CHADEMA na ndoto za kumuondoa Meya Arusha!

CHADEMA na ndoto za kumuondoa Meya Arusha!

Sheria hiyo ni nzuri sana, Cha msingi itisheni uchaguzi wa haki na amani halafu ikikosekana hiyo 2/3 basi aendelee na ikipatikana ampishe mwingine. Ya nini kulumbana sana.

Uchaguzi ulishafanyika siku nyingi mlipozira! Ndio faida ya kuzira!
 
Tatizo ni dogo sana umechanganya uongo na ukweli pamoja ndo maana hauliki! Ni kweli kuwa mie muumini wa uimara wa upinzani kuisaidia CCM kufanya vizuri zaidi.Na imani hii siisemei chumbani naisema hadharani. Mengine ni hisia zako ambazo hazinihusu!

ningekuwa mhariri wa gazeti kesho ningeibuka na kichwa cha habari:

Nape: Mimi ni Muumini wa Chadema

Ipo siku Nape tutakuvalisha gwanda!!!
 
Sihusiki na hisia zako, huu ndio ukweli Chama makini kingejadili kuwatumikia watu badala ya kupoteza siku nzima mnajadili jambo lisilowezekana

Huwezi kujadili jinsi ya kupata madini bila kuzungumzia kupasua miamba.....Meya ni kizingiti kwa madiwani wa Arusha kuwatumikia wananchi ipasavyo....ni muhimu kwa chama makini kuzungumzia jinsi ya kuondoa kikwazo cha wao kutekeleza sera zenye manufaa kwa wananchi!
Asante
 
Hizi kauli ndo zinatuharibia chama Nape, sijui hamjui hali halisi huku mitaani au mnajua ila mnapuuzia!! au ndio mmeamua kuua chama wakati sisi tikijitahidi kukijenga!!! inakatisha tamaa sana kwa sisi wanachama na viongozi wa ccm, unapokuwa kiongozi sometime kabla hujaandika tafuta hata ushauri kwanza, tuache ushabiki jamani, ccm yetu inakufa taratibu, namna ya kurudisha imani kwa watu ni kwa kuwa wakeli, kutumikia watu kwa weledi na kuleta chama kwa watu!!! issue ya arusha mlishauriwa kuanzia mwanzo kuwa zile mbinu za kuchagua meya hazitasaidia, zitabomoa chama, sitazidisha chuki na zitakiangamiza chama ccm kanda ya kaskazini!!!! Tusidharau hii kanda ya kaskazini Nape, hii kanda ni muhimu sana, kuna wasomi wengi na wanaojijuia, wako kila mahali, ni kama kwa wazungu ambavyo hawawadharau hata siku moja Waisrael!!!! Nafikiri kuna haja ya kuwa na mradi kabambe kabisa wa kukusanya maoni nchi mzima Nape kutoka kwa wana CCM ya namna ya kuboresha chama, kama tunatakitakia mema chama chetu lkn,!! otherwise tutakataliwa nchi nzima kama arusha walivyotukataaa!!!! Mwenyenzi Mungu mwingi wa Rhehema na Utukufu atujalie kuyaona haya!!!!!!

Kumbe ccm kuna watu waliobaki wenye busara hihi? Mi ndo mara ya kwanza nimemkubali mwanaCCM hongera ila nakushauri uwahame make watakupaka kinyesi!
 
Kwa idadi ya madiwani katika Jiji la Arusha na mgawanyo wake hakuna chama kinachoweza kufikisha 2/3 ya madiwani na kwa kuwa kanuni zinasema ili umwondoe Meya kwa kura ya kutokua na imani naye lazima upate 2/3 ya madiwani wote...

Hata kama ni lazima upate 2/3 kufanikisha a no confidence vote, CHADEMA wanahitaji kura tano zaidi kufikisha hiyo 2/3. Ukichukua mbili za TLP, ni kazi rahisi kupata tatu kutoka CCM. Nasema ni kazi rahisi maana kuna madiwani wenu wana hasira za kuliwa wake zao, thanks to Savimbi
 
Kelele nyiiiiingi mi nilidhani Arusha yote ni CDM kumbe mambo ni hivi.
Nasikia hata kura walizopata CCM uchaguzi huu ni nyingi kuliko 2010.
Ni ndoto na kujidanganya eti CCM itaondoka 2015!!

Na hapo bado Kiti Maalum cha TLP!
 
nape ningekuona wa maana kama ungejaribu kukumbuka niwatu wangapi wamepoteza maisha hapo arusha,kutokana na mabavu waliyoonyeshwa na chama chako kwakutumia vyombo vya dora.tangu wananchi wa arusha wakatae chama chenu mmewafanyia sarakasi nyingi zilizopelekea watu kufa.kuanzia kwenye kulazimisha kumweka huyo mayor wenu hata juzi kwenye marudio yakata hizo.sometimes its better kufikiria haya kuliko umayor.

Hapo penye red, Nape atakuambia wapigwe au wauawe tu.
 
Kujipa matumaini ni jambo zuri lakini kujipa matumaini ya uongo ni jambo la hovyo! Kwa idadi ya madiwani katika Jiji la Arusha na mgawanyo wake hakuna chama kinachoweza kufikisha 2/3 ya madiwani na kwa kuwa kanuni zinasema ili umwondoe Meya kwa kura ya kutokua na imani naye lazima upate 2/3 ya madiwani wote, basi Meya is there to stay!

Ushauri wangu ni kuwa waliochaguliwa wafanye kazi ya kuwatumikia wananchi badala ya kuahangaika na ndoto za mchana!
Naumia sana kusikia kua kumbe tatitizo lilikua umeya wakati mmewaua ndugu zangu,mjane wa ndugu yangu na vitoto wanateseka pasipo matumaini,,MUNGU ASIWAACHE HIVIHIVI KWA UROHO WA UMEYA....NDUGU YANGU NAPE 4SURE NIMEUMIA...NATOKWA KWA MACHOZI NA KUANZIA LEO MIMI SI MWANA CCM TENA....NITAJITAIDI KUIRUDISHA KADI YE CCM KATIKA UZINDUZI WA KAMPENI ZA CCM SOMBETINI....NIMEUMIA...KUMBE THE PROBLEM WAS UMEYA?????MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU WABARIKI WAHANGA WA MABOMU NA UWAAIBISHE WAHUSIKA WOTE WA TUKIO HILO....
 
Wakuu, naona mnahangaika sana katika masuala ya kisheria. Nape yuko sahihi. hebu tujikumbushe jinsi Madiwani wa Mwanza walivyomng'oa Meya wao

[h=2]Madiwani Mwanza wamng'oa Meya wa halmashauri wapiga kura ya kutokuwa na imani naye
[/h]





[COLOR=#]Rate This[/COLOR]​



Aliyekuwa mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza,Bw.Josephat Manyerere ameng'olewa katika nafasi hiyo jana baada ya kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye na Madiwani,wakimtuhumu kutumia wadhifa wake vibaya,kushiriki vitendo vya rushwa na kushindwa kufanya kazi.

Kwa mujibu wa Fullshangwe tuhuma zingine dhidi ya Diwani huyo wa Kata ya Nyakato (CHADEMA) ni mwenendo mbaya wa ukosefu wa adabu ulemavu wa kimwili au kiakili kiasi cha kumfanya ashindwe kutekeleza majukumu yake kama mwenyekiti wa vikao vya halmashauri ya jiji.


Kutokana na kadhia hiyo, Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Bw.Wilson Kabwe, aliwasilisha hoja ya Madiwani waliojiorodhesha na kufikia theluthi mbili ya wajumbe wapatao 17 kati ya wajumbe 33 wa vikao halali vya baraza la madiwani wa Jiji hilo,alidai suala hilo ni la kisheria na kanuni ya 80 za kudumu za halmashauri hiyo.

"Halmashauri inaweza kumuondoa Mwenyekiti au Meya madarakani kwa azimio linaloungwa mkono na theluthi mbili ya wajumbe kutokana na sababu yoyote ya ni (a) Kutumia nafasi yake vibaya(b),Kushiriki vitendo vya rushwa(c),Kushindwa kazi(d),Mwenendo mbaya wa ukosefu wa adabu na(e) ulemavu wa kimwili aidha kiakili kwa kiasi cha kumfanya kushindwa kutekeleza majukumu yake kama Mwenyekiti ama Meya." Alifanunua Kabwe.

Tuhuma hizo kumi zilizowasilishwa kwa wajumbe na kusababisha kung'olewa kwake zilitajwa kwanza ni pamoja na kusimamia ujenzi wa kanisa moja bila kufuata utaratibu na kanuni za Halmashauri,kutoa maelezo kwa barua ya kushinikiza madiwani wenzake kuihoji na kupinga bajeti ambayo kimsingi na kikanuni bajeti hiyo niya kwakwe pia na ndiye msimamizi akiwa Meya.

Kabla ya kung'olewa akifungua kikao hicho aliyekuwa Meya Bw.Manyerere, baada ya kusomwa dua na baadhi ya madiwani kama alivyoomba Meya huyo kutokana na imani za dini za Kikristo na Kiislamu, ambapo Meya huyo alimwomba Katibu wa baraza hilo kusoma Ajenda ya kikao hicho cha dharula kwa wajumbe, kufuatia ombi la madiwani kwa barua yao waliyoiwasilisha tangu Mei 24 mwaka huu.
Kabwe ,alisema kuwa katika kikao hicho ajenda ni moja tu ya wajumbe kutokuwa na imani na Meya hivyo kanuni ya 80 ya kumuondoa madarakani waliyoomba itekelezwe lakini kabla ya kufanya uamuzi huo baraza hilo lilitakiwa kujibadili na kukaa kama kamati.
Meya Manyerere aliwahoji wajumbe 28 kati ya 33 waliohudhuria kikao hicho kulingana na kanuni,sheria na taratibu za halmashauri wanaokubali waseme hoja hiyo imeafikiwa na wanaopinga waseme hapana.
"Wajumbe hoja hiyo iliyotolewa, wanaosema ndiyo waseme inaafikiwa ambapo bila kujali itikadi zao za vyama vya siasa kwa kauli moja madiwani hao waliitikia Ndiyooooooooo!!! "na hakuna madiwani waliopinga hoja hiyo kwa kusema hapana.
Baada ya kukubalika kwa hoja hiyo Mkurugenzi huyo wa Jiji,aliwataka watu wasio wajumbe wa kikao hicho cha Kamati kutoka nje ya ukumbi huku viongozi waalikwa waliongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Evarist Ndikilo,Katibu Tawala, Dorothy Mwanyika na Wakuu wa wilaya na Ilemela, Baraka Konisaga (Nyamagana) na Amina Masenza (Ilemela) wakitakiwa kubaki kwa mujibu wa taratibu za Halmashauri.
Baada ya hatua hiyo baraza lilirejea kama kawaida,ambapo lilisikiliza utetezi wa Meya Bw.Manyerere ambapo katika madai hayo kumi yaliyowasilishwa kuhusu tuhuma zilizokuwa zinamkabili kusomwa, alijitetea kabla ya kufanyika uamuzi wa wajumbe kupiga kura za kumuondoa madarakani ama kumuacha aendelee na nafasi yake ya Umeya.
Baada ya Naibu Meya kutangaza matokeo ya kura za kumng'oa Meya Manyerere aliwaambia Madiwani hao kwa kutumia kauli kama ilivyokuwa kwa aliyekuwa Waziri Mkuu katika utawala wa serikali ya awamu ya nne Bw.Edward Lowassa, alipojiuzulu wadhifa wake kufuatia sakata la kampuni ya kufua umeme ya Richmond,".

"Tunapokezana kijiti,mimi siwezi kusikitika lakini kama ni kwa mtindo huo, hata aingie nani,hata aingie nani.Niwatakie eh shughuli njema kwa kuwa bado tunayo halmashauri yetu,baada ya kugawanywa kusema eti lakini provided bado tupo pamoja na basi sitaji feel sana inferior, kwa sababu ndiyo uamuzi wenu ndiyo mliniona;"
"Lakini niwaombe tu kwamba unapomchukia mtu kwa kitu,kwa sababu kuna ile chuki binafsi na kama hiyo ndiyo ita to read kwenye maongozi basi hatutafika.Basi nibaki tu kusema kama mheshimwa Lowassa alivyosema,kwamba kama shida ni Uwaziri Mkuu ? Basi kama shida ilikuwa ni Umeya basi is okay, nawatakia kazi njema na amani kwa bwana Sharom,"alisema Meya huyo wa zamani wa jiji la Mwanza,Manyerere
Naibu Meya wa Jiji hilo na Diwani wa Kata ya Mahina, Bw.Charles Chichibela (CHADEMA) ambaye kwa sasa ataliongoza kwa muda baraza hilo akitangaza matokeo ya kura hizo alisema kura 20 zilikuwa zimemkataa Meya huyo kati ya kura 28 zilizopigwa.
Meya huyo anadaiwa kushindwa kufanya kazi yake na kusimamia kanuni na utaratibu za vikao vya halmashauri na kusababisha fujo bila kuchukua hatua kama kanuni zinavyomtaka.Kwamba katika vikao vyote alivyoendesha aliruhusu fujo kutokea na kusababisha aitwe kwenye kamati ya maadili ambayo aliidharau.
Kwamba alishindwa kutunza siri za halmashauri akiwa kiongozi mkuu wa madaiwani wa halmashauri ya Jiji la Mwanza,pia alishindwa kuzuia kuvuja kwa kabrasha la bajeti ya halmashauri hiyo,akishirki kikao kilichofanyika katika hoteli ya G&G Mei 13 mwaka huu.
Meya huyo tangu achaguliwe kiushika wadhifa huo alishindwa kabisa kusimamia mikutano ya Jiji, ikiwa ni pamoja na kusahindwa kusimamia ratiba za vikao na kanuni za halmashauri na kusababisha zogo la mara kwa mara kwa madiwani,ambao amekuwa akihoji maazimio ya mikutano anayoisimamia na kutia saini.
Ilidaiwa katika tuhuma hizo kuwa Manyerere akiwa Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza, alitia saini mikataba bila kupitishwa na vikao vya halali vya baraza la madiwani.anatuhumiwa kusaini mkataba wa Sheriff na kusababisha shule ya msingi Mbugani kuchukuliwa na taasisi ya watu binafsi kutoka serikalini.
Tuhuma nyingine ni kukataa kusaini mikataba halali iliyoazimiwa na baraza la madiwani, hivyo kuchelewesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya Jiji la Mwanza, ambapo pia anatuhumiwa kutumia madaraka ya ofisi yake vibaya kwa kutoa upendeleo dhidi ya madiwani wenye uhusiano wa karibu naye ama wanaomwunga mkono.
Kabla ya Naibu Meya kutangaza matokeo hayo diwani wa Kata Sangabuye Bw.Dede Swila Dede alisimama na kuomba mwongozo ambapo alimtaka Meya Bw. Manyerere kupisha katika nafasi hiyo na kuchukuliwa na Naibu Meya Bw. Chichibela ili kuendesha kikao hicho na kutangaza matokea hayo.
"Tumepiga kura na madiwani waliosema kwamba Meya Bw.Manyerere ang'oke kwenye wadhifa huo ni wajumbe 20 na waliosema aendelee kubaki ni wajumbe nane tu (8 ) hivyo kwa mujibu wa matokeo hayo namuomba Mkurugenzi atusaidie kufafanua kanuni zetu zinasemaje"alisema Naibu huyo.
Madai ambayo yaliwasilishwa na madiwani hao kwa hoja iliyotolewa na Diwani wa CCM Kata ya Bugogwa, Dede Swila (CCM)na kuungwa mkonona Diwani wa Kata ya Igoma,Adam Chagulani (CHADEMA) wakati akichangia hoja kwenye baraza hilo kwa Diwani wa Kata ya Igoma (CHADEMA ) alionekana kuwahamasisha na kuwagusa baadhi ya wajumbe kwa kuiwasilisha upya baada ya Mkurugenzi kukataa barua ya hoja hiyo mwanzoni kwa madai kwamba haikufuata utaratibu na kanuni za vikao.
 
Kujipa matumaini ni jambo zuri lakini kujipa matumaini ya uongo ni jambo la hovyo! Kwa idadi ya madiwani katika Jiji la Arusha na mgawanyo wake hakuna chama kinachoweza kufikisha 2/3 ya madiwani na kwa kuwa kanuni zinasema ili umwondoe Meya kwa kura ya kutokua na imani naye lazima upate 2/3 ya madiwani wote, basi Meya is there to stay!

Ushauri wangu ni kuwa waliochaguliwa wafanye kazi ya kuwatumikia wananchi badala ya kuahangaika na ndoto za mchana!

Mzee kwani alichaguliwa kwa sheria ipi? 2/3 aliipata? Arusha kunaitaji mazungumzo ya kina kwa maendeleo ya wana Arusha, muda aliotumikia unatosha, sasa ni zamu ya CDM kama walivyofanya Kigoma.
 
Ndugu yangu acha hofu isiyo na sababu, hawa jamaa zako hata ukiwapa mbinu zako zote kwenye maandishi ni sawa na kumpa nguruwe pilau halafu ukitegemea aburudike wakati hajui hata kumugunya. Ebu fikiria mijitu kama vile imelogwa ianenda kulipua mabomu kwenye mikutano, inaenda kutengeneza video za ugaidi na mizinga sijui kama kweli Nape Nnauye naye ni sehemu ya jopo la ma-editors au naye ni mtazamaji tu, atajibu mwenyewe.

Njia pekee waliyobaki nayo ni kuita polisi na jeshi tu pale wanapokosa hoja lakini sasa na baba yao (Mwenyekiti wa CCM) amewazuia waache kukimbilia polisi sijui anataka wafanyeje? Kinana huyo ameamua kuufyata, nasikia ameenda mahakamani kufungua kesi ili watu wanyamaze apate kuwa-kinana TEMBOs wetu vizuri, makamu mwenyekiti huyo kakimbilia shambani kwake baada ya kukuta Chama kilishaota kutu hakisuguliki hata kwa jiki.

Sijui siku Polisi na jeshi watakapoelimika na wao kukataa kutumiwa kama ma-loboti hawa jamaa watafanyaje, halafu huwa hwajiulizi mbadala wa mbinu yao hii ya mwisho utakuwa nini....!!

Watu wa Chadema kuweni makini Nape Nnauye anachokonoa mada makusudi wengine wanaanza kutoa siri bila kujua wakidhani wanamtisha.

Kuweni makini mada zingine zina malengo maalum.
 
Mzee kwani alichaguliwa kwa sheria ipi? 2/3 aliipata? Arusha kunaitaji mazungumzo ya kina kwa maendeleo ya wana Arusha, muda aliotumikia unatosha, sasa ni zamu ya CDM kama walivyofanya Kigoma.

mkuu, madaraka hayalazimishwi. subiri muda utafika tu na si kulazimisha kwa sasa
 
Sihusiki na hisia zako, huu ndio ukweli Chama makini kingejadili kuwatumikia watu badala ya kupoteza siku nzima mnajadili jambo lisilowezekana

Hapo napingana na wewe. Iweje uchaguzi ufanyike kimagumashi halafu suala la kumtoa zishikiliwe kanuni??. Na unauhakika gani kuwa hiyo 2/3 haitafika??? Acha watu watumie demokrasia yao kama watashindwa basi....
 
Kujipa matumaini ni jambo zuri lakini kujipa matumaini ya uongo ni jambo la hovyo! Kwa idadi ya madiwani katika Jiji la Arusha na mgawanyo wake hakuna chama kinachoweza kufikisha 2/3 ya madiwani na kwa kuwa kanuni zinasema ili umwondoe Meya kwa kura ya kutokua na imani naye lazima upate 2/3 ya madiwani wote, basi Meya is there to stay!

Ushauri wangu ni kuwa waliochaguliwa wafanye kazi ya kuwatumikia wananchi badala ya kuahangaika na ndoto za mchana!
Hakuna uongo wowote hapo Nape, 2/3 kwa idadi iliyopo sasa ni 16! na CDM ina 15 sasa kumbuka hata ccm kuna mamluki na hilo ndilo linalowasumba labda kama kura zitapigwa za wazi lakini kama ni siri Meya anaondoka bila ubishi.

Naomba nikuulize ulikuwa mlokole unayehubiri mimbarani.. hivi nini kimekupata ndugu yangu maana kubwa kuliko yote ni uzima wa milele.. au umeupa kichogo?
 
Ningejuaje kama usingesema, ungesemaje kama nisingesema? Ahsante kwa taarifa

Kidogo Nape kwa thread yako ya leo ya kichokozi nimeipenda,umeonekana kama mchokozi lakini mwenye ufahamu!!!Ebu jijengeni kuwa watu wa kushindana na CDM kwa hoja ya kuwin wananchi,lakini si yale mawazo ya kuiangamiza CDM na tuhuma na matendo yenye sura mbaya.

Kwa statement yako hapo juu,kama kweli your great thinker inatosha kukupa sura ya either unyoe au usuke kupata jawabu la tiba.Yani vice versa is true!!!ndivyo mlikuwa mnapayuka na kutenda wananchi wasivyopenda kwenye eneo husika la mnyukano wa kujinadi.

Kwa taadhali hiyo baada ya kuangaika kuisurubu CDM ambae kwa kuzaliwa kwake tayari ni mkinzani [Opposition] wako wewe kama CCM basi shughurika na watu wako huku pia ukishughurika ni vipi utawin kiti hicho cha umeya hata ikibidi kwa gharama ya wao opposition kama wao wanavyoangaika kuwin kiti hicho ikibidi kwa gharama ya CCM.

Utamu wa siasa uwe kwenye HOJA na MANIPULATION na sio DEMAGE kwenye jamii na opposition parties.Ebu jaribu kuwa smart kama ulivyotumia statement hii " Ningejuaje kama usingesema, ungesemaje kama nisingesema? Ahsante kwa taarifa" .Kama kuna statement bora nimepata kuisikia kutoka kwako yenye kuonyesha hoja inajibiw akwa hoja basi hii ni YA KWANZA.

Ebu tumieni HOJA KUJIBU HOJA KWA UHAKIKA !!Na kama mnaleta thread mjipange kuzijibu kwa hoja na statement zinazonyesha werevu na ufahamu wa hali halisia na sio kukurupuka na bora liende kuwa mmewajibu CDM au mmepata nafasi ya kuwaproveke humu JF.

Na kama ni ya kichokonozi au propaganda basi iwe imeenda shule kiasi kuwa nasi wengine tuone raha ya vyama vya siasa vyenye nia na uthabiti wa kujenga Nchi kupitia kauri na matamshi.Baba wa Taifa akipata kusema ukimsikiliza mtu anaeomba nafasi ya kupewa madaraka ya umma, basi kupitia KAURI zake tukimwangalia USONI tuseme huyu nae kweli!!!
 
Kujipa matumaini ni jambo zuri lakini kujipa matumaini ya uongo ni jambo la hovyo! Kwa idadi ya madiwani katika Jiji la Arusha na mgawanyo wake hakuna chama kinachoweza kufikisha 2/3 ya madiwani na kwa kuwa kanuni zinasema ili umwondoe Meya kwa kura ya kutokua na imani naye lazima upate 2/3 ya madiwani wote, basi Meya is there to stay!

Ushauri wangu ni kuwa waliochaguliwa wafanye kazi ya kuwatumikia wananchi badala ya kuahangaika na ndoto za mchana!
Naumia sana kusikia kua kumbe tatitizo lilikua umeya wakati mmewaua ndugu zangu,mjane wa ndugu yangu na vitoto wanateseka pasipo matumaini,,MUNGU ASIWAACHE HIVIHIVI KWA UROHO WA UMEYA....NDUGU YANGU NAPE 4SURE NIMEUMIA...NATOKWA KWA MACHOZI NA KUANZIA LEO MIMI SI MWANA CCM TENA....NITAJITAIDI KUIRUDISHA KADI YE CCM KATIKA UZINDUZI WA KAMPENI ZA CCM SOMBETINI....NIMEUMIA...KUMBE THE PROBLEM WAS UMEYA?????MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU WABARIKI WAHANGA WA MABOMU NA UWAAIBISHE WAHUSIKA WOTE WA TUKIO HILO....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom