Wao wana pesa Chadema tuna Mungu aliye hai
Kamanda! Kwa nini msichukue pesa kwenye mfuko wa M4C mkalete mabadiliko Chalinze.
Teh teh teh ebu acheni usanii yani unaji PM mwenyewe.asante sana mkuu nimepokea tzs 30,000 kutoka kwako..
shakamo bibi naomba mchango wako..
Kwani zile pesa za Chopa Kalenga nani alikuwa anatoa, mimi tachangia 50,000 lakini nataka kujua mchanganuo wa matumizi.
Crashwise nimetuma laki mbili kwa ajili ya kukomboa nchi, hawa voda wanasema imetumwa kwa AGNES BELA, ndio wewe nini?
mkuu. agnes bela ni cashier pale ufipa.
mkuu. agnes bela ni cashier pale ufipa.
Tena wasituzoee kabisa pesa wanakwenda kutumia pikiniki na familia zao halafu leo ndiyo wanatuletea mambo ya ajabu hapa.Mnataka kushindana kununuwa majumba Dubai?
Mbona wanasema ni ni namba ya CHADEMA MTANDAONI?
Chadema lakuvunda tukiwachangia wanapelekea wake zao mambo gani haya waende zao bana ruzuku wanagawana kifamilia tena wanataka michango toka kwetu hii sacos sasa inakufa kabisa.
Tuambiwe kwanza ile michango inayotolewa kwenye mikutano ya hadhara inatumikaje kwa maana ya mchanganuao vinginevyo tuheshimiane na tuishi kwa adabu.