Ntuzu
JF-Expert Member
- Aug 8, 2013
- 17,418
- 10,877
Nahisi hasira na usongo mkali darajani...na hata humu jukwaani. darajani nahisi kuna hii hali:
1. Hasira za kukisahau kipigo cha Tottenham. hasira hizi zitaisha kama kitatolewa kipigo cha mbwa mwizi.
2. Nahisi kipigo hiki kitatolewa kwa Newcastle wiki endi hii
3. Nahisi pia hasira za kulipiza nuksi waliyotuanzishia hawa Newcastle kwao St. James Park. Na hili ukijumlisha na Namba 1 na namba 2 hapo juu, inahamasisha hasira ya kuwapiga Newcastle zaidi ya hizo bao 5 tulizopigwa sisi tena bila majibu!
4. Nahisi pia kuna presha kwa wachezaji kujituma zaidi ili wasije wakakatwa pindi uvumi wa ujio wa Messi utakapokuwa kweli. sitashangaa kuwaona watu kama Schurrle na Salah wakijituma zaidi na kujikakamua zaidi kulinda namba zao au kutengeneza opportunities za kuchukuliwa na timu kubwa pindi watakapoonekana kutolewa
5. Nahisi pia tutataka kutoa onyo kwa game ijayo na Man City kuwa kudondoka kwetu kwa hvi karibuni kumefikia kikomo na tunataka kufungua tena gap la point lililokuwepo awali, hususan kwa vile mechi na Man City iko tu jirani.
Wadau Ntuzu kalou Viol Mentor na wengineo mnasemaje? Karibuni tuijadili timu yetu na mikakati yetu. tuachane kubishana na wanaotucheka. hao watatucheka tu siku zote tufungwapo. ila hatutawaona tushindapo
Mkuu Manumbu nimekua tait sn kwa muda mfupi lkn soon nitakua na nafasi na kuweza kuingia humu mara kwa mara.
Kuhusu mchezo wetu na hao Newcastle kuwafunga hilo ni lazima watake wasitake.
pamoja sn mkuu
Last edited by a moderator: