Ngoja niwachambue ndugu zangu wa zizini
Kuhusu usajili wa timo Werner na hakim ziyech [emoji23]
Ndio timo anajua kufunga kama msimu ulio kwisha wa bundesliga kawa namba mbili kwa kufunga goal 28 sio mbaya kwa streka
Kama huyu ndio anatakiwa hapa kweli mlilamba dume hilo halina shaka[emoji122]
Kingine kwa hakim hapa pia mlilamba Dume kwani hakim yeye kufunga na assist anaweza kazi itakua ni kumlisha timo palembele[emoji122]
Lakini[emoji22] nawakumbusha huku nyuma hakuna kitu jamani
Timo anaweza kufunga goal 30 kwa msimu huku nyuma kwa kina kepa
Wanaweza kucheza mechi kumi wakaruhusu goal 40 kabla hata msimu haujaisha
Kingine na huyu kepa ndie atakua mpinzani wa timo katika kufunga magoli kwani yeye timo
Akifunga kepa yeye anaruhusu[emoji23] tu huku nyuma mwisho wa msimu wanaweza kulingana kila kitu kuanzia magoli hadi assist [emoji23]
Yani hapo ndugu zangu wa Chelsea wanajenga nyumba bila msingi na msingi ni huku nyuma
Na nyumba pasipo msingi itanguka
Ushauri wangu ni kwamba pesa ya kumsajili kai bora watafute beki na kipa [emoji23]
Kuliko kuja kuona kepa na kina Zuma wakishindana kwenye kufunga magoli na mastreka wao[emoji23] na assist huku nyuma wakichoma
Kingine ziyech ni mzuri mzoefu mwenye ubora kuliko kai
Ukweli usemwe kai hana umuhimu wowote kama beki na kipa pale zizini
Lampard anatakiwa kushtukia huu mchezo kwa kai [emoji23]
Mfano embu angalia mbugani pamoja na Bruno kuwasaidia kupiga penalty huku nyuma
Magwaya na lindelof wanashindana naye kufunga au kutoa assist kwa timu pinzani[emoji23]
Yangu ndio hayo
Nakwenda zangu[emoji23][emoji23][emoji23][emoji125][emoji125][emoji125]