MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 20,582
- 42,548
Kwa ambaye hajafika Arusha kwa miaka mitatu iliyopita akienda kwa sasa lazima ashangae kila kitu. Hapa namaanisha mkoa mzima wa Arusha yaani kuanzia Arusha jiji hadi huko wilayani. Yaani mkoa mzima umechafuka maendeleo ndani ya miaka mitatu tu. Mimi hadi naandika huu uzi bado ninatafakari kwa kina hii kasi ya maendeleo mama kaiwezaje?
Kwa mfano Arusha mjini hadi 2020 sehemu nyingi hazikuwa na barabara za lami ila ghafla ndani ya miaka michache lami zimemwagwa hadi mitaa ya ndanindani huko Sokoni 1, Unga Ltd. Kwa sasa unapiga lami kutoka town (france corner) hadi huko Nadosoito wakati lami ilikuwa haifiki hara dampo. Kwa sasa shortcut zimekuwa mingi ile laana. Kikubwa zaidi zinapigwa njia nne town hadi Kisongo, yaani ni hekaheka, Mama anaupiga mwingi.
Huko wilayani Karatu nako sehemu iliyokuwa makao makuu ya vumbi kwa sasa zimetandazwa lami mitaa yote ya mjini. Vumbi imekuwa historia. Na kwa vile mama anaupambania utalii kwa sasa huo mji mdogo umekuwa na camps, lodges na hotel za hadhi ya juu. Wawekezaji wamefurika. Kimsingi ukiitoa Arusha inafuatia Karatu kwa shughuli nyingi za utalii. Huko kaskazini watu wanatajirika sana kwenye uongozi huu wa Dr Mama Samia.
Kwa mkoa wa Arusha mama kafanya makubwa mno. HATUMDAI. Mama Samia ni kiongozi mwema mwenye upendo na watanzania wote. Nilipita Lindi pia naona kwa sasa nao hawako nyuma. Nyumba za kisasa zimejengwa nyingi huko.
Kwa mfano Arusha mjini hadi 2020 sehemu nyingi hazikuwa na barabara za lami ila ghafla ndani ya miaka michache lami zimemwagwa hadi mitaa ya ndanindani huko Sokoni 1, Unga Ltd. Kwa sasa unapiga lami kutoka town (france corner) hadi huko Nadosoito wakati lami ilikuwa haifiki hara dampo. Kwa sasa shortcut zimekuwa mingi ile laana. Kikubwa zaidi zinapigwa njia nne town hadi Kisongo, yaani ni hekaheka, Mama anaupiga mwingi.
Huko wilayani Karatu nako sehemu iliyokuwa makao makuu ya vumbi kwa sasa zimetandazwa lami mitaa yote ya mjini. Vumbi imekuwa historia. Na kwa vile mama anaupambania utalii kwa sasa huo mji mdogo umekuwa na camps, lodges na hotel za hadhi ya juu. Wawekezaji wamefurika. Kimsingi ukiitoa Arusha inafuatia Karatu kwa shughuli nyingi za utalii. Huko kaskazini watu wanatajirika sana kwenye uongozi huu wa Dr Mama Samia.
Kwa mkoa wa Arusha mama kafanya makubwa mno. HATUMDAI. Mama Samia ni kiongozi mwema mwenye upendo na watanzania wote. Nilipita Lindi pia naona kwa sasa nao hawako nyuma. Nyumba za kisasa zimejengwa nyingi huko.