CHADEMA na Udikteta Makao Makuu

hapa ni hoja kwa vielelezo hakuna cha majeshi wala nini hapa ni data zinatumika tuu kwani huyu mzee anajua tuu ile propaganda nyeusi sasa atakoma na najua kuwa humu hawezi kuja kama mpo naye muwe mnampelekea japo yaliyojiri humu ili aweze kujua jinsi watu wanavyojua alichopewa ....
 
Nimemkuta huyu mzee leo akiwa Sinza anafanya biashara ya kuuza kalenda kwani jamani huwa hammpi chochote?
 

huyo aliyeandika hii habari ametumia akili yake kureflect yale yanayotokea ndani ya chadema ! Mbaya zaidi mnamuongelea aliyeandika hii habari badala ya habari yenyewe ! ama kweli kichwa cha mbuzi ni kichwa cha mbuzi tu siku zote !
 

Dada Asha, kumtetea Mh. Mbowe kwa kunukuu gazeti lake mwenyewe haimsadii mwenyekiti wenu wala Chadema kama chama. Ni bora ungejenga hoja zako mwenyewe au vinginevyo mwachie Mh. Lunyungu ndie anaweza spinning za aina hii.

huyo asha anatakiwa aangalie context na sio aliyetoa hoja, hadi hivi sasa hajakubali wala kukataa kama ni kweli. huyu lunyungu amezidi nae kupotosha na wakati wake wa kutolewa uvivu upo njiani ! you can quote me on that one !
 
Taifa linazama; Kama kweli mpaka leo 2008; Chama chetu kitakatifu cha Upinzani bado kinahitaji kujisafisha chenyewe; bado ndani hawajiamini kwa kweli Taifa lina safari ndefu sana ya maendeleo!!!

Kwa vyovyote vile hizo hoja zinatoka ndani ya CHADEMA yenyewe... hii ni hatari kwa Taifa letu... lini litakuwa na Upinzani ule aliousifia/alioutabiri Kambarage?

Tutajidanganya kujibizana hapa kishaghala baghala lakini tatizo halijatatuliwa... na kwa kweli rasilimali za CHADEMA hazijaonekana vijijini bado... muda unaenda waheshimiwa wapenda maendeleo
 

Dada Asha, kumtetea Mh. Mbowe kwa kunukuu gazeti lake mwenyewe haimsadii mwenyekiti wenu wala Chadema kama chama. Ni bora ungejenga hoja zako mwenyewe au vinginevyo mwachie Mh. Lunyungu ndie anaweza spinning za aina hii.


Kakalende unapaswa kuniomba msamaha sana kwa kuniita spinner .Ila nakushangaa sana kusema gazeti la mbowe linajibu mapigo kwani Mbowe ndiye kaandika ? Katika historia ya wafanya biashara Tanzania na hasa media Mbowe hata Balile anaweza kumtetea huwa haulizi leo mmeandika nini ili abadilishe yeye kesha achana na haya .Karugendo anakaa Mwanza tena si Mwanza tu anakaa kijijini na akitaka kuandika nan kutuma anakuja Mwanza mjini .Au u nataka kusema anatumiwa kuandika kumsifu Mbowe ? Ama kweli ni mufilisi soon utaishiwa hata uwezo wa kufikiri.
 
Kada Mpinzani,
Hizo content ni zipi haswa?..Huyu mwandishi anasifia sana kuwepo kwa makundi ndani ya chama na haelewi kwa nini CCM wanapinga akieleza mazuri ya uwakilishi wa mbinu tofauti ktk chama ili kufikia malengo yaliyotarajiwa.. Huyu huyu tena anaiponda Chadema inayojitokeza kuwa na makundi ya watu wanaotaofautiana mbinu ndani ya chama akivuta Uadui kati ya viongozi wa ndani. Hoja iliyotangulia kuwa objective kaiweka madongo upande wa pili hali mtu huyu Chacha Wangwe anayezungumziwa anatumikia wadhifa wake kama mwenyekiti msaidizi wa chama ana anatambuliwa na hao watu wa Makao makuu..

Bila kupoteza muda sio lazima chama kizima kiunge mkono mbinu za kiongozi mmoja anapochukua jukumu lake binafsi kutangaza ama kusema maoni yake kama alivyofanya ktk swala la mgogoro wa Kenya..Na ikiwa kuna kiongozi ama viongozi toka maakao makuu wanatofautiana na wale wa mikoani ningependa sana kuelewa kitu kimoja... Makao makuu ni wapi na mikoani ni wapi?..
Pengine haya matatizo yanatokana na ushindani wa madaraka ndani ya chama toka mkoa mmoja au mtu mmoja!..Nina hakika kwamba tatizo kubwa la mwafrioka ni ile TITLE, siku zote tunagombea kiti kwa sababu tunataka kuitwa Mheshimiwa, Mwenyekiti, katibu na kadhalika hali sii lazima uwe ktk nafasi hizo kuweza kupanda ngazi.. Tumewaona kina Obama, Mama Clinton na wengine wote ambao wamefikia hatua za mwisho za kuchaguliwa kuwa marais bila kushika nafasi za juu ndani ya chama.
Mkuu haya ni mawazo finyu sana kukitazama chama na uendeshaji wake wa ndani kama kielelezo cha Taifa zima. Huyu mzee hana tofauti kabisa na wale wazee wa Kariakoo wanaotazama nyumba za jirani wanakula nini? ama kama kwao wamekula sembe la mlenda basi matusi yote yatapelekwa mtaani kuwa ni mateso ya wazazi..Yeye kaleta kitu gani ndani ya chama!.. hakuna zaidi ya majungu..
 



Kasheshe it is only CCM will tae ages kujibu tuhuma za Kichama ama mtu mmoja mmoja kulingana na uozo walio nao .Muda wote CCM hawajibu hoja na sasa wanatumia media kufanya damaging .Spinning yangu iko wapi ?Kama sina data siwezi kuandika that is me .Nikijua na nikapata ushahidi naandika na ndiyo mimi.Siandiki kama Kanda ama wengine kwa kutimiza neno la mkono wa mjinga huandika kokote no .Siandiki kwa kuwa nina access na net no .Naandika nikiwa najua cha kuandika na si kupoteza muda .Mada kibao huwa nikiwa sina cha kusema napita na huwezi kukuta nimeandika kila mada hapana .Ila nyie ambao haya kuweka hoja hamuweki ila ushabiki mnaumia.Leo Chadema wanakuja na nondo mnasema majeshi .What a shame ? Mlitegemea nini ? Kwamba mlete umbeya na uzandik watu wakae kimya ? Endeleeni kupambana na hali halisi .Mzee Chama alifukuzwa , kama Balile yuko kwenye payroll .Kada una akili mbovu kaka .baada ya maelezo yote haya bado unasema wakubali ama wakatae ? Utatia akili mwenyewe rudi usome uelewe .The writer anakuwa attacked ili aje in public domain atetee maandiko yake.Najua anapita hapa kila siku anaweza kusema ama akupe desa uje nalo hapa .Wacha habari za Ukarume kenge hapa .
 

LUNYUNGU, you are now officially crowned as a spinner and a whinner (sp.)!! Good to have you here, now take your crown !
 
LUNYUNGU, you are now officially crowned as a spinner and a whinner (sp.)!! Good to have you here, now take your crown !

Nilidhani umechangia hoja kumbe unaendeleza yale yale ambayo wamekuzoea wengi wetu hapa ? Lini utakuja na hoja bila ushabiki na hoja ya faida ua jamii na Nchi yangu Tanzania ?
 
nusura niijibu hii hoja lakini wakati mwingine mtoto usimcheke mzee wako akikaa uchi; ningeifumua hiyo hoja ya huyo mzee na kuiacha iwe na matundu kama nguo ya kaniki.. but then ningeitwa Chadema!
 
Nilidhani umechangia hoja kumbe unaendeleza yale yale ambayo wamekuzoea wengi wetu hapa ? Lini utakuja na hoja bila ushabiki na hoja ya faida ua jamii na Nchi yangu Tanzania ?

you can take the crown home spinner!
picture me tomorrow and the thread that will be brought by Kada !
 

Mkuu Lun,
Ingawa hii article inaelekea kwenye kumpamba Lungwi, bila kuonyesha mapungufu yake, lakini nafikiri inafunua maswali muhimu ambayo wote, CHADEMA na nonCHADEMA, wanahitaji kujibiwa.
  1. Suala la ruzuku kutofika mikoani ni rahisi sana kwa CHADEMA kuliondolea kelele kwa kuchapisha mahesabu yao. Hii sio tu kuwa itaondoa kusingiziana, bali pia itawatofautisha na vyama vingine, hasa CCM, kwa kuonyesha kuwa sera ya uwazi na ukweli ni CHADMA kiukwelikwli na sio Mkapa.
  2. Ukabila nao ni kati ya mambo mengi yanayowafanya watu wengi hasa wasomi wasijiunge na CHADEMA. Hii iko wazi tokea enzi za mzee Mtei. Kwa mfano, kama 50% ya wabunge wake wote wanatokea Kilimanjaro, mmoja tu akiwa amechaguliwa, karibu 70% ya wa kuteuliwa ni wa Kilimanjaro, 25% ya wanaSecretariati ni wa Kilimajaro. Hii sidhani ni coincedence. Hawa ni kati tu ya wale waliowekwa wazi kwenye www.chadema.net. Sio ajabu kuna zaidi lakini hatuwezi kufahamu. Kwa hiyo ni muhimu kwa WanaCHADEMA wote, na wasio, kuyaongelea haya yote kwa uwazi na CHADEMA kuyatafutia ufumbuzi, bila kuficha, maana ni chama pekee hivi sasa kinachotegemewa siku moja kuchukua nafasi ya CCM.
Kwa hiyo ni kuwa hata kama Freeman au mtu mwingine yeyote atakuwa anachangia kwa kiasi kikubwa chamani kuliko wengine, hapatakuwa na Demokrasia kama atajaza watu wake na chama kukosa sura ya kitaifa.
 

Kwa argument yako hii, naona tunarudi palepale kwenye ile thread nilianzisha hapa kuwa CCM ni chama cha kiislam kwa vile 75% ya viongozi wa juu wa ccm, wajumbe wa CC na NEC ni waslam?

Hii formula yako hapa inaweza kutumiwa vyovyote vile na kutafsiri CCM na kuigeuza kuwa CCK (Chama Cha Kiislam) maana inaonekana unasahau kuwa halmashauri ya Tarime inaongozwa na Chadema (labda watu wa Tarime nao ni wachaga)!
 

Bw. Mgaya,
Nafikiri ni vema kutoifanya hii hoja kuwa ni ya CCM vs CHADEMA, bali iwe a fair analysis ya yasiyopendeza ndani ya CHADEMA kwani huenda kikawa chama chenye mguso kwa taifa zima kama hayo yasemwayo yakirekebishwa.

CCM ni grand party ambayo kwa wakati fulani kila mtu alikuwa mwanachama by default, kwa hiyo ni vigumu kuishutumu kuwa ina misingi ya udini n.k., hata kama takwimu ulizoweka ni sahihi, bado ni rahisi kwa CCM kujitetea kwa sababu ya historia yake. Hii ni tofauti kwa CHADEMA. Pia, hata kama CCM ina 75% ya viongozi wa juu wakiwa wa dini moja, hii haihalalishi CHADEMA nao kuwa na mfumo wenye sura ya kikabila.
 

Kubwajinga

1. Matangazo ya gazetini pekee ya mwaka mmoja hayatoshi kuweka sura ya ruzuku kusambazwa kwa kuwa hayawezi kutaja orodha ya wilaya zote zilizopokea ruzuku. Si unajua kwamba huwa zinachapwa audited statements ambazo ni summary? Sheria ya vyama vya siasa inasema msajili anawajibu wa kuchapa mahesabu ya vyama. Sasa kamuulize msajili kwa nini hachapi wakati CHADEMA inampelekea kila wakati? CHADEMA wakati wote inaweka wazi matumizi yake kwa wanachama kupitia vikao ikiwemo kiasi kilichosambazwa na jina la eneo. Mimi ya kwetu niliyapata Zanzibar. Lakini baada ya baraza kuu unakumbuka Tamko la CHADEMA lilionyesha kwamba wajumbe walijadili na kupitisha ripoti ya fedha ikiwemo mgawanyo wa ruzuku?

2. Hilo la Uchagga wa sekretariati acha kuwasingizia. Mbona iliwahi kusemwa hapa kwamba Wasukuma ni wengi kuliko wachagga? Kama wasukuma ni zaidi ya 30% katika makao makuu ya CHADEMA kwanini unawataja wachagga tu wakati mwenyewe umesema ni 25&, au unafanya spinning? Na ni kiongozi gani wa sekretariati au mbunge ambaye amechaguliwa kwa shinikizo la Freeman kutokana na mchango wake ambao amechangia chama yeye kama Freeman?

Hebu Mods tuleteeni tena hapa tamko la CHADEMA walilolitoa kujibu suala la Uchagga, au tupe link ambapo suala hili lilishajadiliwa na kujibiwa na Zitto, Mnyika, Kitila na wengineo.

Wallah napata uchungu haya mambo kurudiwa rudiwa ili hali yalishajibiwa mpaka makada wa CCM wakasalimu amri wakati huo

Asha
 

Historia ipi hiyo ya CHADEMA inaonyesha kuwa ni chama chama cha wachagga? Hebu soma historia ya CHADEMA kwenye tovuti uone jinsi toka wakati chama kinaanzishwa Mzee Mtei pamoja na kuwa alikuwa mchagga lakini alijenga misingi ya chama chenye sura ya kitaifa.

Ama utakumbuka mchangiaji mmoja humu Paparazi Muwazi aliweka hii habari hapa. Ambayo hakika nimeihifadhi katika kumbukumbu zangu- hii nadhani itakupa majibu kwa maswali yao:




MNYIKA: CHADEMA SI CHAMA CHA WACHAGA
• Asema wachaga wako mpaka serikalini
• Atoa rai kwa watanzania kuwakanya wanachochea ukabila


Na Mwandishi wetu

 

Jamani kuna mtu mwenye ile makala ya Mzee Mtei aliyoandika "CHADEMA ni nini, CHADEMA ni nani?" ambapo aliweka wazi historia ya kuanzishwa kwa CHADEMA na wakina nani alianzisha nao na katika maeneo gani? Iliwahi kuwekwa hapa JF na kati ya Zitto au Mnyika; hebu toeni link basi

Asha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…