama alivyoanza
TATIZO LAKE MOJA TU
Akifika golini anabutua nje siku zote
 
Kuna wachambuzi wa Suppersports walikuwa wanamchambua Tuchel na aina ya wachezaji watakaomfaa pale Chelsea

Wanadai Tuchel is a tactical manager kama Conte, anabadilika kulingana na timu pinzani, wachezaji waliopo na mchezo unavyochezwa
Alonso atamfaa zaidi kwa sababu ya ujanjaujanja na uzoefu alionao Alonso kwenye kushambulia wakati mwenzake Chillwell atahitaji muda kuadjust kwenye tactical approach za Tuchel.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom