Wanabodi,
Ili chama fulani kishinde uchaguzi na kupata mamlaka ya kuunda serikali, lazima chama hicho kipate asilimia fulani ya idadi ya viti bungeni!. Hivyo kama CCM itapata pungufu ya asilimia inayohitaji kuunda serikali, lazima ifanye coalition na the underdogs, ili kuweza kupata idadi ya viti vinavyotakiwa kuunda serikali.
Ujio wa ACT, unaweza kuwa ndio mwanzo wa the underdogs wa Tanzania, yaani for the first time in Tanzania, tunaingia kwenye uchaguzi mkuu wa vyama vingi tukiwa na vyama vikuu viwili "the dominant parties, CCM na UKAWA, ambao ndio serious contenders, lakini pembeni kuna ka small parties ambao wanajijua kabisa kuwa hawana watu, hawana uwezo, wala hawawezi kushinda uchaguzi, ila wataweka tuu mgombea kwenye kila jimbo na hadi mgombea urais kwa lengo moja tuu, sio kushinda uchaguzi bali kuzigawa kura za 'the dominant parties' hivyo hawa "the underdog" ndio determinant yachama gani kitaunda serikali, nikimaanisha iwapo hivi vyama viwili CCM na UKAWA havitafikia idadi ya viti inavyovihitaji kuunda serikali, lazima vishirikiane na "the undedog" ambao kwa kawaida wanaweza kuwa na mbunge mmoja au wawili watatu, ili viweze kupata mandate ya kuunda serikali!, na itakuwa ni serikali ya mseto!.
Hivyo ndugu zangu Chadema na WanaUkawa, mtake msitake, ACT sio chama cha kupuuzwa hata kidogo!. Mnaweza kuendelea kumpuuza Zitto kama Zitto Zuberi Kabwe, lakini hamuwezi kuumpuuza Zitto kama Kiongozi Mkuu wa ACT, unless Chadema na UKAWA, mnataka kuwa vyama cha upinzani milele!.
Kumbukeni kwenye siasa, hakuna rafiki wa kudumu, wala adui wa kudumu, bali a common interest!, kama ni kweli IKULU mnaitaka, na ACT inaweza kuwa ndio kikwazo pekee, then lazima pia mta deal na ACT as well ether kuibomoa ili isiwe kikwazo, na ikitokea if you can't beat them, UKAWA will be forced to join them against CCM!.
Pasco.