Maisha baada ya Kibongo cha 5-3:
Hakuna mwana chelsea yoyote ambaye alitegemea kibondo kikubwa namna ile, binafsi nilishuhudia dakika zote 90, baada ya jamaa kupata bao la tatu, nikamwambia jirani yangu kwamba kocha lazima ataanza game ya kushambulia zaidi - utaona Full backs zote zinapanda mbele na kuacha nyuma uwazi. Athari yake ni kwamba kama tukipoteza mipira mingi kwenye midfield basi tunaweza kufungwa hata bao 6 kwa counter attack, unless tufunge haraka mabao mawili iwe 4-3 ili kocha abadilishe mfumo tena.
Jamaa akaniambia, mzee mzima huko umefika mbali bao sita zitoke wapi, hawa mbona wa kwetu leo.
Oooh mara bao la 4, nikamwambia unaona?, lakini mimi nikabaki na kauli yangu ile ile - hatimaye yakaingia mengine 2 na tukawa tumelala 5-2, kipigo cha mtoto mtukutu tukawa tumekipata.
Way Foward
Mimi namshauri kocha machachari kuangalia uwezekano wa kumpumzisha JT, Metic na Fabregas hii ni kutokana na wao kucheza mechi nyingi bila mapumziko. Kuna mmakonde nafikiri kwa sasa yupo fit basi apewe nafasi ya ku-hold. Hasa ukizingatia umri wa kepteni wetu kweli umesonga kwa sasa.
Wote mmeona game ya juzi na Watford, alipumzisha akina JT, Ivanovic, Fabregas, Metic, Hazard na Kipa wetu Thibaut. Jumla ya wachezaje Key 6 kwenye line yetu ya kwanza ya primership ya vijana wale wakali tukawashindiliamo bao 3 bila majibu.
Hii ni way forward, naungana na Metic kwamba makombe 4 yanawezekana, WHY NOT??