Hili nalo neno Mkuu
Mie na "declare interest ni shabiki wa kutupa tena teja kabisa" wa Chelsea Fc lakini naona kuna tatizo ndani ya klabu yenyewe. Inaweza kuwa bodi au hata mmiliki maana kila kocha anaekuja akimaliza miaka miwili ni bahati
Kuna nyakati lazima tuwe wakweli, kushinda makombe makubwa kama UEFA inataka timu iliyojengwa imara na kocha japo kwa muda mrefu kidogo. (Sitaki tuzungumzie akina Arsenal nkhawa wana sababu zao japo kocha ana muda mrefu) Sasa sie tumekuwa watu wa kutaka mafanikio wakati timu yetu inakuwa kama ni kikundi cha wachezaji walioletwa kwa mashindano ya muda maalumu ambapi watacheza vema wakiwa hawajafahamina vema na kocha. Wakishamzoea tu kocha bhasi vitimbi haviishi. Haya, ukija bodi yetu nayo imezingua kiukweli, kocha anataka wachezaji wa aina hii wao wanaamua tofauti (kuna maelezo ya kutosha yapo bbc sports/football, nikipata muda ntayaweka hapa). Emenalo alikuwa anaonekana anazingua lkn sasa ukweli unaanza kudhihiri
Hapa, isitafsiriwe kama namtetea Conte laa hasha lakini ifike wakati timu itulie na kocha japo kwa muda mrefu huwezi kushinda kila mwaka makombe na ile ligi ngumu. Penye mapungufu ya kocha yarekebishwe lakini maamuzi yale ya kumfukuza kocha ukiangalia takwimu (nilikuwa nafuatilia mtandao mmoja nadhani bbc sports/football nirekebishwe km nimekosea kuukopi) mashabiki wengi hawaungi mkono tena suala la timua timua. Ni kweli kuna baadhi wa wachezaji wanacheza chini ya kiwango mf Cahil, Bakayoko ambayo labda kwa uchovu, kushuka kwa kiwango nk, lkn sasa yatosha
Mambo ya "who will be Chelsea next coach" kila baada ya muda mfupi haifai