CHADEMA wazungumze na Zitto na ACT

CHADEMA wazungumze na Zitto na ACT

Mkuu utaona sijasema akaribishwe moja kwa moja UKAWA
nimesema tu CHADEMA waanze kuzungumza nae...labda anataka majimbo mawili tu au matatu
aachiwe na UKAWA au jimbo lake tu moja....na wao wana UKAWA in return wanaweza kumpa masharti
labda ACT wasisimamishe mgombea kwa Lissu na Mdee....na hapo labda ukawa 'mwanzo mpya'

Wanasema in Politics there are no permanent enemies nor permanent friends....

Tuko kwenye kipindi cha demokrasia Zitto na ACT wanahaki ya kusimamisha wagombea mahali popote palipo na wagombea wa CHADEMA ili mladi hawako ndani ya UKAWA hata kama watasimamisha wagombea watatu watatu kwa mgombea mmoja wa CHADEMA poa tu,kwani lengo lao siyo kushinda bali ni kutaka kuidhofisha CHADEMA.
 
Lissu na Mdee kwangu ni watu muhimu bungeni
kama wewe ni mwana CHADEMA na unafikiri hao wako equal na wagombea wote wa CHADEMA kina
Shibuda na Msigwa basi hata wewe ni kazi bure kukuelewesha
sio Lissu na Mdee hata Mnyika anapaswa kupewa free pass na upinzani wote

Free pass ambayo hao wabunge wataupata kutoka kwa vyama vingine vinavyounda UKAWA unawatosha. Lakini pia unavyosema 'Free Pass' ieleweke kuwa kuna upinzani wa UKAWA kutoka vyama vingine sio tu ACT. Tusiongee kama vile nje ya UKAWA kuna ACT peke yake. Hata hivyo Chama ambacho sio tu hakina mbunge, hakijapata usajili wa kudumu hakiwezi kuwang'oa hao wabunge uliowataja hata kama Zitto akikomaa na hayo majimbo peke yake. Huyu jamaa 'popularity' yake ilipanda kwa sabab kazi yake bungeni enzi hizo, ila sasa hivi 'popularity' yake ina image ya 'usaliti' kitu ambacho kinammaliza kisiasa taratibu.
 
Mkuu The Boss, ili kuweza kufanya kitu kinachomake sense, kwanza, ni hao wahusika wawe na uwezo 'ability' to see that sense!, ndipo then wafanye maamuzi yanayomake that sense!, hao wenye uwezo wa kuona hiyo sense huko Chadema wapo?!. I don't think!.

Pasco.
Tunapingana na hiyo sense unayoizungumzia. Kwako sense ni UKAWA au Chadema kukaribisha ACT-Wazalendo, chama kilichofadhiliwa na CCM. Kwetu sisi sense ni kuachana na wale ambao walikuwa wakivujisha siri za chama kwa CCM na usalama wa taifa eti wanaona ni tija kuwa na uhusiano na maafisa wakuu wa usalama wa taifa. Uhusiano gani? Obama katika kampeni zake hakuona umuhimu wa kuwa na uhusiano na CIA kwa sababu alijua CIA ni chombo cha serikali kinachopaswa kumtii yeyote atakayechaguliwa na Wamarekani kuwa kiongozi wao.l Kwa hiyo kama viongozi wa Chadema hawana sense mimi nataka waendelee hivyo hivyo.
 
Tuko kwenye kipindi cha demokrasia Zitto na ACT wanahaki ya kusimamisha wagombea mahali popote palipo na wagombea wa CHADEMA ili mladi hawako ndani ya UKAWA hata kama watasimamisha wagombea watatu watatu kwa mgombea mmoja wa CHADEMA poa tu,kwani lengo lao siyo kushinda bali ni kutaka kuidhofisha CHADEMA.

Zitto akiendelea kusambaza uzalendo UKAWA wasahau uraisi ni bora wakalime mahindi maana huyu panya ni shidaaaaaaaaaaa kazi yake ni kutoboa magunia ya mahindi af anayeyaaaaaaa... kitaeleweka tu october nani ataamua kura za raisi indirectly :loco:
 
Kama ACT wazalendo ni wapinzani wa kweli na kama wa nania ya kweli ya kutaka kuing'oa CCM na kama wanaamini kuwa kile wanachokifanya kinawaharibia wapinzani katika juhudi zao za kutaka kuing'oa CCM madarakani,ACT ndio wanaotakiwa wawe wa kwanza kuacha mambo yao yanayorudisha nyuma harakati za kuiondoa CCM madarakani.

Wasisubiri kuombwa wakati wameshajitangaza kuwa ni wapinzani,vinginevyo watu tutazidi kuwa na walakini na upinzani wao.
 
Kuna kitu naona unakisahau
Enzi za TANU na Mtevu angala chaguzi zilikuwa fair..
enzi hizi chaguzi zina 'all dirty tricks'

Mtemvu hakuwahikushinda lolote before,Zitto kashinda twice uchaguzi
enzi hizi zenye 'all dirty tricks' na kashiriki mipango mingi ya CHADEMA iliyopelekea CHADEMA kushinda
majimbo......hate him but he is no fool....akiamua kuijeruhi CHADEMA anaweza...kuzungumza nae
kunaweza saidia sana tu.....hasa kama atapata 'a little respect' from CHADEMA...nafikiri
ni Abraham Lincoln aliwahi sema 'i destroy my enemies by making them my friends'

Kwa mtazamo wako unaona kuwa Zitto ni kila kitu. Kumbuka kuwa CHADEMA wamezungumza sana na Zitto akiwa ndani ya chama na wamemshauri kwa mengi lakini hakutaka kuckia hatimae akatimuliwa. Uonavyo ww Leo hii ndio Zitto atawackiliza CHADEMA akiwa nje ya CHADEMA???. Hapana hapa nakataa, CHADEMA kama chama wamemfukuza Zitto inatosha hawawezi kumrudia Zitto kumbembeleza eti kisa Lisu atakosa kura Singida. Kama ndio ivyo unavyoamini basi Zitto ndio rais wako kama anaweza kuchukua majimbo yote hayo. Zitto aende kwa Mdee, Lisu, Mnyika na kuwapigia kampeni wagombea wa ACT na kuwashinda Ukawa. Kweli unawaza mbali, na hapo hapo nae ajipigie kampeni. Yani mtu ametenda makosa asiadhibiwe eti kisa Lisu atakosa ubunge, CHADEMA wanasema acha Lisu akose ubunge lakini hawawezi kumwomba msamaha Zitto au kumwomba arudi. Nguvu ya Zitto inatokana na ccm subiri uchaguzi uishe kama utaisikia Act. CHADEMA Co ccm wenye kuwakumbatia watu hata ukiwa na kosa kisa chama kitakosa madaraka. Nasubiri kuona io nguvu ya Zitto ya kuishinda Ukawa
 
Kwa mgogoro uliofukuta kwa mda mrefu kati ya Chadema na Zitto nadhani mpaka sasa Chadema wanamakovu mengi sana yaliyosabishwa na huyu Zitto.

Mpaka Wanaamua kumfukuza waliangalia vitu vingi ikiwemo faida na hasara za Chama.

Zitto alisema hawezi kuomba msamaha kwenye chama wakati yeye anajua hahusiki na tuhuma alizoelekezw. Hamuwezi kusameheana kama mmoja wenu hataki kukiri makosa.

Unataka Chadema wambombe msamaha Zitto, kwamba samahani tulikusingizia shutuma dhidi yako zilikuwa za uongo. Je ni jambo linalowezekana.?

Kama sivyo hivyo Zitto yupo tayari kukubali makosa yake, ili afungue ukurasa mpya wa mazungumzo na Chama.

Huyu huyu Zitto wakati wenzie wanaunda ukawa Bungeni yeye aliunda kinachoitwa DARAJA sijui alikuwa na malengo gani.

Kiukweli Zitto hana morali wa kufanya kazi kama timu.Akijiunga na UKAWA Tutaanza kusikia Zitto amesema badala ya Ukawa wamesema

Na vipi Zitto aongee na Chadema na Sio ACT na Chadema?

Maana kumrudisha Zitto Sawa na kuikubali Taasisi nzima ya ACT.Vipi akina Kitila, Mwigamba na Wengineo Mtawaweka wapi.? Kama unavyojua karibia act nzima ni zao la Chadema japo kila mmoja alikuwa na shutuma tofauti.

Ndio Zitto anaweza kukiathiri Chadema, ila Chadema ni taasisi naamini watapambana majukwaani.
 
ZZK ni mwanasiasa msomi na mweledi wa mambo. Binafsi napenda kumfananisha na chumvi. Lakini chumvi inapoharibika utaitia nini ili iwe bora? Kikubwa ni kuitupa. Moja ya sifa za msingi za chama bora cha siasa ni kuenenda kwa kufuata katiba, kanuni na taratibu. Kama kuna wanachama/mwanachama anajiona yupo juu ya katiba, kanuni na taratibu basi hafai. Kama chama hakiwezi kusimamia katiba, kanuni na taratibu basi hakifai maana chama kinaposhinda uchaguzi na kuunda serikali kazi yake kubwa ni kulinda na kuhifadhi katiba&sheria. Kama hilo hawawezi basi hawasitahili kupewa ridhaa ya kutawala.
 
Ushauri wangu kwa Zitto nimeutoa humu
kuna thread nimesema Zitto ajifunze kusema 'we' na 'sisi'
kama anataka 'bright future'ya kisiasa..ukisoma between the line ni ushauri mkubwa

Kuhusu hiyo ya mimi kuamini wenye Obession...well you can ignore me
kumbuka CHADEMA hawa deal na mimi hapa......but Zitto is out there kuendelea kumuita msaliti na kum ignore
na the fact yeye Zitto ana 'machungu' yake binafsi na individuals ndani ya CHADEMA kutapekelea asiwe
na kizuizi cha kuweka wagombea kwenye majimbo ambayo tunapenda kuona wabunge wake wakirudi bungeni
hivi Suppose ACT waweke mgombea kwa Tundu Lissu achukue kura za kutosha hadi Lissu ashindwe
unafikiri hilo ni jeraha dogo?
the way kuzuia hilo ni ku negotiate na Zitto baasi

Mkuu The Boss yaani nimekudharau kabisa unaposema eti Zitto anaweza weka mtu jimboni kwa Lissu eti akamshinda Lissu....dude what are u drinking?

Yaani kwa utashi wako unaona kuna mtu yeyote,narudia yeyote,anaeweza kuchukua jimbo la Lissu Tanzania ya leo hii??Stop smoking man!
 
Mkuu The Boss, hii ni kitu inayoitwa busara za hali ya juu!, it is very unfortunately, Chadema haina watu wenye busara za level hii, wengi wao wanatawaliwa na chuki dhidi ya Zitto, hawataki kuchukua 'tahadhari yoyote kabla ya hatari', bali wako tayari kwa 'majuto ni mjukuu!'. Maadam umesema kuhusu wenye akili wanafanya nini na wajinga watafanya nini, sisi tukiwaita watu ni wajinga humu, tutashutumiwa tunawatukana!, nasisitiza Watanzania kama hawako tayari kuwaingiza 'wajinga' kwenye ikulu yao!.

Kuliko kuingia ikulu na ujinga wao, bora wakae na ujinga wao huko huko, mpaka watakapo pata akili ndipo tuwakabidhi ikulu yetu!.

Pasco

U are always a bandwagoner!Always!
 
Mkuu The Boss yaani nimekudharau kabisa unaposema eti Zitto anaweza weka mtu jimboni kwa Lissu eti akamshinda Lissu....dude what are u drinking?

Yaani kwa utashi wako unaona kuna mtu yeyote,narudia yeyote,anaeweza kuchukua jimbo la Lissu Tanzania ya leo hii??Stop smoking man!


Soma vizuri sijasema atamuweka mtu ashinde
nimesema kura za upinzani zinaweza kupungua jimbo likapotea
kurudi CCM.....
 
Soma vizuri sijasema atamuweka mtu ashinde
nimesema kura za upinzani zinaweza kupungua jimbo likapotea
kurudi CCM.....

Hayo mahesabu yako yana poor basis. Hata hivo hiyo ndio kazi yake anayolipwa, kupunguza kura za upinzani. Vyovyote vile hayo majimbo yaturudi CDM. Jiulize yeye ZZK kuna uwezekano wa kurudi bungeni ?
 
Kama ikitokea Zitto afanikiwe kugawa kura kwa nia ya kumkomoa Lisu,Mnyika,Mbowe,Msigwa,Silinde,Sugu na majembe mengine ya CDM,NCCR na CUF,basi ninaogopa kuibashiria nchi yangu mabaya lakini watu hawa wanaotaabika taifa hili,sidhani kama wataogopa tena kuchukua hatua sitahiki kwa huyu aliyeamua kufanya hivi.Kumbuka kung'oka kwa ccm siyo faida kwa CDM na washirika wake tu,bali ni hatua ya Taifa kuzaliwa upya na hivyo wananchi watapumua huku wakiwa na matumaini ya angalau maisha yanayojali hadhi ya ubinadamu
 
mkuu hakuna namna yoyote kwa cdm kuhangaika na zitto ; hakuna , kamati kuu iliangalia mengi sana kabla ya kumtimua ,nakuhakikishia kwamba zitto hana na wala hataweza kuwa na madhara kwa cdm iliyofika hapa ilipo baada ya tabu nyingi ikiwemo damu ya watu .CC - PASCO .
 
Mkuu The Boss, hii ni kitu inayoitwa busara za hali ya juu!, it is very unfortunately, Chadema haina watu wenye busara za level hii, wengi wao wanatawaliwa na chuki dhidi ya Zitto, hawataki kuchukua 'tahadhari yoyote kabla ya hatari', bali wako tayari kwa 'majuto ni mjukuu!'. Maadam umesema kuhusu wenye akili wanafanya nini na wajinga watafanya nini, sisi tukiwaita watu ni wajinga humu, tutashutumiwa tunawatukana!, nasisitiza Watanzania kama hawako tayari kuwaingiza 'wajinga' kwenye ikulu yao!.

Kuliko kuingia ikulu na ujinga wao, bora wakae na ujinga wao huko huko, mpaka watakapo pata akili ndipo tuwakabidhi ikulu yetu!.

Pasco

Pasco unakuwaga kama umedata flani muda mwingine! wewe unayekesha ukimlilia Zitto na ACT kwanini Team MAMVI msimchukue?! mnajua kwamba CHADEMA wamecheza karata yao vizuri kuelekea 2015-wasaliti wapo nje sasa!--HIKI NDICHO KINACHOWAUMIZA team Mamvi+Magamba woote!
 
Soma vizuri sijasema atamuweka mtu ashinde
nimesema kura za upinzani zinaweza kupungua jimbo likapotea
kurudi CCM.....
kwa ushawishi gani alionao zitto ambaye nchi nzima inafahamu kuhusu usaliti wake ? hii mikutano anayofanya haitofautiani
na mbio za mwenge , ametembea mikoa kumi plus lakini hakuna mahali wamefanya hata kijiofisi uchwara , siasa si rahisi kama unavyodhani , umewahi kuhudhuria tamasha la airtel coco beach ? hakika unaweza kudhani hakuna mtandao mwingine nchi hii ! msingi uliojengwa na cdm nchi hii hakuna anayeweza kubomoa , kwa mfano mkoa kama mbeya wala hata hawamjui kabisa huyu msaliti .
 
Sina hakika una maanisha Zitto na ACT Tanzania?Wazalendo? yake na CHADEMA wa negotiate nini iwapo ni juzi tu walikuwa pamoja na yet negotiation ilishindikana na badala yake Zitto akaamua kutumia mahakama kama namna yake ya negotiate?..To me, this is too late and it's absolutely impossible!!

Na hii maana yake ni moja tu, kwamba,tukutane katika uwanja wa mapambano ya kisiasa na hukohuko atajulikana nani mwanaume.

Tulicho na uhakika nacho ni kuwa huyu kibaraka wa CCM na hiyo organization yake inayoitwa ACT WASALITI INC. hawana lolote, period!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom