permanides
JF-Expert Member
- May 18, 2013
- 12,430
- 15,221
Usisahau pia kwa upande wa kocha
Bora mechi zimeisha tumechoka kuangalia Chelsea ya ovyo kuwahi kutokea ndani ya miaka 10 ya karibuni.
Tujipange kwa msimu ujao, kwa maana ya kusajili wachezaji wazuri kila idara.
Itakuwa upumbavu kuendelea kuwa na makipa wa ovyo msimu ujao
Itakuwa upambavu kuendelea kuwa na mabeki wa ovyo msimu ujao
Itakuwa upambavu kuendelea kuwa na viungo nyanya wasiokuwa na ubunifu msimu ujao
Itakuwa upambavu kuendelea kutegemea vijana wadogo wanaopambwa ni talent za baadae ili hali viwango vyao ni vya kwenye training ground.
Itakuwa upambavu mkubwa kuendelea kuona Chelsea inayocheza kwa kurelax na kumpa adui nafasi ya kujipanga na kutufunga.
Tunataka Chelsea ya wachezaji wapambanaji, wachezaji wanaume na sio vivulana vya academy visivyokuwa na P.O BOX