Wakuu,
Shughuli inaanza weekend hii na Stoke City - ARE WE READY WITHOUT MODRIC at the heart of midfield?
Lets us see what we have at Midfield positions currently,
Frank Lampard - Mkongwe, Mzoefu - chini ya AVB anaweza kuongoza kiungo cha chelsea msimu huu- anaonekana kuwa fit sana.
Remires - Ana miaka 23, ana pumzi sana na kasi - anakaba na anaweza kusaidia ushambuliaji.
Mikel Obi - Ana miaka 24, Ana pumzi, ni kiungo mkabaji - msimu uliopita hakufanya vizuri sana, so far yupo fit hasa pre season zinavyoendelea.
Josh McEachran - Kinda aliyelelewa Chelsea - anaonekana kuwa na kipaji cha pekee. anaweza ku break kwenye first team msimu huu.
Yosh Benayoun - Mzoefu, Mid iliyokamilika - ana kasi na anachezesha washambuliaji - so far yupo fit - tegemeo mwaka huu
Kakuta - Kijana mfaransa - anaonekana kuwa na kipaji cha pekee - kwa sasa yupo na timu ya taifa U20 ya ufaransa.
Oriol Romeu - Kijana mdogo kabisa kwa ki hispaniola - tumempata juzi tu toka barca, ni kiungo mchezeshaji na anaweza kuwa replacement ya
essien ambaye kaumia. Tunategemea combination nzuri hasa kwa striker mhispania mwenzie Toreess.
Ni kweli tunahitaji Modric kuongeza creativity kwenye sehemu ya kiungo, lakini kama hatutapata signature yake nafikiri ni muda wa vijana hawa 5 waungane na Lampard, Benayoun Kurudisha Kombe letu darajani. Pia tumebahatika kuwa na wingers ambao ni wakabaji na wanaweza kucheza kwenye midfield kama Malouda. Pia kuna baadhi ya games tumemwona Anelka akicheza nyuma ya Drogba wenye Diamond midfield. so bado chelsea ina option nyingi sana. YES WE ARE READY.