Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Jioni ya leo tumeona Ferdnando Torres alivyoweza pata goli lake la kwanza toka ajiunge na club yake mpya ya Chelsea.Tumeweza kuona jinsi mashabiki pamoja na Kocha wao walivyo mshangilia mithili ya gamba jipya la sisi em linavyoshangiliwa na wanachama wake kwa kufanikisha kulivua gamba walilshindwa kulivua kwa mda mrefu na hatimaye wamefanikiwa kulivua.Uwanja mzima ulilipuka kwa furaha, wachezaji wote walimrukia Torres utadhani lile goli lilikuwa lina wapa ubingwa Chelsea.Swali ni kwamba, je kulivua gamba la kuto funga magoli kwa Torres kunatoa matarajio gani? Au kajivua gamba wakati sumu bado ileile nikimaanisha ukame wa magoli kuendelea? Atafanikisha kuleta taji tajiri na mashabiki walivyo kuwa wakitarajia?
 
Hatimaye Torres apata goli

Hatimaye Fernando Torres amemaliza ukame wake wa magoli, baada ya kupata bao na Chelsea kupata ushindi wa 3-0 dhidi ya West Ham.

Torres aliingia kama mchezaji wa akiba kipindi cha pili, akiichezea Chelsea kwa mara ya 14, tangu ahamie kutoka Liverpool kwa pauni milioni 50.

Aliachia mkwaju na kuandika bao la pili.

Frank Lampard tayari alikuwa ameipatia Chelsea bao la kuongoza katika kipindi cha kwanza.

West Ham walipoteza nafasi nyingi, kabla ya Torres kufunga bao la pili, lakini hata Hivyo West Ham ilizamishwa na bao la tatu lililofungwa na Florent Malouda.

Chelsea sasa ina tofauti ya pointi sita nyuma ya Manchester United wanaoongoza ligi ikiwa imesalia michezo minne kumalizika kwa msimu.

West Ham wametitia mkiani.
 
_52320800_011820745-1.jpg




_52321274_011821037-1.jpg
 
Khe khe kheeeeeeeeeeee new director wa Chelsick kuanzia summer AV Grant ameuza timu hebu angalia wanavyokenua, Grant kaamua kuwashusha daraja West Ham kwa kuahidiwa kazi aliyopoteza kwa Mafioso chacha tuangalie kama Abraham O vich atatimiza ahadi zake kwa huyu Israel nut! Nasikia Tor the res alibahatika kutokana na cowshed kujaa cow dungs .. .... .... bila hivyo angetoka tena bila mrisi khe khe kheeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
 
Bonge la controversy simchezo. Mpira si ukivuka mstari kidogo ni goli tayari au mpaka mpira wote? Manake ule karibia nusu na zaidi umevuka mstari na kama mshika kibendera angekuwa kwenye kona kule angekubali goli.
 
Bonge la controversy simchezo. Mpira si ukivuka mstari kidogo ni goli tayari au mpaka mpira wote? Manake ule karibia nusu na zaidi umevuka mstari na kama mshika kibendera angekuwa kwenye kona kule angekubali goli.

Mpira ukigusa laini tayari ni bao. Its not a must for the whole damn thing to hit the net.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom