Mkuu kipindi cha Sarri tulicheza mpira mzuri sana mpaka ikatoka ile statement "Sarri Ball" na kipindi kile wachezaji wengi walipandisha sana viwango vyao kama RLC, Odoi lakini mashabiki wakamponda hana plan B na wakati hakua amemaliza plan A. Kipindi hicho mimi ni mmoja wa walioumia sana kuondoka kwa Sarri na tetesi za Lampard kupewa timu zikaanza watu wakaja na maComment marefu kumsifia na kutaja jinsi soka lake litakavyokuwa zuri. Wengi wao wakasahau kuwa kocha unahitaji experience siyo tu kwakua mchezaji ni legend basi apewe timu. Nilikua mmoja wa walioliona hili wakati ule lakini hatukua na say tunasema tu inaishia humu humu jukwaani.
Liverpool hawakua wajinga kutompa timu Gerald wakati huo alikua keshaanza kufanya vizuri Rangers, Zidane anafanya vizuri kwa sababu amefanya kazi chini ya Ancelloti kwa iyo ana experience, sitoshangaa Arteta kufanya vizuri Arsenal kwa sababu keshakua chini Pep ivyo ana experience kidogo, kuna kipindi Giggs alipewa Man Utd kwa muda na timu ikawa inafanya vizuri lakini haikuwapumbaza kumpa aifundishe moja kwa moja kwa sababu walijua matatizo kama haya.
So nachotaka kusema uteuzi wa Lampard from the first time haukua sahihi, tutamlaumu, tutamtukana, tutamkejeli na kadhalika lakini mwisho wa siku tumembebesha mzigo mkubwa toka mwanzo huku tukimpamba kwa maneno mazuri mazuri. Sioni Lampard akibadilika kiuchezaji jwa hiyo tuache afanye kazi yake mpaka pale mambo yatakapobadilika kwa sababu tumeletewa na hatuna budi kukubaliana naye.
Halafu nilichogundua mashabiki wa Chelsea hawafuatilii mpira ni watu wa kufuata mkumbo na kuna wanakwambia hawajawahi kumuona RLC akiwa bora Chelsea

na hao ndio wakawa wanasema Sarri atimuliwe. Tuwe wavumilivu tu Lampard atatufikisha mahala pazuri sijui kwa njia ipi ila naamini bodi kumteua wanajua wanachofanya.