Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Nadhani suala si formation ila ni rotation ya wachezaji, hiyo formation si ndio inatumiwa mpaka na academy? na labla kuswitch baadhi ya positions za wachezaji,
Kwa mfano me nadhani ni muda muafaka sasa Hazard awe anacheza kama no.10, aongezee creativity pale katikati na kumsaidia Fabregas kupasua kuta ngumu na hii itawapa nafasi wachezaji wengine kucheza winga ya kushoto, mtu kama Cuadrado au Remy
Just imagine Hazard acheze nyuma ya mshambuliaji, zile chenga zake, uwezo wake wa kuumiliki mpira, atakua anatengeneza magoli na nafasi ngapi kwa wenzake kufunga? Tofauti na kule pembeni ambako pamoja na mchango mkubwa anaotoa bado nahisi anaweza kusababisha madhara makubwa akicheza kama no.10

Fomesheni kutumika na academy sio ishu sana... Solanke si ndo mshambuliaji wa U-21 yuko vizuri labda akicheza peke take mbele.. Na juzi kapasha na timu ya taifa ya wakubwa.. He is good.

Mabadiliko ni muhimu na fomesheni pia, ambayo itaruhusu tuwe na washambuliaji wawili hadi watatu.
 
Fomesheni kutumika na academy sio ishu sana... Solanke si ndo mshambuliaji wa U-21 yuko vizuri labda akicheza peke take mbele.. Na juzi kapasha na timu ya taifa ya wakubwa.. He is good.

Mabadiliko ni muhimu na fomesheni pia, ambayo itaruhusu tuwe na washambuliaji wawili hadi watatu.

Wewe wasema, kocha wako ana miaka mingapi anatumia 4-2-3-1? Unadhani atakubaliana na wewe unavyosema formation sio muhimu sana?
Yaani kwa sababu team imekosa kasi yake kama ya mwanzoni ndio ubadili mfumo wa uchezaji wakati sababu za kushuka kwa kiwango ziko wazi kabisa? Mbona kabla mwaka hujageuka mfumo huohuo uliwapa mafanikio zaidi, magoli mengi, tight defense, possession, passes n.k
Chelsea na Burnley ndio team zilizotumia wachezaji wachache zaidi katika msimu huu kwenye ligi, huoni hii inaweza kuwa sababu kubwa? Yule Matic aliyekua monster kwenye midfield yuko wapi siku hizi?
Ukienda Barca, team za level zote zinacheza 4-3-3 ndio maana ni rahisi kwa watoto wanaotoka La Masia kufit kwenye team ya wakubwa kwa sababu mfumo na falsafa ya club ni moja kwa level zote.
 
Nimesha andaa dawa ya kukabiriana na hayo mashetani mekundu....mifupa ya nguruwe kila mchezaji atakua nayo mfukoni mwake...lol.
Ntunzu
Ile mechi yenu na Hull inakupa tamaa kuwa mna timu ya kutwaa ubingwa?

Baada ya zile bao 2 kurudi, Mou alianza kupata maumivu ya tumbo na alikimbilia kwenda kujisaidia ikiwa imebakia muda mfupi kufikia mapumziko ya nngwe ya mwanzo.

Remmy aliharibu kabisa utamu wa mechi ile.

Kwa nini Mou hakupeana mkono na Bruce mechi ilipomaliza au alikuwa anakimbilia tena kwa choo?
 
Wewe wasema, kocha wako ana miaka mingapi anatumia 4-2-3-1? Unadhani atakubaliana na wewe unavyosema formation sio muhimu sana?
Yaani kwa sababu team imekosa kasi yake kama ya mwanzoni ndio ubadili mfumo wa uchezaji wakati sababu za kushuka kwa kiwango ziko wazi kabisa? Mbona kabla mwaka hujageuka mfumo huohuo uliwapa mafanikio zaidi, magoli mengi, tight defense, possession, passes n.k
Chelsea na Burnley ndio team zilizotumia wachezaji wachache zaidi katika msimu huu kwenye ligi, huoni hii inaweza kuwa sababu kubwa? Yule Matic aliyekua monster kwenye midfield yuko wapi siku hizi?
Ukienda Barca, team za level zote zinacheza 4-3-3 ndio maana ni rahisi kwa watoto wanaotoka La Masia kufit kwenye team ya wakubwa kwa sababu mfumo na falsafa ya club ni moja kwa level zote.

Hujanipata kamanda.. Nilisema hivi hata kama academy inatumia huo mfumo sio ishu nikimaanisha... Vijana wengi wa Chelsea academy hawatumiki team A (TOFAUTI NA VIJANA WA LA MASIA NA BARCA A) afu pia ni rahisi kuwabadilishia mfumo wale vijana.

Chelsea haitegemei sana academy, pia hili suala la Costa kuwa mshambuliaji pekee pale mbele unalionaje!??

Suala la mabadiliko ya wachezaji ni muhimu sana... Lakini timu ina wachezaji walioko kwa mkopo ktk club nyngne wengi so hakuna wengi wa kubadili...
 
Ntunzu
Ile mechi yenu na Hull inakupa tamaa kuwa mna timu ya kutwaa ubingwa?

Baada ya zile bao 2 kurudi, Mou alianza kupata maumivu ya tumbo na alikimbilia kwenda kujisaidia ikiwa imebakia muda mfupi kufikia mapumziko ya nngwe ya mwanzo.

Remmy aliharibu kabisa utamu wa mechi ile.

Kwa nini Mou hakupeana mkono na Bruce mechi ilipomaliza au alikuwa anakimbilia tena kwa choo?

Nani anaongoza ligi mpk sasa?

Lazima mtu uende kwa choo km unaumwa tumbo la kuendesha....

Remy aliharibu utamu haswaa wa mpira siku hiyo maana ata ktk thread yetu hapa tumepumzika lkn km ingekua mbili mbili basi mpk leo tungekua na kz ya kuwajibu hoja zao wakaanga sumu.....maana chelsea ndio habari inayouza ktk vyombo vya vya habari vingi....ata wewe umekua na likizo kidogo baada ya remy kuharbu utamu wa mpira....

Kafungwa LFC juzi lkn sijaona thread ya LFC kuvamiwa na kina Nonda.....lkn chesea angepata sare na Hull City haki ya nani tungekoma sie.....lol.


Mou alikua anakimbia tena kwa choo mkuu...na si lazima kupeana mkono......
 
Hujanipata kamanda.. Nilisema hivi hata kama academy inatumia huo mfumo sio ishu nikimaanisha... Vijana wengi wa Chelsea academy hawatumiki team A (TOFAUTI NA VIJANA WA LA MASIA NA BARCA A) afu pia ni rahisi kuwabadilishia mfumo wale vijana.

Chelsea haitegemei sana academy, pia hili suala la Costa kuwa mshambuliaji pekee pale mbele unalionaje!??

Suala la mabadiliko ya wachezaji ni muhimu sana... Lakini timu ina wachezaji walioko kwa mkopo ktk club nyngne wengi so hakuna wengi wa kubadili...


Mkuu kuchezesha strikers wawili ni sawa lkn km utachezesha hao wawili mmoja lazima akae pembeni na awe na uwezo wa kudrive mipira na kuingia nayo....sasa kwa chelsea ni nani anaweza hiyo kazi,Remy au Costa? Au km wote strikers utawaweka katikati basi mfumo hautokua km huu wanaocheza sasa, lazima ubadilike....Angalia PSG, PSG wako na Ibra,huyu Ibra wanamchezsha katikati na Cavani inamlazimu acheze akitokea pembeni...lkn Cavani anaonekana kufaya vizuri na kufunga magoli kutokana na uwezo wake na Ibra na yeye akiwa kati anafaya vzr pia...sasa sisi chelsea tuna strikers wa aina km ya Cavani? Costa ni mtu wa kusubiri mipira.....uwezo wake wa kuendesha mipira ni mdogo sn sio km Cavani....Remy kidogo anaweza hiyo kazi ingawa sio km Cavani alivo na uwezo....kwahiyo mkuu mimi bado naona kuchezesha mshambuliaji mmoja ni vzr tu ila wawe wanapewa nafasi ya kucheza wote...

Na pia kuna hoja moja amesema Mourinho hapo nyuma ya kuwabadilisha wachezaji sehemu zao za kucheza, hilo mimi naliunga mkono kabisa hasa km Hazard atapangwa kucheza namba kumi nyuma ya striker....hii itafanya kz sn hasa kutokana na ule uwezo wa Hazard kungia na mipira ndani....tunaweza kuliona hili lilifanikiwa ktk timu ya Fc Barcelona walipomtoa Messi kucheza pembeni na kumuweka acheze kati....hii iliwapa uwezo wa kupangua ngome yoyo ile na kufunga magoli.....
 
Last edited by a moderator:
Mpaka kesho ntaendelea kumkubali mourinho ila kuwauza de bruyne na mata ni pigo kubwa sana kwa chelsea haka ka0scar kanazingua tu chelsea kanavurunda kakienda brazil ndo kanacheza fresh
 
Mpaka kesho ntaendelea kumkubali mourinho ila kuwauza de bruyne na mata ni pigo kubwa sana kwa chelsea haka ka0scar kanazingua tu chelsea kanavurunda kakienda brazil ndo kanacheza fresh

hapo ni de brune tu , matta hana kitu mkuu
 
Mpaka kesho ntaendelea kumkubali mourinho ila kuwauza de bruyne na mata ni pigo kubwa sana kwa chelsea haka ka0scar kanazingua tu chelsea kanavurunda kakienda brazil ndo kanacheza fresh

Hapo utaishia kuwataja wote na kuhisi kama Mou alikosea...D Luiz akiwa PSG unamuona? Schurrle? Mo Salah? Demba Ba (huyu si ndo aliwatoa kina Malafyale ??!)...et al et al..
 
Last edited by a moderator:
Ntuzu;

Mkuu.. Hazard ukimfanya acheze kama INSIDE LEFT maana yake unaeza chezesha hao watu wawili ktk 4-1-3-2 lakini kama hiyo haitoshi bado 4-3-3 tunaiweza, Costa sio mshambuliaji wa kusimama peke yake hasa ktk EPL
 
Last edited by a moderator:
Nani anaongoza ligi mpk sasa?

......
Mou alikua anakimbia tena kwa choo mkuu...na si lazima kupeana mkono......

Kuongoza ligi sio kuwa "Bingwa". Ngoja muda fupi ijayo tutapata mwanga zaidi wa kujua kama ni Man City, Man United, Arsenal au Liverpool ndio anatwaa taji la EPL. Mimi naipa Chelsea kumaliza ligi katika nafasi ya tatu au ya nne.

Ntuzu kwa nini unamtetea Mou kwa kufanya umafiaso ( dharau). Mechi alishinda dakika za mwisho, ingawaje alikuwa tayari amechanganyikiwa, alijua anatota sare. Si uliona alikuwa pia nataka kumwingiza Cuadrado na alikuwa hafatilii kinachoendelea uwanjani, akaambiwa Remy amemuokoa. Na Mou akapiga chini wazo la kumwingiza Cuadrado.
Sasa kwa nini alikimbia kumpa mkono Bruce?

Kweli kupeana mkono si lazima lakini ile ni alama ya sportsmanship au???

Unakwenda nyumbani kwa watu na unafanya "madharau" kwa "host" wako?

What Mou did was a "class act" in the contrary!! and my ndugu, Ntunzu thinks it is just fine.
Mhh. Interesting!
 
Hapo utaishia kuwataja wote na kuhisi kama Mou alikosea...D Luiz akiwa PSG unamuona? Schurrle? Mo Salah? Demba Ba (huyu si ndo aliwatoa kina Malafyale ??!)...et al et al..

Mata, De Bruyne, Salah ni wachezaji ambao ni wazuri kushambulia tatizo José anataka wewe wanarudi kukaba kitu ambacho hawawezi, Oscar na Willian walikuwa wazuri sana but José kawabana na mfumo wake wanaonekana wabovu, Muda unavyozidi kwenda Oscar anazidi kuporomoka . So far sijaona sana Pengo la Luiz, Zouma anacheza vizuri sana(CB , DM). Andrea Schurle huyu ni mchezaji anayefaa mfumo wa Mourinho sijui kwa nini alimuuza
 
Last edited by a moderator:
Waungwana mmesikia Chelsea wanamuwania Gareth Bale? Hebu tu imagine Chelsea ikiwa na Gareth Bale utakuwaje...!
 
kalou Ntuzu Manumbu everlenk

Naona mpo kinywa sana au sababu siku za kucheza na Majogoo zimekaribia sasa mmekosa raha?

Majogoo yakiwa kamili hayafungwi ya yyt yule EPL!Majogoo tunaenda kuwika Emirates



Umekuja na huku mkuu!!!!! Kweli IMBOMBO JILIPO.......

Mkuu unapoona ukimya basi ujue kua mambo yote yako shwari kabisa!

Wewe utakuja kwetu tarehe 9 mwezi ujao siku hiyo utakuja tufanye sherehe ya kukabidhiwa kombe
 
Last edited by a moderator:
kalou Ntuzu Manumbu everlenk

Naona mpo kinywa sana au sababu siku za kucheza na Majogoo zimekaribia sasa mmekosa raha?

Majogoo yakiwa kamili hayafungwi ya yyt yule EPL!Majogoo tunaenda kuwika Emirates

Majogoo yameshapigwa mechi 8 kwenye ligi kuu msimu huu, inaonekana majogoo yanamatatizo ya kuwa "kamili"
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom