Ni kweli formation hiyo ndio imetufikisha hapo tulipo na pia ni ukweli kwamba tangu second part ya season ianze, tumetaabika kiasi flani huku tukitoa draws mechi tulizopaswa kushinda. Inawezekana sana labda wachezaji wamechoka au team pinzani sasa zinapredict tutachezaje, ukichukulia 97% ya starting eleven na/au formation yetu inafahamika vizuri.
Mkuu kuna vitu vichache ningependa kuongelea juu ya timu yetu pamoja timu tunazokutana nazo na mifumo yote kwa ujumla.
Kwanza kuhusu mfumo wetu....huu mfumo karibu timu nyingyi siku hizi zinatumia...huu mfumo unasaidia timu kushambulia kupitia sehemu zote.....Fc Barcelona wamekua wakiutumia sn na B Munich...na sasa umetapakaa karibu timu nyingi pamoja na kua huu mfumo ulikuwepo muda mrefu....
Changamto ambazo timu yetu inakutana nazo siku hizi nyingi sn....nikianza na Costa...Costa ni leading top scorer wa EPl kwahiyo timu tunazokutana nazo zinakuja zikiwa tayari wameshamsoma vzr na marking kwake inakua kubwa ikiwa na kumchezea hovyo ili kumtoa ktk kucheza mpira na kumfanya achukie na.....nafikiri km unafatilia vituko anavofanyiwa uwanjani Costa utaliona hilo....
Ufumbuzi juu ya swala la Costa ni bora aanzie benchi kipindi cha kwanza na cha pili aingie hii itatusaidia kucheza mpira wa kasi kipindi cha kwanza na kipindi cha pili akiingia Costa basi mabeki wengi watakua wamechoka na zile vurugu zake basi atakua anatupia kirahisi tu.
Swala jingine ni km hilo la Costa...Fabregas ni top assist wa EPL mpk sasa kwahiyo timu pinza zinakutana na sisi zinakua zinajua hili vema kiasi kwamba huyu bwana atakabwa na kufanyiwa vurugu zote mpk asipate nafasi kufanya yake....hii ina aplly na kwa Hazard pia. Na yeye ndio hivo hivo ni taabu tu.
Ni wakati sasa wa Mou kuwapa dakika 45 au 70 au 30 kwa hawa watu kucheza...hii itasaidia kuwapa nguvu iwapo watatokea bench au wakianza ingawa ni muhimu kuanza na full mkoba lkn km ni mechi kubwa basi waanze lkn km ni mechi ndogo waanzie benchi.
Matic, huyu jamaa sasaivi ameanza kuchoka na hii inatokana na kucheza kwa muda mrefu bila kupata msaada hasa kutokana na Obi kua majeruhi na Ramires kua majeruhi pia ingawa sasa Ramires amerudi na anafanya vzr lkn tunahitaji pacha pale kati km Obi na Ramires ili Matic na yeye apate kupumzika ndio maana unaona ata Mou siku hizi anamtupia Zouma ktk hiyo nafasi ili kupata angalau wachezaji ktk hiyo nafasi. Na wapinzani wanajua kua uimara wa ngome yetu unajengwa na Matic sasa wakikutana na sisi wanacheza mipira ya kasi na mirefu na ya kushitukiza km ya Hull city juzi....Lkn nafikiri Obi yuko karibu kurudi na ktk mchezo wetu na ManU tutamuona uwanjani akiwa na Matic....
Kuna mengi sn unaweza ukasema lkn kwa sasa ngoja niishie hapa ila kubwa ni kwamba sasaivi timu iko sawa na itafanya vzr ktk michezo yote iliobaki.