Hii ni best comment ever.
Tayari winning team ilishaanza kuonekana best combinations Mount - Kante- Kovacic hawa jamaa wakicheza pamoja dimba la kati wanalimiliki.
Lampard una mpanga Harvetz wa nini? Mchezaji yupo yupo tuu uwanjani hana P.o BOX. Kwenye kukaba anasindikiza kwenye kushambulia anapoteza mipira ovyo, hana nguvu, hana kasi.
Jana kikosi kingekuwa hivi:-
Werner/Pulisic - Giroud/Werner - James
Mount - Kante - Kovacic
Chilwell - Thiago - Zouma - Azipu
Timu inakuwa na ubunifu kulingana na kocha unavyopanga kikosi, timu inakuwa na morale kwa aina ya wachezaji wanaopangwa.
Timu inacheza flat 1st half & 2rd Half, mechi tungeimaliza 1st half, kipindi cha pili kilikuwa cha ovyo ovyo hata pale Traore ameumia timu haitumii advantage ya gap ndio kwanza wanaongeza utopolo.
Timu kama Liverpool lile gap la Traore kuumia wanaongeza kasi ya mashambulizi wanapata goli.
Chelsea sio title contender bali ni wasindikizaji, title contender anacheza kibingwa, kimbinu, kimipango na sio lelemama jama jana tuombe Mungu tumalize top 4.