lembu
JF-Expert Member
- Dec 31, 2009
- 19,694
- 25,910
Mkuu wanaombeza Odoi si Chelsea fan. Mimi nilichocomment tu ni mshahara wake hauebndani na brand yake ya sasa. Alitakiwa angalau aanze na laki moja, hii ya laki 180,000 halafu kuna uwezekano mkubwa asitumike sana ni ubadhirifu wa pesa na kuwakatisha tamaa wenzake kama akina Tomori, Reece, na Mount plus hao academy wengine ambao wanacheza vizuri kuliko yeye.Sisi mashabiki tuna tabia za ajabu sana yan huwa hatueleweki linapokuja suala la wachezaji wetu. Leo tutamsifia kesho tutamponda na pia tutasahau aliyofanya nyuma. Mfano, Willian katika mechi za mwanzo msimu huu hasa aliporejea kutoka maheruhi watu walimponda balaa mpaka kuna wengine wakaandaa list ya wachezaji wa kuuzwa Chelsea na jina lake likawemo lakini ndan ya mechi mbili za mwisho kabla ya hii ya Grimsby amesifiwa balaa sasa unaanza kujiuliza siyo hawa waliokuwa wanamponda.
Haya issue nyingine ni huyu dogo Odoi leo hii kuna watu wanasema hamna kitu pale kikuweli mimi nawashangaa sana hasa kwa huyu dogo. Hebu rudini mkaangalie zile clip za msimu uliopita mjiridhishe tena ndio mje na izo negative comments zenu. Ukiachana na media za EPL kum hype tukija kwa mitazamo yetu kimpira yan hamuoni chochote kwa huyu dogo wa miaka 18? Ooh the world is difficult for the blind. Huyu dogo ana zaidi ya miezi hagusi mpira msitegemee arudi uwanjani aanze kuonyesha mambo yake halafu bado ni mdogo ndio anajifunza katika umri wake ni kazi kufikia kiwango cha Sancho au Mbappe. Tuache upofu tumuangalie mbele zaidi siyo sasa dogo anajua.View attachment 1217788
Kuhusu mashabiki kugeuka kugeuka ndio ushabiki wenyewe. Mchezaji anasifiwa na kutiwa moyo anapocheza vizuri akitibua anasakamwa ili aondoke au arudi kwenye form. Mimi ni mmojawapo wa mashabiki ambaye naweza kumsifia asubuhi akicheza vizuri na kumponda jioni akiboronga. Ushabiki umebeba sehemu kubwa ya afya zetu. Pressure ya nini
Willian kwa mfano na Alonso wakati wa Sari waliboronga sana. Lakini kwa huu mfumo wa Lampard na pia kwa pressure ya Lampard naona Alonso na Willian wamerudi kwenye form yao nzuri.
So mkuu wala isikupe shida, hata wewe kesho Odoi akiboronga utakuwa wa kwanza kumponda na kumtaka kocha amweke benchi. Kwa umri wake tumuombee acheze vizuri na form yake izidi kuimarika kwa sababu anazo talents nzuri ambazo Chelsea itazihitaji sana