Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

hongera sana all fans wa chelsea kwa ushindi ile mechi ya palace iliniuguza toka siku ile ila leo nimepata ahueni ushindi wa leo umetibu majeraha yote,ila toten nao wamekamia sana hili kombe maana ushindi wao wa leo ni wa maajabu
 
Nampenda sana Diego costa ila siku hizi ananiudhi. Anacheza zaidi na miili ya wapinzani kuliko kuchezea mpira.
 
Bado masaa manne tu
Chelsea amshinde Liverpool points 7!
Week ijayo zitapungua hadi points 4 sababu Chelsea huyu kaisha choka hawezi mfunga Everton
Mtacheka lkn mtakuja nikumbuka siku MAJOGOO yanapewa kombe lao
Chelsea imedorora muda mbaya sana kwenye ligi
Vipi bado tu unaendelea kuota amka sasa kumekucha jogoo kesha wika
 
CHELSEA 2-1 MANCHESTER CITY, Premier League: Post-match reaction

We're Back to winning, baby!

Mara baada ya kupoteza mchezo dhidi ya Crystal Palace weekend iliyopita, Chelsea iliwakaribisha Manchester City kuwaonjesha upepo mzuri katika dimba la Stamford Bridge, hii ilikuwa match kali kwa team zote zikiwa na malengo tofauti tofauti juu ya matumizi ya hizo points tatu; vijana wa Pep Guardiola walionekana kuutawala mchezo in terms of possession but the Blues ndo waliofanya kitu kinacho matter the most katika soccer; baada ya kuzibakiza points zote tatu mbele yao wanaojiita our direct title rival kwa kuwatundika mabao mawili kwa moja.

Kabla ya game nilipatwa na wasi wasi baada ya kuiona line-up ikiwa na Kurt Zouma kwenye backline huku Cesc Fabregas akianza kwenye midfield, but Mungu ni mwema, wamefanya kazi nzuri mno.

Ilikuwa eventful game kama tulivyo tegemea, kwamba Manchester City wange dominate mipira huku wakipiga ma shot ya hapa na pale; but Chelsea walikuwa more efficient mwanzo mwisho.

Game ilikuwa level baada ya Kurt Zouma ambae amerejea kutoka kwenye Injury kumpisha Nemanja Matic ambae alikuja ku strengthen midfield yetu, huku César Azpilicueta ambae aliitendea haki right win back akarejea kwenye centre back.

Kama kawaida yake Eden Hazard kwa mara nyingine tena alisimama kiume katika big game kwa ajili yetu huku akiibuka shujaa kwa kutupia mabao yote mawili.

Ilikuwa powa sana kumuona Pedro Rodriguez akirudi kwenye original position yake, aliwaweka busy ma defenders wa City kitu kilichopelekea tuta lililozaa bao la pili.

Pamoja na kuwazawadia Manchester City bao katika first half, Thibaut Courtois alikuwa na good interventions kadhaa wa kadhaa.

Oh, Diego... tumekumiss sisi mashabiki, tikisa kamba mnyamwezi acha kuwachekea wapinzani.

Nijuwavyo mimi ushindi siku zote ni matokeo matamu, especially siku kama hii ambapo Tottenham almost waangukie pua dhidi ya Swansea.

Mpaka sasa ni only 8 games zimebaki
 
Kama kawaida Chelsea yazidi kujikita kileleni baada ya ushindi wa jana 2-1, hazard katika ubora wake kuweka goli zote mbili na goli la kufutia machozi likifungwa na Aguero.
Congratulation #The_blues
ea89957214e9ef10a91e35c774cdfc06.jpg

ecef2cc56de96c164fb778afa5a075ec.jpg

8fe6e900ce281e80e68119a830600466.jpg

c04f8cd4aab3f75dd346eaaea8b32cf9.jpg

5558d0fc112e0fb506d43ed1f76744a2.jpg
 
Naona spurs wazee kunyata wanatunyatia ila ashukuriwe mungu kwa arsenal ambaye anamuweza ,man u hanaga ujinga nae na lecister anayekwenda kulipa fadhila.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom