CHADEMA si chama cha wananchi, ni kikundi tu cha watu wanaotaka kushika madaraka

Red Giant

JF-Expert Member
Mar 9, 2012
15,658
20,889
Hiki chama ni kundi tu la watu wanaotaka madaraka. Ukiangalia ugomvi wao wote na dola, kelele zao zote karibu asilimia 90 vinahusu wao kuingia madarakani.

Huwezi kuta CHADEMA wanaingia matatani na vyombo vya dola kisa walikusanyika kutetea wakulima wanaonyonywa na vyama vya ushirika, wanaonyimwa fursa ya kutafuta masoko nje nk. Huwezi kuta wameingia matatani kwa kutetea wafanyakazi kwa vitu kama fao la kujitoa au maslahi. Hawajawahi itisha maandamano kupinga kodi kandamizi kwa wafanyabiashara.

Wao siku zote maandamano yao yanahusu fursa za kuingia madarakani. Tena afdhali kipindi cha Slaa ambapo ilionekana shida kubwa ni ufisadi, na wananchi walichoka. Slaa akaishika hoja hiyo na chama kikapata nguvu kubwa sana.

Chama kinakubali kuingiza watu hata wasioamini kwenye sera zao, lengo lao ni kushika madaraka tu. Chama hiki kibadilike. Kisimamie na kupigania hoja zinazowahusu wananchi moja kwa moja. Mfano kikijaribu kujiweka kuwa mtetezi wa wakulima, kitavuna nguvu nyingi sana. Mtu akisikia kuwa wamekamatwa kwa sababu walikuwa wakipigania unyonyaji wa wakulima wa chai au mahindi inamuingia akikini kukutetea. lakini kwa mtindo huu wa kila siku kupigania namna ya kuingia madarakani kinaweza kufa kabisa.
 
Sorry but this post is of the lowest thinking capacity to the maxmum point!.. CHADEMA ni taasisi iliyoandikishwa kisheria kama chama cha siasa
Kina wana chama kuanzia ngazi ya shina
Kina rasilimali watu
Kina rasilimali vitu
Kina Uongozi kamili kuanzia ngazi ya shina
Kina matawi ndani na nje ya nchi
Kina vitengo vyote muhimu kama chama kikuu cha upinzani
Kina wasomi wakutosha
CHADEMA ni taasisi kubwa na imara inayoheshimika na kutambulikana ndani na nje ya nchi
Kukiita CHADEMA ni kikundi cha watu wachache ni mawazo finyu yaliyopitiliza
 
Na ile siku wataanza movement hizi ndipo watanzania mpaka makaburini watainuka kuingia nao barabarani, hakutakuwa na jeshi lenye silaha litakalowadhibiti tena.

kelele zote za katiba ni sababu wanapigwa kura wakiwa wamesimamakuanzia kwa wakutugenzi NEC mpaka msimamizi wa uchaguzi kituo f.
 
na ile siku wataanza movement hizi ndipo watanzania mpaka makaburini watainuka kuingia nao barabarani,hakutakuwa na jeshi lenye silaha litakalowadhibiti tena.

kelele zote za katiba ni sababu wanapigwa kura wakiwa wamesimamakuanzia kwa wakutugenzi NEC mpaka msimamizi wa uchaguzi kituo f.
Kabisa. Unahitaji tu kugusa wananchi.
 
Bila kuiba kura wasingekuwa hata na wabunge wawili, watu wa ovyo sana hawa CCM ila good news mtatoka tuu tena mapema kuliko mnavyofikiria
 
Hiki chama ni kundi tu la watu wanaotaka madaraka. Ukiangalia ugomvi wao wote na dola, kelele zao zote karibu asilimia 90 vinahusu wao kuingia madarakani...

F20AC9E9-E6DD-428F-A345-A02610C649A1.jpeg
 
Bila kuiba kura wasingekuwa hata na wabunge wawili, watu wa ovyo sana hawa CCM ila good news mtatoka tuu tena mapema kuliko mnavyofikiria
Na CCM ikitoka CDM itafanya nini? Maana inaonekana wao akili yao ni kushika tu madaraka.
 
Back
Top Bottom