Vyama vya upinzani anzieni hapa kuelekea kushika dola 2025+

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,603
29,744
Kutokana na uhalisia wa kwamba Chama.Cha Mapinduzi kujikita kwenye siasa zenye malengo ya kuimaliza nchi ishindwe kuwa na uwezo wa kupata maendeleo ya kweli. Nimewaza sasa kutoa ushauri kwa vyama vya siasa hususani vya upinzani kuwapa mbinu za kufikia kutwaa dola kwenye chaguzi zijazo za serikali.

Natoa ushauri huu kama akiba kwani kuna uwezekano mkubwa leo nikaonhea hapa kwa uwazi kama alivyofanya Humphrey Polepole hapa juzi kati baafa ya kuwekwa kando na akili yake ikaanza kumrudia lakini kilichotokea ni kupewa ubalozi ambapo asali imemziba mdomo. Hivyo CCM haina wahuni tena wala viongozi siyo nyatunyatu kama alivyodai.... very shame. Serikali ina mkono mrefu inaweza kumsaka msanii kwa udi wa uvumba kisha ikamnyamazisha kwa njia tatu
  1. Kumtishia aache kuwananga CCM
  2. Kumpa nafasi kwenye sega la taifa
  3. Kumuita ziraili asepe naye
HIvyo najaribu kuwawekea ushauri hapa ambao unaweza kuja kunisuta huko mbeleni endapo nitakuwa sehemu ya kansa.

CCM imejikita kwenye eneo la HADAA yaani uongo wenye ushawishi mwingi. Chama hiki kimehakikisha kuwa wananchi wa Tanzania hususan wanachama wake wengi wanakuwa wajinga ambao wanalishwa uongo mwingi kisha uongo huo wenye vimelea vya hofu unaenea ngazi ya familia hadi kwemye jamii.

CCM ni chama ambacho kilipokuwa no asset kilijikita kwenye siasa za ukombozi na kutetea wanyonge popote pale duniani ambapo kinaelewa mbinu karibia zote zinazotumiwa na wakandamizaji wa haki za binadamu. Viongozi wengi wa CCM ni zao la mfumo (ingawa tunaambiwa askari hawaruhusiwi siasa) hivyo ukifuatilia historia za wengi wesomea Urusi, Cuba, China na nchi ambazo zina ukandamizaji mkubwa wa haki za raia wake.

CCM imejikita kwenye kuhadaa kama nilivyosema awali. Wanaupiga mwingi sana kwenye hilo eneo. Hadaa yenyewe ni kuwa elites wachache wanapeana fursa za hatamu za nchi na wanahakikisha neno UDIKTETA linapigwa vita kwa nguvu zote lakini chama kama chama ni cha KIDIKTETA 100%.

Udikteta wa CCM umejikita kweye mbinu zote chafu tena zinazotishia amani ya nchi kwenye kushika Dola. Kuna muunganiko mkubwa kati ya mihimili yote ya Dola na Chama cha Mapinduzi kwenye kuhakikisha kinaendelea kuwepo madarakani huku kikiwa kimekufa kimeoza.

Kuna haja ya kuhakikisha jeneza la chama hili haliendelei kubebwa na Watanzania daima dumu. Zipo sababu 1001 za kuthibitisha CCM imefilisika kisiasa. Sababu nyingi zimeshasemwa na kuimbwa miaka yote hii na bado kimeendelea kukamata dola kwa kuwaibia wananchi Kura zao na kuwatishia ama kuwashughulikia wale wenye akili wanaojitambua na kuanza kudai UHURU wa kweli wa nchi hii

VYAMA VYA UPINZANI VIANZIE WAPI

1. SERIKALI ZA MITAA
Uchaguzi wa serikali za mitaa ni kipimo kikubwa kinachotumika kwenye kupima namna chama kinavyokubalika. Uchaguzi huo ambao miaka yote unafanyika kwa kiinimacho ni muhimu sana kwa vyama.vya siasa kuhakikisha vinafanya mikakati ya kupata ushindi mwingi. Viongozi wa serikali za Mitaa hukubalika kwenye jamii na kwa namma ambavyo madaraka yao yamejengeka wana ushawishi mkubwa na wanaweza kufanya mikutano ya kiserikali na kisiasa kwenye maeneo yao.

Mwenyekiti wa Mtaa, Kijiji na Kitongoji ndiyo wakuu wa Ulinzi na Usalama maeneo hayo. Hivyo dola inaheshimu mgawanyiko huo na hutumika sana kupin point wananchi ambao wanaonesha dalili za kuiumiza CCM kwenye uchaguzi wa serikali kuu.

Maeneo ambayo vyama vya upinzani vikapata ushindi mwingi wa serikali za mitaa hupelekea kupata washindi kwenye Uchaguzi Mkuu. Hata kura za urais kwa CCM zinapungua eneo hilo

2. NIDHAMU KWA CHAMA
Vyama.vya Upinzani wanapaswa kuweka mstari unaotenganisha majukumu ya chama na majukumu ya wanasiasa walioshinda chaguzi za serikali.

Usimamizi chanya kwenye eneo hili unapelekea kuibuliwa programu za kuwaandaa viongozi wenye weledi, nidhamu na mtazamo wa maendeleo jumuishi.

Vyama vya Upinzani vihakikishe vinatenganisha hizi nafasi ili kuwapa nafasi kila kiongozi kutimiza wajibu wake vizuri. Inapotokea kila anayeshinda uchaguzi wa serikali ndiye anayepewa chapuo kwenye uongozi wa chama hupelekea HADAA ya CCM kwa wananchi kupata dawati la kusikilizwa. Watasema vyama hivyo vina tamaa ya madaraka (ilhali CCM kina ulafi wa madaraka) na kina undugunaizesheni hivyo cha kibaguzi.

Viongozi wa vyama wajikite kukinadi chama, kuandaa ilani na kuzisimamia ilani zao kwenye maeneo waliyoshinda na kupokea taarifa za utendaji wa viongozi wao waliopo serikalini.

3. MAHUSIANO NA VYOMBO VYA DOLA
Ikumbukwe imesemwa sana hapa JF kuhusu ndoa isiyo ya kawaida kati ya vyombo vya usalama na CCM. Wengine walienda mbali zaidi kusema kuwa waajiriwa wote wa UT wana viapo vya siri vya kuitumikia TANU na ASP ambazo sasa ni CCM. Inawezekana kauli hizi zina ukweli kiasi fulani kwa sababu tunashuhudia UTII usio na afya kwa Taifa wa vyombo vyetu vya usalama kwa CCM.

Katiba ya Nchi imetenganisha askari na siasa lakini kwa sababu CCM ni nyakanga wa HADAA kinaishi kwa kutegemea mahusiano hayo.

Tukumbuke zile sauti ambazo zilisambaa mitandaoni za akina Nape, Kinana, Makamba na wemgineo zilipatikana kutokana na udukuzi uliofanywa na vyombo vyetu vya dola na wakazivujisha kwa umma ili kuhakikisha CCM inanufaika na umaluni huo. Chama cha siasa hawana access ya kuingilia mawasiliano ya watu bila usaidizi wa vyombo vya usalama wa nchi.

Hivyo vyama vya upinzani wakiona hakuna dalili ya kupata katiba mpya kabla ya Uchaguzi vijitahidi kupata kuungwa mkono na wananchi na vyombo vya dola. Haiyumkiniki wanao wanachama ambao pia wametokana na vyombo vya dola hivyo wakiwatumia hao wanaweza kuwa na mkakati wenye afya kwa Taifa

4. SERA ZA VYAMA
  1. Sera na Ilani vinapaswa kulenga kuwakomboa wananchi.
  2. Sera za vyama zijibu changamoto sugu zinazowakabili wananchi
  3. Vyama viweke tahadhari na mtazamo wa kijamii kwenye maoni yao kwa katiba na sheria mbalimbali zinazotungwa, vyama visikwame kwenye ibara ya 18 ya Katiba bali viwe na kurunzi la kumulika kila taabu na vijinasaba vya taabu vinavyowapa chanagamoto kwenye katiba na sheria..
  4. Theory of HITMAN isidhaniwe inatumiwa na mataifa yenye nguvu kouchumi dhidi ya madogo pekee. CCM imeadopt mbinu hii hivyo imepandikiza makada wake watiifu ndani ya vyama vya upinzani ili kuhakikisha wanavunja, kuharibu na kuua fikra zozote zenye maslahi ya kitaifa ambayo yanatishia UDIKTETA wake. Mfano wa kinachoendelea NCCR Mageuzi ni mwendelezo wa kuhakikisha vyama havitulii wala kujipanga kuingia kwenye chaguzi kwa utulivu.
  5. Demokrasia ya ndani ya vyama. Well hili kila mmoja anaelewa nini anapaswa kufanya ili kuonesha mfano wa nmna watakavyoishi kwenye dola endapo watapewa usukani wa nchi kupitia sanduku la kura endapo haki itatendeka.
  6. Vyama vifanye tathmini ya mara kwa mara kwenye kukubalika na kuelewea kwa wapigakura. CCM pamoja na kuwa ni nusu-kaputi wamejikita sana kwenye kutathmini kukubalika na kueleweka kwa chama na viongozi kwa wananchi. Tathmini hizi husaidia vikao vya maamuzi kwenye teuzi za kugombea nafasi za dola.
  7. Elimu ya Siasa. Vyama vya upinzani vianzishe darasa la kimkakati kila wilaya la kuwapika viongozi wake kisiasa na uelewa wa uendeshaji wa serikali. Viongozi wa CCM wanapitia semina mbalimbali za kujengwa na kupewa mikakati ya kuendelea kukamata dola. Mafunzo hayo hutolewa hata na watumishi wa umma (matumizi mabaya ya madaraka)
  8. Espionage kwa viongozi hususan mienendo yao kama inahatarisha dira ya Chama kwa maslahi ya umma. Hii pia isaidie kufanya maamuzi thabiti yenye tija kama CHADEMA kilivyofanya kwa wanachama wake 19 wa BAWACHA. Comcept kuu ni kulinda maslahi ya umma ambayo chama kinasimamia kwa mwelekeo waliojiwekea. Uwajibikaji uwe ni utamaduni utakaimarisha vyama hata kama wakiiga drama za CCM
  9. Vyama vipeleke mashushu wake CCM na kuwapenyeza ngazi za uongozi ili kwenda kuidhoofishana kufanikisha kuitoa madarakani kwa maslahi ya Tanzania. Mbinu ya TROJAN HORSE itumike kwa sababu vita vya kisiasa baina ya vyama na vyama imeasisiwa na CCM sasa ni wakati wa kuipelekea moto nayo pia.
  10. Vyama vya upinzani waimarishe misingi yao mashinani ambapo ndipo wapigakura walipo. Watumie ushawishi, weledi, hekima na busara kufanya shughuli zao huko chini. Hakina hilo litawaalika wenye misuli ya fikra ndani ya mfumo uliomilikiwa na CCM kuanza kuvijenga vyama hivyo kuanzia chini hadi juu.
  11. Vyama visiokoteze viongozi wanaotemwa kwenye michakato ya CCM kwa sababu inawezekana kabisa wametemwa kupitia drama ya kwenda kudhoofisha upinzani na hatimaye watarudi walipotokea kupeleka mrejesho na kadhalika
MBinu hizi na mikakati inawezekana kunyambuliwa, kukosolewa au hata kuongezea nyama na walio na nia njema ya nchi hii.

Nimevuka mstari wa mahaba kwa CCM. Ni bora mgonjwa akaondolewa mashine za kupumulia akalala kwa amani kwa sababu kuendelea kumhudumia hakutomfufua

20220310_083203.jpg

Picha haihusiani na mada​
 
💯 💯 💯💯💯💯💯💯💯💯 hakika umenena sisi tupo hatuchoki mpaka ukombozi wa pili
 
Chama chetu ccm ndio kitaamua chama kipi kishike DOLA pale kitapoona kimekosa mvuto!!

Kitajitengenezea upinzani wake na KUUPA DOLA na sio vinginevyo!!

Hivi karibuni kutokana na timu kuwa nyingi hilo linaweza KUTOKEA!!
 
💯 💯 💯💯💯💯💯💯💯💯 hakika umenena sisi tupo hatuchoki mpaka ukombozi wa pili
Chaguzi za Serikali za Mitaa ambazo zina utata mwingi na umuhimu mkubwa sana kwa maendeleo ya nchi zinasimamiwa na kuamuliwa na Wizara ambayo kimsingi inaweza kuamua lolote kwa maslahi ya CCM

Katiba ya Tanzania ifikie mahala iunde Wizara na kuzitaja bayana ili kuondokana na kudura ya Taasisi moja kupanga na kupangua Wizara bila idhini ya wenye nchi.

Kuna mengi muhimu ambayo Upinzani wakipambania wanapata imani ya wapiga kura kwa wingi sana
 
Chama chetu ccm ndio kitaamua chama kipi kishike DOLA pale kitapoona kimekosa mvuto!!

Kitajitengenezea upinzani wake na KUUPA DOLA na sio vinginevyo!!

Hivi karibuni kutokana na timu kuwa nyingi hilo linaweza KUTOKEA!!
Na hili likiruhusiwa ndipo anguko baya sana kwa Watanzania.

Watanzania wapewe uhuru wa kujiamulia na kuvhagua. Waunde vyama na siyo kuundiwa vyama.
 
Kuiua CCM bila kubadili KATIBA iliyopo na kuandika mpya, Nchi itaingia ktk machafuko.

Sababu kuu ni kuwa, mifumo yote imejengwa ikijishikiza ktk chama Dola.

KATIBA mpya itokanayo na Rasimu alosimamia Judge WARIOBA ndo njia pekee ya KUIUA CCM na Bado Nchi ikabaki salama.

CDM shikilieni AGENDA ya Katiba mpya, Tutaona NURU tena ktk TANZANIA.

Ameeen.
 
Kuiua CCM bila kubadili KATIBA iliyopo na kuandika mpya, Nchi itaingia ktk machafuko.

Sababu kuu ni kuwa, mifumo yote imejengwa ikijishikiza ktk chama Dola.

KATIBA mpya itokanayo na Rasimu alosimamia Judge WARIOBA ndo njia pekee ya KUIUA CCM na Bado Nchi ikabaki salama.

CDM shikilieni AGENDA ya Katiba mpya, Tutaona NURU tena ktk TANZANIA.

Ameeen.
Ni wazo na pendekezo sahihi sana
 
Chaguzi za Serikali za Mitaa ambazo zina utata mwingi na umuhimu mkubwa sana kwa maendeleo ya nchi zinasimamiwa na kuamuliwa na Wizara ambayo kimsingi inaweza kuamua lolote kwa maslahi ya CCM

Katiba ya Tanzania ifikie mahala iunde Wizara na kuzitaja bayana ili kuondokana na kudura ya Taasisi moja kupanga na kupangua Wizara bila idhini ya wenye nchi.

Kuna mengi muhimu ambayo Upinzani wakipambania wanapata imani ya wapiga kura kwa wingi sana
Tuko macho sana kama kuibiwa tushaibiwa tumejifunza hatuwezi ludia makosa Tena amini haitatokea kamwe
 
Tuko macho sana kama kuibiwa tushaibiwa tumejifunza hatuwezi ludia makosa Tena amini haitatokea kamwe
Nakubaliana nawe mkuu
Lakini kumbuka vifo vingi vya wanasiasa waliojitoa mhanga kwa umma vilitekelezwa na pamoja na kuinyooshea kidole CCM na serikali hakuna lolote wala chochote cha kuwafanga

Leo Tundu Lisu anaishi uhamishoni kutokana na mahaba yake kwa watanzania kumsababishia kubeba rundo la risasi mwilini
 
Tulitawaliwa na jambazi (Magufuli) bila kujua alikua jambazi sema MUNGU ni mwema sana akatuondolea mapema kabisa kwahio kua na imani turikotoka ni mbali sana Kwa Sasa kunapambazuka Ashukuliwe sana MUNGU
 
Tulitawaliwa na jambazi (Magufuli) bila kujua alikua jambazi sema MUNGU ni mwema sana akatuondolea mapema kabisa kwahio kua na imani turikotoka ni mbali sana Kwa Sasa kunapambazuka Ashukuliwe sana MUNGU
Siasa ni mahessbu
Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa ni mbobezi kwenye sayansi ya siasa.

Amini ninachokuambia mkuu. Hizi imani kuwa YATOSHA sasa zisikupe tumaini kuwa mchezo umekwisha.

Ninaifananisha njia ya siasa kama njia ya waamini ambao wanajiaminisha kuwa shetani ni mjingamjinga kama wanavyodhani. Kuwa makini sana na being ambayo imeishi kwenye mafanikio kisha ikaboronga.

Shetani anataka kuimiliki Mbingu hata leo ndo maana hachoki usiku na mchana.

Natumaini nimesomeka
 
Siasa ni mahessbu
Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa ni mbobezi kwenye sayansi ya siasa.

Amini ninachokuambia mkuu. Hizi imani kuwa YATOSHA sasa zisikupe tumaini kuwa mchezo umekwisha.

Ninaifananisha njia ya siasa kama njia ya waamini ambao wanajiaminisha kuwa shetani ni mjingamjinga kama wanavyodhani. Kuwa makini sana na being ambayo imeishi kwenye mafanikio kisha ikaboronga.

Shetani anataka kuimiliki Mbingu hata leo ndo maana hachoki usiku na mchana.

Natumaini nimesomeka
Tunawajua tunaishi nao tutawakabili mpaka kieleweke hatulegezi mpaka wakae pembeni
 
Kutokana na uhalisia wa kwamba Chama.Cha Mapinduzi kujikita kwenye siasa zenye malengo ya kuimaliza nchi ishindwe kuwa na uwezo wa kupata maendeleo ya kweli. Nimewaza sasa kutoa ushauri kwa vyama vya siasa hususani vya upinzani kuwapa mbinu za kufikia kutwaa dola kwenye chaguzi zijazo za serikali.

Natoa ushauri huu kama akiba kwani kuna uwezekano mkubwa leo nikaonhea hapa kwa uwazi kama alivyofanya Humphrey Polepole hapa juzi kati baafa ya kuwekwa kando na akili yake ikaanza kumrudia lakini kilichotokea ni kupewa ubalozi ambapo asali imemziba mdomo. Hivyo CCM haina wahuni tena wala viongozi siyo nyatunyatu kama alivyodai.... very shame. Serikali ina mkono mrefu inaweza kumsaka msanii kwa udi wa uvumba kisha ikamnyamazisha kwa njia tatu
  1. Kumtishia aache kuwananga CCM
  2. Kumpa nafasi kwenye sega la taifa
  3. Kumuita ziraili asepe naye
HIvyo najaribu kuwawekea ushauri hapa ambao unaweza kuja kunisuta huko mbeleni endapo nitakuwa sehemu ya kansa.

CCM imejikita kwenye eneo la HADAA yaani uongo wenye ushawishi mwingi. Chama hiki kimehakikisha kuwa wananchi wa Tanzania hususan wanachama wake wengi wanakuwa wajinga ambao wanalishwa uongo mwingi kisha uongo huo wenye vimelea vya hofu unaenea ngazi ya familia hadi kwemye jamii.

CCM ni chama ambacho kilipokuwa no asset kilijikita kwenye siasa za ukombozi na kutetea wanyonge popote pale duniani ambapo kinaelewa mbinu karibia zote zinazotumiwa na wakandamizaji wa haki za binadamu. Viongozi wengi wa CCM ni zao la mfumo (ingawa tunaambiwa askari hawaruhusiwi siasa) hivyo ukifuatilia historia za wengi wesomea Urusi, Cuba, China na nchi ambazo zina ukandamizaji mkubwa wa haki za raia wake.

CCM imejikita kwenye kuhadaa kama nilivyosema awali. Wanaupiga mwingi sana kwenye hilo eneo. Hadaa yenyewe ni kuwa elites wachache wanapeana fursa za hatamu za nchi na wanahakikisha neno UDIKTETA linapigwa vita kwa nguvu zote lakini chama kama chama ni cha KIDIKTETA 100%.

Udikteta wa CCM umejikita kweye mbinu zote chafu tena zinazotishia amani ya nchi kwenye kushika Dola. Kuna muunganiko mkubwa kati ya mihimili yote ya Dola na Chama cha Mapinduzi kwenye kuhakikisha kinaendelea kuwepo madarakani huku kikiwa kimekufa kimeoza.

Kuna haja ya kuhakikisha jeneza la chama hili haliendelei kubebwa na Watanzania daima dumu. Zipo sababu 1001 za kuthibitisha CCM imefilisika kisiasa. Sababu nyingi zimeshasemwa na kuimbwa miaka yote hii na bado kimeendelea kukamata dola kwa kuwaibia wananchi Kura zao na kuwatishia ama kuwashughulikia wale wenye akili wanaojitambua na kuanza kudai UHURU wa kweli wa nchi hii

VYAMA VYA UPINZANI VIANZIE WAPI

1. SERIKALI ZA MITAA
Uchaguzi wa serikali za mitaa ni kipimo kikubwa kinachotumika kwenye kupima namna chama kinavyokubalika. Uchaguzi huo ambao miaka yote unafanyika kwa kiinimacho ni muhimu sana kwa vyama.vya siasa kuhakikisha vinafanya mikakati ya kupata ushindi mwingi. Viongozi wa serikali za Mitaa hukubalika kwenye jamii na kwa namma ambavyo madaraka yao yamejengeka wana ushawishi mkubwa na wanaweza kufanya mikutano ya kiserikali na kisiasa kwenye maeneo yao.

Mwenyekiti wa Mtaa, Kijiji na Kitongoji ndiyo wakuu wa Ulinzi na Usalama maeneo hayo. Hivyo dola inaheshimu mgawanyiko huo na hutumika sana kupin point wananchi ambao wanaonesha dalili za kuiumiza CCM kwenye uchaguzi wa serikali kuu.

Maeneo ambayo vyama vya upinzani vikapata ushindi mwingi wa serikali za mitaa hupelekea kupata washindi kwenye Uchaguzi Mkuu. Hata kura za urais kwa CCM zinapungua eneo hilo

2. NIDHAMU KWA CHAMA
Vyama.vya Upinzani wanapaswa kuweka mstari unaotenganisha majukumu ya chama na majukumu ya wanasiasa walioshinda chaguzi za serikali.

Usimamizi chanya kwenye eneo hili unapelekea kuibuliwa programu za kuwaandaa viongozi wenye weledi, nidhamu na mtazamo wa maendeleo jumuishi.

Vyama vya Upinzani vihakikishe vinatenganisha hizi nafasi ili kuwapa nafasi kila kiongozi kutimiza wajibu wake vizuri. Inapotokea kila anayeshinda uchaguzi wa serikali ndiye anayepewa chapuo kwenye uongozi wa chama hupelekea HADAA ya CCM kwa wananchi kupata dawati la kusikilizwa. Watasema vyama hivyo vina tamaa ya madaraka (ilhali CCM kina ulafi wa madaraka) na kina undugunaizesheni hivyo cha kibaguzi.

Viongozi wa vyama wajikite kukinadi chama, kuandaa ilani na kuzisimamia ilani zao kwenye maeneo waliyoshinda na kupokea taarifa za utendaji wa viongozi wao waliopo serikalini.

3. MAHUSIANO NA VYOMBO VYA DOLA
Ikumbukwe imesemwa sana hapa JF kuhusu ndoa isiyo ya kawaida kati ya vyombo vya usalama na CCM. Wengine walienda mbali zaidi kusema kuwa waajiriwa wote wa UT wana viapo vya siri vya kuitumikia TANU na ASP ambazo sasa ni CCM. Inawezekana kauli hizi zina ukweli kiasi fulani kwa sababu tunashuhudia UTII usio na afya kwa Taifa wa vyombo vyetu vya usalama kwa CCM.

Katiba ya Nchi imetenganisha askari na siasa lakini kwa sababu CCM ni nyakanga wa HADAA kinaishi kwa kutegemea mahusiano hayo.

Tukumbuke zile sauti ambazo zilisambaa mitandaoni za akina Nape, Kinana, Makamba na wemgineo zilipatikana kutokana na udukuzi uliofanywa na vyombo vyetu vya dola na wakazivujisha kwa umma ili kuhakikisha CCM inanufaika na umaluni huo. Chama cha siasa hawana access ya kuingilia mawasiliano ya watu bila usaidizi wa vyombo vya usalama wa nchi.

Hivyo vyama vya upinzani wakiona hakuna dalili ya kupata katiba mpya kabla ya Uchaguzi vijitahidi kupata kuungwa mkono na wananchi na vyombo vya dola. Haiyumkiniki wanao wanachama ambao pia wametokana na vyombo vya dola hivyo wakiwatumia hao wanaweza kuwa na mkakati wenye afya kwa Taifa

4. SERA ZA VYAMA
  1. Sera na Ilani vinapaswa kulenga kuwakomboa wananchi.
  2. Sera za vyama zijibu changamoto sugu zinazowakabili wananchi
  3. Vyama viweke tahadhari na mtazamo wa kijamii kwenye maoni yao kwa katiba na sheria mbalimbali zinazotungwa, vyama visikwame kwenye ibara ya 18 ya Katiba bali viwe na kurunzi la kumulika kila taabu na vijinasaba vya taabu vinavyowapa chanagamoto kwenye katiba na sheria..
  4. Theory of HITMAN isidhaniwe inatumiwa na mataifa yenye nguvu kouchumi dhidi ya madogo pekee. CCM imeadopt mbinu hii hivyo imepandikiza makada wake watiifu ndani ya vyama vya upinzani ili kuhakikisha wanavunja, kuharibu na kuua fikra zozote zenye maslahi ya kitaifa ambayo yanatishia UDIKTETA wake. Mfano wa kinachoendelea NCCR Mageuzi ni mwendelezo wa kuhakikisha vyama havitulii wala kujipanga kuingia kwenye chaguzi kwa utulivu.
  5. Demokrasia ya ndani ya vyama. Well hili kila mmoja anaelewa nini anapaswa kufanya ili kuonesha mfano wa nmna watakavyoishi kwenye dola endapo watapewa usukani wa nchi kupitia sanduku la kura endapo haki itatendeka.
  6. Vyama vifanye tathmini ya mara kwa mara kwenye kukubalika na kuelewea kwa wapigakura. CCM pamoja na kuwa ni nusu-kaputi wamejikita sana kwenye kutathmini kukubalika na kueleweka kwa chama na viongozi kwa wananchi. Tathmini hizi husaidia vikao vya maamuzi kwenye teuzi za kugombea nafasi za dola.
  7. Elimu ya Siasa. Vyama vya upinzani vianzishe darasa la kimkakati kila wilaya la kuwapika viongozi wake kisiasa na uelewa wa uendeshaji wa serikali. Viongozi wa CCM wanapitia semina mbalimbali za kujengwa na kupewa mikakati ya kuendelea kukamata dola. Mafunzo hayo hutolewa hata na watumishi wa umma (matumizi mabaya ya madaraka)
  8. Espionage kwa viongozi hususan mienendo yao kama inahatarisha dira ya Chama kwa maslahi ya umma. Hii pia isaidie kufanya maamuzi thabiti yenye tija kama CHADEMA kilivyofanya kwa wanachama wake 19 wa BAWACHA. Comcept kuu ni kulinda maslahi ya umma ambayo chama kinasimamia kwa mwelekeo waliojiwekea. Uwajibikaji uwe ni utamaduni utakaimarisha vyama hata kama wakiiga drama za CCM
  9. Vyama vipeleke mashushu wake CCM na kuwapenyeza ngazi za uongozi ili kwenda kuidhoofishana kufanikisha kuitoa madarakani kwa maslahi ya Tanzania. Mbinu ya TROJAN HORSE itumike kwa sababu vita vya kisiasa baina ya vyama na vyama imeasisiwa na CCM sasa ni wakati wa kuipelekea moto nayo pia.
  10. Vyama vya upinzani waimarishe misingi yao mashinani ambapo ndipo wapigakura walipo. Watumie ushawishi, weledi, hekima na busara kufanya shughuli zao huko chini. Hakina hilo litawaalika wenye misuli ya fikra ndani ya mfumo uliomilikiwa na CCM kuanza kuvijenga vyama hivyo kuanzia chini hadi juu.
  11. Vyama visiokoteze viongozi wanaotemwa kwenye michakato ya CCM kwa sababu inawezekana kabisa wametemwa kupitia drama ya kwenda kudhoofisha upinzani na hatimaye watarudi walipotokea kupeleka mrejesho na kadhalika
MBinu hizi na mikakati inawezekana kunyambuliwa, kukosolewa au hata kuongezea nyama na walio na nia njema ya nchi hii.

Nimevuka mstari wa mahaba kwa CCM. Ni bora mgonjwa akaondolewa mashine za kupumulia akalala kwa amani kwa sababu kuendelea kumhudumia hakutomfufua

View attachment 2417134
Picha haihusiani na mada​
Nchi zote wananchi ndio wanaleta mageuzi kichekesho Tanzania tunawasukumia wachache.
 
Nchi zote wananchi ndio wanaleta mageuzi kichekesho Tanzania tunawasukumia wachache.
Ni nchi gani duniani ambayo watu wake wametepeteshwa kama Tanzania.

Mfano mzuri ni huu. Tunabidi kutumia pen names kutoa maoni. Wakikujua wanakunyonya damu unakauka
 
Chama chetu ccm ndio kitaamua chama kipi kishike DOLA pale kitapoona kimekosa mvuto!!

Kitajitengenezea upinzani wake na KUUPA DOLA na sio vinginevyo!!

Hivi karibuni kutokana na timu kuwa nyingi hilo linaweza KUTOKEA!!
Hatuna Chama Cha Mapinduzi bali tuna DOLA inayojiita Chama cha Mapinduzi - yaani kifupi tunatawaliwa kijeshi na ndiyo maana shughuli za kisiasa zote hazipo kwa sasa.
 
CCM uchaguzi UKIFANYIKA hachomoki, hata wachukue kamkaze drone , Himars, spider n.k WENDA yakawa yanawalipukia wao tu wanao yaendesha,

No way out ccm itakua Madarakani tena , naliongea kila siku na confidence ya Hali ya juu Sana maana najua Bwana hajawai sema kitu na kuniabisha,

Niombacho wapewe Moyo kwepesi kuyakubali yajayo vinginevyo wakilazimisha Kama ilivyo mazoea yao , hasira ya Bwana itakua ya kishindo kikuu juu yao na familia zao, WENDA wakalazimika toa machozi ya kujaza pipa ila nayo hawatayapata,

Nyakati huja na kupita, na hakuna binadam yeyote wa kuzuia nyakati flani zikifika ziwe za furaha,/ uzuni n.k ndo maana hata wakati wa kifo Cha binadam ukifika zitakuepo sababu nyingi tu Ili litimie, so bila kujali wewe nani, maskin/ tajiri / umekua unasali vipi so far ni wakati umefika utakufa tu, hili la wakati/ nyakati, binadamu huwa tunajiona wajanja kwamba tunaweza WEKA u- turn ,hakuna Cha u -turn hapa,

Mfano wakati wa SSH kuwa Rais ulikuepo ila ulikua haujafika na hulipofika mnaona Sasa ni Rais haijalishi kulikua na vikwazo vingapi , kutoka KWa binadam lakini wakati umefika unashangaa mnakodeleana macho hamjui hata Cha kufanya,

Hivyo wakati wa ccm kuongoza taifa Kama chama Cha siasa haupo tena na hakuna binadam yoyote , narudia yoyote wa kulizuia Hili, Twendee tu si tupo
 
Kutokana na uhalisia wa kwamba Chama.Cha Mapinduzi kujikita kwenye siasa zenye malengo ya kuimaliza nchi ishindwe kuwa na uwezo wa kupata maendeleo ya kweli. Nimewaza sasa kutoa ushauri kwa vyama vya siasa hususani vya upinzani kuwapa mbinu za kufikia kutwaa dola kwenye chaguzi zijazo za serikali.

Natoa ushauri huu kama akiba kwani kuna uwezekano mkubwa leo nikaonhea hapa kwa uwazi kama alivyofanya Humphrey Polepole hapa juzi kati baafa ya kuwekwa kando na akili yake ikaanza kumrudia lakini kilichotokea ni kupewa ubalozi ambapo asali imemziba mdomo. Hivyo CCM haina wahuni tena wala viongozi siyo nyatunyatu kama alivyodai.... very shame. Serikali ina mkono mrefu inaweza kumsaka msanii kwa udi wa uvumba kisha ikamnyamazisha kwa njia tatu
  1. Kumtishia aache kuwananga CCM
  2. Kumpa nafasi kwenye sega la taifa
  3. Kumuita ziraili asepe naye
HIvyo najaribu kuwawekea ushauri hapa ambao unaweza kuja kunisuta huko mbeleni endapo nitakuwa sehemu ya kansa.

CCM imejikita kwenye eneo la HADAA yaani uongo wenye ushawishi mwingi. Chama hiki kimehakikisha kuwa wananchi wa Tanzania hususan wanachama wake wengi wanakuwa wajinga ambao wanalishwa uongo mwingi kisha uongo huo wenye vimelea vya hofu unaenea ngazi ya familia hadi kwemye jamii.

CCM ni chama ambacho kilipokuwa no asset kilijikita kwenye siasa za ukombozi na kutetea wanyonge popote pale duniani ambapo kinaelewa mbinu karibia zote zinazotumiwa na wakandamizaji wa haki za binadamu. Viongozi wengi wa CCM ni zao la mfumo (ingawa tunaambiwa askari hawaruhusiwi siasa) hivyo ukifuatilia historia za wengi wesomea Urusi, Cuba, China na nchi ambazo zina ukandamizaji mkubwa wa haki za raia wake.

CCM imejikita kwenye kuhadaa kama nilivyosema awali. Wanaupiga mwingi sana kwenye hilo eneo. Hadaa yenyewe ni kuwa elites wachache wanapeana fursa za hatamu za nchi na wanahakikisha neno UDIKTETA linapigwa vita kwa nguvu zote lakini chama kama chama ni cha KIDIKTETA 100%.

Udikteta wa CCM umejikita kweye mbinu zote chafu tena zinazotishia amani ya nchi kwenye kushika Dola. Kuna muunganiko mkubwa kati ya mihimili yote ya Dola na Chama cha Mapinduzi kwenye kuhakikisha kinaendelea kuwepo madarakani huku kikiwa kimekufa kimeoza.

Kuna haja ya kuhakikisha jeneza la chama hili haliendelei kubebwa na Watanzania daima dumu. Zipo sababu 1001 za kuthibitisha CCM imefilisika kisiasa. Sababu nyingi zimeshasemwa na kuimbwa miaka yote hii na bado kimeendelea kukamata dola kwa kuwaibia wananchi Kura zao na kuwatishia ama kuwashughulikia wale wenye akili wanaojitambua na kuanza kudai UHURU wa kweli wa nchi hii

VYAMA VYA UPINZANI VIANZIE WAPI

1. SERIKALI ZA MITAA
Uchaguzi wa serikali za mitaa ni kipimo kikubwa kinachotumika kwenye kupima namna chama kinavyokubalika. Uchaguzi huo ambao miaka yote unafanyika kwa kiinimacho ni muhimu sana kwa vyama.vya siasa kuhakikisha vinafanya mikakati ya kupata ushindi mwingi. Viongozi wa serikali za Mitaa hukubalika kwenye jamii na kwa namma ambavyo madaraka yao yamejengeka wana ushawishi mkubwa na wanaweza kufanya mikutano ya kiserikali na kisiasa kwenye maeneo yao.

Mwenyekiti wa Mtaa, Kijiji na Kitongoji ndiyo wakuu wa Ulinzi na Usalama maeneo hayo. Hivyo dola inaheshimu mgawanyiko huo na hutumika sana kupin point wananchi ambao wanaonesha dalili za kuiumiza CCM kwenye uchaguzi wa serikali kuu.

Maeneo ambayo vyama vya upinzani vikapata ushindi mwingi wa serikali za mitaa hupelekea kupata washindi kwenye Uchaguzi Mkuu. Hata kura za urais kwa CCM zinapungua eneo hilo

2. NIDHAMU KWA CHAMA
Vyama.vya Upinzani wanapaswa kuweka mstari unaotenganisha majukumu ya chama na majukumu ya wanasiasa walioshinda chaguzi za serikali.

Usimamizi chanya kwenye eneo hili unapelekea kuibuliwa programu za kuwaandaa viongozi wenye weledi, nidhamu na mtazamo wa maendeleo jumuishi.

Vyama vya Upinzani vihakikishe vinatenganisha hizi nafasi ili kuwapa nafasi kila kiongozi kutimiza wajibu wake vizuri. Inapotokea kila anayeshinda uchaguzi wa serikali ndiye anayepewa chapuo kwenye uongozi wa chama hupelekea HADAA ya CCM kwa wananchi kupata dawati la kusikilizwa. Watasema vyama hivyo vina tamaa ya madaraka (ilhali CCM kina ulafi wa madaraka) na kina undugunaizesheni hivyo cha kibaguzi.

Viongozi wa vyama wajikite kukinadi chama, kuandaa ilani na kuzisimamia ilani zao kwenye maeneo waliyoshinda na kupokea taarifa za utendaji wa viongozi wao waliopo serikalini.

3. MAHUSIANO NA VYOMBO VYA DOLA
Ikumbukwe imesemwa sana hapa JF kuhusu ndoa isiyo ya kawaida kati ya vyombo vya usalama na CCM. Wengine walienda mbali zaidi kusema kuwa waajiriwa wote wa UT wana viapo vya siri vya kuitumikia TANU na ASP ambazo sasa ni CCM. Inawezekana kauli hizi zina ukweli kiasi fulani kwa sababu tunashuhudia UTII usio na afya kwa Taifa wa vyombo vyetu vya usalama kwa CCM.

Katiba ya Nchi imetenganisha askari na siasa lakini kwa sababu CCM ni nyakanga wa HADAA kinaishi kwa kutegemea mahusiano hayo.

Tukumbuke zile sauti ambazo zilisambaa mitandaoni za akina Nape, Kinana, Makamba na wemgineo zilipatikana kutokana na udukuzi uliofanywa na vyombo vyetu vya dola na wakazivujisha kwa umma ili kuhakikisha CCM inanufaika na umaluni huo. Chama cha siasa hawana access ya kuingilia mawasiliano ya watu bila usaidizi wa vyombo vya usalama wa nchi.

Hivyo vyama vya upinzani wakiona hakuna dalili ya kupata katiba mpya kabla ya Uchaguzi vijitahidi kupata kuungwa mkono na wananchi na vyombo vya dola. Haiyumkiniki wanao wanachama ambao pia wametokana na vyombo vya dola hivyo wakiwatumia hao wanaweza kuwa na mkakati wenye afya kwa Taifa

4. SERA ZA VYAMA
  1. Sera na Ilani vinapaswa kulenga kuwakomboa wananchi.
  2. Sera za vyama zijibu changamoto sugu zinazowakabili wananchi
  3. Vyama viweke tahadhari na mtazamo wa kijamii kwenye maoni yao kwa katiba na sheria mbalimbali zinazotungwa, vyama visikwame kwenye ibara ya 18 ya Katiba bali viwe na kurunzi la kumulika kila taabu na vijinasaba vya taabu vinavyowapa chanagamoto kwenye katiba na sheria..
  4. Theory of HITMAN isidhaniwe inatumiwa na mataifa yenye nguvu kouchumi dhidi ya madogo pekee. CCM imeadopt mbinu hii hivyo imepandikiza makada wake watiifu ndani ya vyama vya upinzani ili kuhakikisha wanavunja, kuharibu na kuua fikra zozote zenye maslahi ya kitaifa ambayo yanatishia UDIKTETA wake. Mfano wa kinachoendelea NCCR Mageuzi ni mwendelezo wa kuhakikisha vyama havitulii wala kujipanga kuingia kwenye chaguzi kwa utulivu.
  5. Demokrasia ya ndani ya vyama. Well hili kila mmoja anaelewa nini anapaswa kufanya ili kuonesha mfano wa nmna watakavyoishi kwenye dola endapo watapewa usukani wa nchi kupitia sanduku la kura endapo haki itatendeka.
  6. Vyama vifanye tathmini ya mara kwa mara kwenye kukubalika na kuelewea kwa wapigakura. CCM pamoja na kuwa ni nusu-kaputi wamejikita sana kwenye kutathmini kukubalika na kueleweka kwa chama na viongozi kwa wananchi. Tathmini hizi husaidia vikao vya maamuzi kwenye teuzi za kugombea nafasi za dola.
  7. Elimu ya Siasa. Vyama vya upinzani vianzishe darasa la kimkakati kila wilaya la kuwapika viongozi wake kisiasa na uelewa wa uendeshaji wa serikali. Viongozi wa CCM wanapitia semina mbalimbali za kujengwa na kupewa mikakati ya kuendelea kukamata dola. Mafunzo hayo hutolewa hata na watumishi wa umma (matumizi mabaya ya madaraka)
  8. Espionage kwa viongozi hususan mienendo yao kama inahatarisha dira ya Chama kwa maslahi ya umma. Hii pia isaidie kufanya maamuzi thabiti yenye tija kama CHADEMA kilivyofanya kwa wanachama wake 19 wa BAWACHA. Comcept kuu ni kulinda maslahi ya umma ambayo chama kinasimamia kwa mwelekeo waliojiwekea. Uwajibikaji uwe ni utamaduni utakaimarisha vyama hata kama wakiiga drama za CCM
  9. Vyama vipeleke mashushu wake CCM na kuwapenyeza ngazi za uongozi ili kwenda kuidhoofishana kufanikisha kuitoa madarakani kwa maslahi ya Tanzania. Mbinu ya TROJAN HORSE itumike kwa sababu vita vya kisiasa baina ya vyama na vyama imeasisiwa na CCM sasa ni wakati wa kuipelekea moto nayo pia.
  10. Vyama vya upinzani waimarishe misingi yao mashinani ambapo ndipo wapigakura walipo. Watumie ushawishi, weledi, hekima na busara kufanya shughuli zao huko chini. Hakina hilo litawaalika wenye misuli ya fikra ndani ya mfumo uliomilikiwa na CCM kuanza kuvijenga vyama hivyo kuanzia chini hadi juu.
  11. Vyama visiokoteze viongozi wanaotemwa kwenye michakato ya CCM kwa sababu inawezekana kabisa wametemwa kupitia drama ya kwenda kudhoofisha upinzani na hatimaye watarudi walipotokea kupeleka mrejesho na kadhalika
MBinu hizi na mikakati inawezekana kunyambuliwa, kukosolewa au hata kuongezea nyama na walio na nia njema ya nchi hii.

Nimevuka mstari wa mahaba kwa CCM. Ni bora mgonjwa akaondolewa mashine za kupumulia akalala kwa amani kwa sababu kuendelea kumhudumia hakutomfufua

View attachment 2417134
Picha haihusiani na mada​
Hii nondo vipi
 
CCM uchaguzi UKIFANYIKA hachomoki, hata wachukue kamkaze drone , Himars, spider n.k WENDA yakawa yanawalipukia wao tu wanao yaendesha,

No way out ccm itakua Madarakani tena , naliongea kila siku na confidence ya Hali ya juu Sana maana najua Bwana hajawai sema kitu na kuniabisha,
Ukweli mtupu
 
Back
Top Bottom