CHADEMA imewasaliti Watanzania

CHADEMA imewasaliti Watanzania

Yeye ndio ameweka masharti aachiwe huru ili aweze kuingia katika mazungumzo, hapo usaliti upo wapi ? Kwenye mazungumzo kuna kukubaliana na kukataliana pia
Pia,

Hawa watu wanakataa vipi masharti ya kisiasa katika kumtoa Lissu gerezani wakati kesi nzima ni ya kisiasa?

Where is the logic here?

Ozon
 
Simfurahii wala simchukii Lissu, na ningependa atoke gerezani haraka. Hata hivyo, tukitafakari kwa utulivu bila hisia, suala la maridhiano lilipaswa kufanyika kabla ya uchaguzi wa Oktoba 29; huo ndio uliokuwa msimamo wa CHADEMA na baadhi ya Watanzania.

Badala yake, kuliripotiwa matukio mabaya yaliyosababisha vifo na madhara makubwa, huku serikali ikiendelea kubaki madarakani.

Baada ya matukio hayo, kuanzisha mazungumzo kunaibua maswali, je, wale waliokataa mazungumzo kabla ya uchaguzi sasa watayakubali baada ya hali kubadilika?

Ninasisitiza kuwa naheshimu Lissu, lakini siweki imani yangu yote kwa wanasiasa.
Wanasemaga kwenye siasa hakuna Rafiki wa kudumu wala Adui wa kudumu !
Ngoja Tusubiri tuone !
 
Sasa wakikubali mazungumzo haya ambayo wameyawekea masharti na misimamo yake, kwa kuzingatia masharti na misimamo hiyo, tatizo liko wapi?
Mazungumzo na wanaodaiwa kuwa wahalifu? Mazungumzo na watu ambao hawataki kuwajibishwa? Kwa sasa, mazungumzo si jambo linalopaswa hata kufikiriwa; ni hatua ya mwisho kabisa. Kuna mambo ya msingi ambayo yanapaswa kupewa kipaumbele, na ambayo hayahitaji kukaa meza moja na kufanya mazungumzo.
 
Mazungumzo na wanaodaiwa kuwa wahalifu? Mazungumzo na watu ambao hawataki kuwajibishwa? Kwa sasa, mazungumzo si jambo linalopaswa hata kufikiriwa; ni hatua ya mwisho kabisa. Kuna mambo ya msingi ambayo yanapaswa kupewa kipaumbele, na ambayo hayahitaji kukaa meza moja na kufanya mazungumzo.
Haya,

Usipotaka mazungumzo una jeshi gani la kupindua serikali?

Mmeandamana mmeuawa kama digidigi.

Mtafanya nini zaidi ya mazungumzo?
 
Pia,

Hawa watu wanakataa vipi masharti ya kisiasa katika kumtoa Lissu gerezani wakati kesi nzima ni ya kisiasa?

Where is the logic here?

Ozon
Kulingana na taarifa hiyo ya chama, kuna hoja (au masharti) aliyotoa Lissu kuelekea kile kinachoitwa mazungumzo. Hata hivyo, kwa nini hoja ya kwanza kabisa na ya msingi kwake ni kuachiwa huru kabla ya kufanyika kwa mazungumzo yoyote?
 
Kulingana na taarifa hiyo ya chama, kuna hoja (au masharti) aliyotoa Lissu kuelekea kile kinachoitwa mazungumzo. Hata hivyo, kwa nini hoja ya kwanza kabisa na ya msingi kwake ni kuachiwa huru kabla ya kufanyika kwa mazungumzo yoyote?
Sasa unataka afanye mazungumzo kutoka jela?

Huoni kuwa hiyo tu ni negotiating from a position of weakness?
 
Sasa wakikubali mazungumzo haya ambayo wameyawekea masharti na misimamo yake, kwa kuzingatia masharti na misimamo hiyo, tatizo liko wapi?
Na hapo ndo usaliti wake kwa Watanzania unapokuja. Kwahiyo mazungumzo ni ya CHADEMA na CCM/serikali baada ya serikali kutimiza takwa lao la kisiasa? Hapa hakuna ukombozi wa maana na kama CHADEMA wanavyojinasibisha nao kama hii ndiyo namna wanavyofanya mazungumzo na ‘devil’.
 
Na hapo ndo usaliti wake kwa Watanzania unapokuja. Kwahiyo mazungumzo ni ya CHADEMA na CCM/serikali baada ya serikali kutimiza takwa lao la kisiasa? Hapa hakuna ukombozi wa maana na kama CHADEMA wanavyojinasibisha nao kama hii ndiyo namna wanavyofanya mazungumzo na ‘devil’.
Kesi ya kisiasa imefutwa kwa masharti ya kisiasa.

Tatizo lipo wapi?

Wewe unaruhusiwa kuanzisha chama chako halafu ukatae kuongea na huyo devil, umeanzisha?
 
Kufanya mazungumzo na wahalifu waliokataa kufanya maridhiano kabla ya uchaguzi wa tarehe 29 Oktoba?
Kuna vitu nje ya box,watawala wameminywa kende wanatapa tapa.

Wanatafuta picha kuweka kwamba lissu kawap9gia goti,lakini sio kweli hakuna maridhiano.

Usikubali kulishwa propaganda na media uchwara.
 
Haya,

Usipotaka mazungumzo una jeshi gani la kupindua serikali?

Mmeandamana mmeuawa kama digidigi.

Mtafanya nini zaidi ya mazungumzo?
Kushindwa kwetu sasa hakumaanishi kwamba haiwezekani tena. Lakini kama CHADEMA wanaona kwamba suluhisho la mwisho ni kufanya mazungumzo na ‘shetani’, basi wafanye hivyo, lakini hilo litakuwa kwa manufaa yao kama chama cha siasa tu, siyo cha ukombozi kama wanavyojiita kwa sasa.
 
Kesi ya kisiasa imefutwa kwa masharti ya kisiasa.

Tatizo lipo wapi?

Wewe unaruhusiwa kuanzisha chama chako halafu ukatae kuongea na huyo devil, umeanzisha?
Kama ndivyo ilivyo, basi CHADEMA hapa inaonekana kama chombo kinachotumika kudhoofisha au kuzima harakati za kupigania haki nchini. Bado tuna safari ndefu mbele.
 
Kama ndivyo ilivyo, basi CHADEMA hapa inaonekana kama chombo kinachotumika kudhoofisha au kuzima harakati za kupigania haki nchini. Bado tuna safari ndefu mbele.
Usilazimishe CHADEMA wawe na msimamo kama wako.

Hususan kwa sababu na wewe una haki za kuanzisha chama kama CHADEMA ukapigania haki unavyotaka wewe.

Nimekuuliza umeanzisha chama?

Hujajibu.

Sasa kwa nini unataka kuwapangia CHADEMA jinsi ya kuendesha chama chao?
 
Kushindwa kwetu sasa hakumaanishi kwamba haiwezekani tena. Lakini kama CHADEMA wanaona kwamba suluhisho la mwisho ni kufanya mazungumzo na ‘shetani’, basi wafanye hivyo, lakini hilo litakuwa kwa manufaa yao kama chama cha siasa tu, siyo cha ukombozi kama wanavyojiita kwa sasa.
Unalazimisha CHADEMA wawe na msimamo kama wako.

Unataka kuwa dikteta wa CHADEMA?
 
Mimi ni mmoja wa watu wa mwanzo kabisa kuona vifo ndio maana nipo hai, nimepoteza ndugu na marafiki, huo muda umefika lini? Nilishakuwepo.
Hongera na pole kwa dhati kabisa. Si kwamba napuuza au kudogosha ulichoandika, naona kama tuangalie alternative nyingine ambayo haimwagi damu. Tukiri kuwa hawa jamaa wanatumia maguvu mengi na hatujaona jumuiya ya kimataifa ikifanya harakati za makusudi.

Pia nimemwangalia kuhusu Mheshimiwa Tundu Lissu kama father figure na mtu mwenye upendo na taifa hili na uwezo wake mkubwa wa kufikiri kama kaona mazungumzo yanaweza kuleta tija, tumuamini tena.

Kama angekuwa mtu wa kuuza mechi hili angelifanya siku nyingi, alishapewa offer kibao na zinazojaza mdomo mate akakataa. Pia nimefikiria kwa upande wangu wa giza (Dark side) kuwa mambo kama haya yaliyotokea yanaweza kuleta impacts hatari.

Lets say mimi ndugu yangu kapotezwa, nashindwa kujimudu, naamua kununua milipuko naenda ktk mechi kubwa maarufu, halafu nafanya upalestina mpaka hata wasiohusika yanawakuta.
 
😀😀😀😀Yawezekana kweli jamaa wanapima upepo. Wanafanya utafiti mdogo kuona kama bado chama kinakubalika hata baada ya madhira yote kabla na baada ya Uchaguzi. Wajue tu ngoma bado ngumu na inaendelea kuwa ngumu cause shida si chadema, kwa sasa shida ni mbogamboga wenyewe wanavyojichanganya wakifikiri WaTz ni walewale wa siku zote.WAKATI NI UKUTA!
Huko ndani ya CCM yenyewe wakati huu hakuna wanachama wanaokubali huu upumbavu unaofanywa na hao wanaojiita viongozi wa chama.
CCM sasa hivi ni jina tu linalotumiwa na kundi la watu waovu waliowahi kuonekana ndani ya taifa hili.
 
Mkuu Mshana

Wazo zima la kufanya mazungumzo na CCM/Serikali linaonekana kuwa na kasoro tangu mwanzo. Je, CHADEMA wanaanzaje kufanya mazungumzo na wale waliokataa kufanya mazungumzo nao kabla ya tarehe 29 Oktoba?
Wewe toa ushauri ulitaka nini kifanyike? Siyo unalaumu bila kuwa wazo mbadala.
 
Hivi we una akili timamu? Amepambana kuliko waliofumuliwa vichwa october 29? Kuna sapoti kubwa kama ile ya october 29?, chadema haikushiriki maandamano lakini vijana waliingia mitaani kwa kupambania ajenda zilizopambaniwa na chadema, hivyo hata lissu ana deni, akitoka huko anatakiwa kuendeleza mapambano, watu wamemwagwa utumbo huku nje , yeye yuko jela lakini shavu dodo, TUNAWADAI
Naona kama unajichanganya. Huku mnasema kuwa waliouawa walikuwa wanapambana lakini kule mnasema wengi wa watu waliouawa Oktoba 29 hawakuhusika katika yale maandamano. Kwa mtazamo wangu Chadema kama Chadema haikuhusika sana katika kuwaamsha vijana. Mchango wa Mange ulikuwa mkubwa kuliko wa chama chochote cha siasa. Post zake Insta n.k. ziliwagusa vijana kuliko hotuba ya mwanasiasa yeyote. Hata Maria Sarungi na Clubhouse yake hakumfikia.

Amandla...
 
Inasemekana ametishiwa kuuawa kama alivyouawa hampered polepole kama ataendelea kupinga serikali haramu ya huyu bibi wa makunduchi
Cha ajabu hivi unajua kabisa kwamba una kundi kubwa tu linaloamini porojo kama hizi
 
Lissu anataka aachiwe ili aingie kwenye mazungumzo na serikali iliyoiba kura, imeua watu, wameteka kina Soka, Mdude, Polepole na wengineo . Kama atafanya hivyo utakuwa usaliti mkubwa.
 
Back
Top Bottom