Ngoja niwachambue ndugu zangu wa zizini
Kuhusu usajili wa timo Werner na hakim ziyech
Ndio timo anajua kufunga kama msimu ulio kwisha wa bundesliga kawa namba mbili kwa kufunga goal 28 sio mbaya kwa streka
Kama huyu ndio anatakiwa hapa kweli mlilamba dume hilo halina shaka
Kingine kwa hakim hapa pia mlilamba Dume kwani hakim yeye kufunga na assist anaweza kazi itakua ni kumlisha timo palembele
Lakini

nawakumbusha huku nyuma hakuna kitu jamani
Timo anaweza kufunga goal 30 kwa msimu huku nyuma kwa kina kepa
Wanaweza kucheza mechi kumi wakaruhusu goal 40 kabla hata msimu haujaisha
Kingine na huyu kepa ndie atakua mpinzani wa timo katika kufunga magoli kwani yeye timo
Akifunga kepa yeye anaruhusu

tu huku nyuma mwisho wa msimu wanaweza kulingana kila kitu kuanzia magoli hadi assist
Yani hapo ndugu zangu wa Chelsea wanajenga nyumba bila msingi na msingi ni huku nyuma
Na nyumba pasipo msingi itanguka
Ushauri wangu ni kwamba pesa ya kumsajili kai bora watafute beki na kipa
Kuliko kuja kuona kepa na kina Zuma wakishindana kwenye kufunga magoli na mastreka wao

na assist huku nyuma wakichoma
Kingine ziyech ni mzuri mzoefu mwenye ubora kuliko kai
Ukweli usemwe kai hana umuhimu wowote kama beki na kipa pale zizini
Lampard anatakiwa kushtukia huu mchezo kwa kai
Mfano embu angalia mbugani pamoja na Bruno kuwasaidia kupiga penalty huku nyuma
Magwaya na lindelof wanashindana naye kufunga au kutoa assist kwa timu pinzani
Yangu ndio hayo
Nakwenda zangu





