Bado anatakiwa asajili watatu
Kiungo,mshambuliaji na beki mmoja wa ziada
Yeaaaaaaaah.... This is Chelsea"
Luiz, Azpilicueta, Rudiger, Moses, Alonso, Christensen, Kante, Bakayoko hawa wanadamu laiti kama wangechoka kama Willian na Morata basi nadhani hadithi zingekuwa nyingine. Kuna wakati Tottenham Hotspur walikuwa hawajui chakufanya japo mpira ulikuwa chini ya miguu yao.
Chelsea walikaa kwenye njia zote za mipira ya Tottenham Hotspur, waliamua kuwafanya Spurs wacheze tu mpira mbele ya eneo la hatari la Chelsea bila mafanikio yeyote(hii tunaiita mbinu vitani).... Kuna wakati kila mtu alitamani Spurs acheze kama walivyocheza, ila kuna wakati watu walichukizwa na namna Chelsea walivyocheza na kumaliza mchezo.... Raha ya mpira huu ni swahiba aliyeshangilia ushindi wa Chelsea, huku akiwatusi Chelsea pia kwa kuchana mkeka wake

(hii tunaiita chagua moja).
Chelsea walikuwa bora zaidi ya Spurs kimbinu, walifanya pressing kuanzia katikati ya uwanja, wakaziba mianya yote ya mpira na kuwafanya Spurs kupiga back pass nyingi ambazo zilikuwa hazina faida.... Alichokikosa Spurs ni Dembele mwingine ukiachia Yule wa kwanza, kwamaana ukiachia Dembele hakukuwa na mtu mwingine aliyekuwa anatembea na mipira kwa upande wa Spurs, ila viumbe hawaaaa

kante na Willian hawa walikimbia na mpira mara nyingi zaidi na walikuwa wanaweza kuwakimbiza walinzi wa Spurs mara nyingi zaidi walipohitajika kukimbia.
Kuanza na watu 6 wenye kaliba ya ukabaji ilikuwa sehemu ya kwanza ya ushindi kwa Conte wetu. Spurs wameondoka na possession zao ila Chelsea wameondoka na alama zao 3. Njia rahisi ya kupigana vita ni mbinu... Master tactician Anthony Conte.
Miguu ya Marcos Alonso imeokoa sura ya Batshuay kwa siku ya jana..... Kidogo tu ingegeuka, na hii ingekuwa zamu ya Morata kumcheka Batshuay