Kusema lengo kuu la chama cha siasa ni kushika madaraka ni kupotosha

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,204
12,700
Kumekuwa na haka kamsemo ka kizembe kuwa lengo kuu la chama cha siasa ni kushika madaraka. Huu ni upotoshaji. kwanza chama cha siasa ni kitu gani? chama cha siasa ni umoja wa watu wenye mawazo(Sera) zinazofanana juu ya kuendesha nchi. Mwanachama wa chama cha siasa lengo lake kuu ni kuona sera hizo zinafanyiwa kazi.

Mfano, mwanachama wa chama cha CDM anatamani kuona sera ya majimbo ikitekelezwa. Haijalishi CDM wapo madarakani au la. CDM ikishika madaraka na isitekeleze zile sera zilizokubaliwa na wanachama, malengo ya chama cha siasa yanakuwa bado hayajafikiwa.

Kuna njia nyingi za kufanya sera za chama zitekelezwe. Chama kinaweza kisiwe ndani ya madaraka lakini sera zake zikatekelezwa. Mfano ni jinsi sera ya ufisadi ya CDM ilivyofanyiwa kazi(Kwa sehemu kubwa) na serikali ya CCM. Hili la kusema lengo ni kushika madaraka ndiyo maana serikali inakataza siasa baada ya uchaguzi.

Lengo kuu la chama cha siasa ni kuona sera zake zinatekelezwa na si kushika madaraka.
 
Hiyo maana umejifunza wapi? Lazima chama kiwe madarakani ili kiweze kusimamia sera zake vizuri, sio zitekelezwe na mwingine. Ulichoeleza ni sawa na kujipiga ngwara, nyie ndio waiba kura na kutaka kuja kusawazisha ground. Mnatetea mfumo kea kutaka kuvipangia vyama nini vifanye
 
Hakika ujinga wa uzeen lazma utakufa nao tu pole sana
Kumekuwa na haka kamemo ka kizembe kuwa lengo kuu la chama cha siasa ni kushika madaraka. Huu ni upotoshaji. kwanza chama cha siasa ni kitu gani? chama cha siasa ni umoja wa watu wenye mawazo(Sera) zinazofanana juu ya kuendesha nchi. Mwanachama wa chama cha siasa lengo lake kuu ni kuona sera hizo zinafanyiwa kazi.

Mfano, mwanachama wa chama cha CDM anatamani kuona sera ya majimbo ikitekelezwa. Haijalishi CDM wapo madarakani au la. CDM ikishika madaraka na isitekeleze zile sera zilizokubaliwa na wanachama, malengo ya chama cha siasa yanakuwa bado hayajafikiwa.

Kuna njia nyingi za kufanya sera za chama zitekelezwe. Chama kinaweza kisiwe ndani ya madaraka lakini sera zake zikatekelezwa. Mfano ni jinsi sera ya ufisadi ya CDM ilivyofanyiwa kazi(Kwa sehemu kubwa) na serikali ya CCM. Hili la kusema lengo ni kushika madaraka ndiyo maana serikali inakataza siasa baada ya uchaguzi.

Lengo kuu la chama cha siasa ni kuona ser zake zinatekelezwa na si kushika madaraka.
 
Hiyo maana umejifunza wapi? Lazima chama kiwe madarakani ili kiweze kusimamia sera zake vizuri, sio zitekelezwe na mwingine. Ulichoeleza ni sawa na kujipiga ngwara, nyie ndio waiba kura na kutaka kuja kusawazisha ground. Mnatetea mfumo kea kutaka kuvipangia vyama nini vifanye
Hiyo ndiyo maana yake. Nchi ina vyama karibu 18. Kila chama kikipata madaraka kwa miaka mitano, kitasubiri miaka 80 ili kushika tena madaraka. Lengo la chama cha siasa ni kutekeleza sera zake. haijalishi zimetekelezwa namna gani. Furaha ya mwanachama ni kuona sera za chama chake ambazo anaziunga mkono zinatekelezwa.
 
Kwani uongo?

Vyama vyote vya siasa lengo lao na dhumuni ni moja tu ''KUSHIKA NCHI" huo ndio ukweli.

Ingekuwa kutetea wananchi basi kusingekuwa na haja za kupitisha michango ya kichama na kuitumia kujenga majengo ya kiofisi badala yake hiyo michango mungeitumia kusaidia wagonjwa na masikin mitaani.

Hizo ruzuku mngezitumia kuijenga jamii na sio kudumisha hali za vyama vyenu.

Kusubiri chama fulan eti kikuletee maendeleo huo ni uongo by 100%, hakuna chama cha kumtetea mwananchi, hakipo, bali kiongozi makini anaweza kuibuka ndani ya chama kwaajili ya maendeleo ya nchi.

Vyama vyote malengo yao ni kuingia ikulu, ndiomaana kuna kelele za kudai tume huru ya uchaguzi na mabadiriko ya katiba mpya, lengo kuu ni kupata mwanya wa kuingia ikulu.

Acheni kudanganya watu, waambieni ukweli kuwa mnania ya kuingia ikulu ili mpate nafasi za kuwaletea hayo maendeleo mnayohubiri kila siku.

Wanasiasa wote ni WAONGO
 
Back
Top Bottom