Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

'IT'S A BIG PROBLEM' - WENGER SLAMS CHELSEA-STYLE LOAN SYSTEM"
Hapa ndipo namkumbuka Mourinho sana kwa haya mambo ya wenger
 
81419b66b5d0b3734c8e2ab364d8d055.jpg
 
usiitoe liver mkuu nawaogopa sana wale jamaa mwaka huu wako kwenye form
Mkuu wale hawana lolote. Wale ni timu inayokania timu kubwa tu lkn wakikutana na timu ndogo inacheza hovyo. Hiyo sio Sawa lazima timu icheze Ktk kiwango kile kile ata km inacheza na timu kubwa au ndogo. Alafu walituotea tu pale awali lkn tukienda kwao watajuta.
 
usiitoe liver mkuu nawaogopa sana wale jamaa mwaka huu wako kwenye form
Ni ngumu kidogo kuitoa Liverpool kwa sasa wako vizuri ila hao Spurs hata kama kocha wao anasema anasubiri mwezi wa 4 hiyo ni mikwara butu

Lakini ukweli Chelsea tuko vizuri mno
 
Ni ngumu kidogo kuitoa Liverpool kwa sasa wako vizuri ila hao Spurs hata kama kocha wao anasema anasubiri mwezi wa 4 hiyo ni mikwara butu

Lakini ukweli Chelsea tuko vizuri mno
spurs huwa wanamkamia chelsea tu na wala spurs hata big 4 sidhani kama wataingia ila liver ndugu yangu kwa hizi timu kubwa huwa anakamia sana usishangae akatusumbua inatakiwa tuwe na taadhari sana
 
Mkuu wale hawana lolote. Wale ni timu inayokania timu kubwa tu lkn wakikutana na timu ndogo inacheza hovyo. Hiyo sio Sawa lazima timu icheze Ktk kiwango kile kile ata km inacheza na timu kubwa au ndogo. Alafu walituotea tu pale awali lkn tukienda kwao watajuta.
mkuu Ntuzu hawa liver hata kwa timu ndogo wameimprove sana yaani si timu ya kuiondoa ktk ubingwa
 
uzi utaajaa picha za messi kuanzia asubuhi mpaka usiku!

kwa ufupi itakuwa sio uzi wa barcelona bali uzi wa promo kwa messi.
kwani ni sababu ipi inayokufanya umchukie King
 
simchukii ila wewe una mahabati yaliyopitiliza kwa messi,

hata akinya uwanjani utamsifu tu!
Mimi huwa naongea ukweli mtupu na sina mahaba kwa mchezaji yeyote Kama King akifanya vizur namsifia na akiboronga namponda
 
usiitoe liver mkuu nawaogopa sana wale jamaa mwaka huu wako kwenye form

Mkuu Liver wapo vizuri sana mbele pale, ila kiungo yao na beki yao bado sana ndio maana wanafunga mengi na kufungwa mengi. Tukicheza nao tukifanikiwa kumiliki kiungo na kukata mawasiliano kati ya kiungo chao na forward yao tutakuwa tumemaliza kazi. Maana lazima akina Mane na wenzake waje kutafuta mpira kati hapo ndipo utaona Chelsea anacheza 3-5-2 na tutashinda tu. Pia la msingi ni kuhakikisha hawakai na mpira kama tunavyoziachia timu nyinge hizi.

spurs huwa wanamkamia chelsea tu na wala spurs hata big 4 sidhani kama wataingia ila liver ndugu yangu kwa hizi timu kubwa huwa anakamia sana usishangae akatusumbua inatakiwa tuwe na taadhari sana

Spurs lazima watukamie maana kwanza ni London Derby, ila wanafungika sana. watakuja na mchezo wao ule ule wasiku ile na tutawamudu vizuri naamini.
 
wadau ligi bado iko tight mno liver bado anatung'ang'ania hataki tuongeze gape la point 6 ngoja tusubiri mechi ya liver na man city hapa ndipo tutajua liver ipo serious au nguvu za soda

Kwa kweli Liver anatukaba sana sana,

Kwa mechi yao na City, Liver wana asilimia kubwa ya kushinda, wako wepesi zaidi ya City, city ni wazito sana hasa viungo na mabeki hawataiweza kasi ya Liver,
Liver atadondosha point kwa vitumu vidogo au timu kubwa kama Chelsea, Man na Totenham
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom