Red Giant
JF-Expert Member
- Mar 9, 2012
- 15,658
- 20,889
Hiki chama ni kundi tu la watu wanaotaka madaraka. Ukiangalia ugomvi wao wote na dola, kelele zao zote karibu asilimia 90 vinahusu wao kuingia madarakani.
Huwezi kuta CHADEMA wanaingia matatani na vyombo vya dola kisa walikusanyika kutetea wakulima wanaonyonywa na vyama vya ushirika, wanaonyimwa fursa ya kutafuta masoko nje nk. Huwezi kuta wameingia matatani kwa kutetea wafanyakazi kwa vitu kama fao la kujitoa au maslahi. Hawajawahi itisha maandamano kupinga kodi kandamizi kwa wafanyabiashara.
Wao siku zote maandamano yao yanahusu fursa za kuingia madarakani. Tena afdhali kipindi cha Slaa ambapo ilionekana shida kubwa ni ufisadi, na wananchi walichoka. Slaa akaishika hoja hiyo na chama kikapata nguvu kubwa sana.
Chama kinakubali kuingiza watu hata wasioamini kwenye sera zao, lengo lao ni kushika madaraka tu. Chama hiki kibadilike. Kisimamie na kupigania hoja zinazowahusu wananchi moja kwa moja. Mfano kikijaribu kujiweka kuwa mtetezi wa wakulima, kitavuna nguvu nyingi sana. Mtu akisikia kuwa wamekamatwa kwa sababu walikuwa wakipigania unyonyaji wa wakulima wa chai au mahindi inamuingia akikini kukutetea. lakini kwa mtindo huu wa kila siku kupigania namna ya kuingia madarakani kinaweza kufa kabisa.
Huwezi kuta CHADEMA wanaingia matatani na vyombo vya dola kisa walikusanyika kutetea wakulima wanaonyonywa na vyama vya ushirika, wanaonyimwa fursa ya kutafuta masoko nje nk. Huwezi kuta wameingia matatani kwa kutetea wafanyakazi kwa vitu kama fao la kujitoa au maslahi. Hawajawahi itisha maandamano kupinga kodi kandamizi kwa wafanyabiashara.
Wao siku zote maandamano yao yanahusu fursa za kuingia madarakani. Tena afdhali kipindi cha Slaa ambapo ilionekana shida kubwa ni ufisadi, na wananchi walichoka. Slaa akaishika hoja hiyo na chama kikapata nguvu kubwa sana.
Chama kinakubali kuingiza watu hata wasioamini kwenye sera zao, lengo lao ni kushika madaraka tu. Chama hiki kibadilike. Kisimamie na kupigania hoja zinazowahusu wananchi moja kwa moja. Mfano kikijaribu kujiweka kuwa mtetezi wa wakulima, kitavuna nguvu nyingi sana. Mtu akisikia kuwa wamekamatwa kwa sababu walikuwa wakipigania unyonyaji wa wakulima wa chai au mahindi inamuingia akikini kukutetea. lakini kwa mtindo huu wa kila siku kupigania namna ya kuingia madarakani kinaweza kufa kabisa.