CHADEMA imewasaliti Watanzania

CHADEMA imewasaliti Watanzania

Iwapo jambo hili ni kweli, basi ni wazi kwamba CHADEMA imewasaliti Watanzania.
View attachment 3574549ma
Kwahiyo ni sawa akae mpaka afe huko jela kesi ikiwa inaahirishwa tu ??! Au ??!
Hata Marekani na Iran wanapigana kisha wanaamua kuzungumza tena !!!
Mbona hawaamui kubaki na option moja tu ya VITA PEKEE ?? !

Kwenye mapambano yeyote yale Options zote huwa zipo mezani na kwamba itakayokuwa na manufaa ndiyo itakayotumiwa !
 
Lazima kuzungumza kueleza unachopigania, hats kama vita ni kali.
Kama hutazungumza basi hujui unachopigania.
Sio mazungumzo tu, chadema inahoja saba ikiwemo watu kuwajibika Kwa mauwaji ya October, tume huru, katiba mpya na zingine. Sasa mapoyoyo kama Yeriko Nyerere yameshindwa kuelewa ndio maana yanaitwa vishoia. Yamebaki kuongelea hoja ya mazungumzo pekee hoja hapa ni kwamba zote hoja saba lazima zitekelezwe watake wasitake ndio chadema iingie kwenye mazungumzo.
 
Kwa hyo wewe ulitaka afungwe miaka yote huku wewe ukiwa uraiani unaenjoy TU

Sion atakacho tusaliti njia nzur n yeye kuwa huru na KISHA kufanya majadiliano

NIMEGUNDUA KUNA WATU WANANUFAIKA NA LISU KUKAA JELA
 
Iwapo jambo hili ni kweli, basi ni wazi kwamba CHADEMA imewasaliti Watanzania.
View attachment 3574549ma
Alisema yuko tayari kwa mazungumzo akiwa huru na Chadema kufutiwa kesi zote, sasa hapo kasaliti nini? Kwa sababu kwa hali tuliyofikia hatuwezi kukwepa mazungumzo kabisa unless tungekuwa na majeshi na sisi tungesema mtanziko huu umalizwe kwenye uwanja wa mapambano. CCM wamepora uchaguzi kwa kutumia majeshi yake na kujisimika tena madarakani sasa utashindana nao vipi bila kukaa mezani? Nafikiri umekurupuka laa siyo wewe ni mccm mhafidhina.
 
Watu wamepoteza maisha kwa ajili ya nchi hii tarehe 29 October, Lisu bado yupo hai nani kapambana zaidi ya mwingine.!?
Cha ajabu wewe unaye mlaumu lissu huna hata kovu la fimbo, nanl huyo unaye mlaumu amekuwa na kesi zaidi 100 mahakamani kwa upinzani wake, amepigwa mara nyingi na kudhalilishwa na vyombo vya dola sababu ya upinzani wake, amepigwa risasi zaidi ya 10 mwilini mwake hadi kumpa kilema cha maisha sababu ya upinzani wake , amewekwa jela kwa zaidi ya mwaka sababu ya upinzani wake ,

Halafu wewe upo tuu umekaa nyuma ya keyboard mzima wa afya huijui jela wa mahakama, huzijui risasi wala mabomu unaenjoy tu na familia yako mwenzako ana mwaka haijui familia yake wala mke na watoto wake,halafu pamoja na hayo bado unalaumu na wakati msimamo wake upo bayana na ameusema wazi hata ya hivyo anao watetea ndio nyie mnajua kelele za mitandaoni tu hamtoi ushirikiano kwa vitendo,

Mimi nasema kwa aliyo yapitia kwa ajili ya hawa watanzania vilaza kama atabadilisha misiamamo sina deni nae kaumizwa sana kwa ajili ya kutetea mang'ombe yasiyo jitambua kama wewe yanayo jua kulaumu mtandaoni halafu field hayaendi

Wewe ukapimwe akili si bure una matatizo mengi na mengine ya akili na huna utu wala huruma
 
Nakubaliana nawe kabisa kwamba Lissu ni shujaa katika harakati za kupigania haki na demokrasia nchini Tanzania. Hata hivyo, hatua anayopanga kuchukua inaweza kuathiri sifa na heshima yake. Aidha, tukumbuke kuwa Watanzania wengi wamepoteza maisha wakipigania haki katika nchi hii; hivyo si vyema kutumia vifo vyao kwa manufaa ya kisiasa. Nina imani kwamba hatafanya hivyo
We jamaa uelewa wako wa mambo uko chini sana ingawa wewe unajiona uko smart , sasa wewe kwa akili yako unataka lissu aendelee kukaa gerezani kwa muda gani ili uone hajakusaliti? Maana kama ni kesi kawashinda kwa hoja ndio maana kesi imesimama lakini bado kwasababu ka kibri cha mamlaka wameendelea kumshikilia ndani wakati huo na ninyi mliopo huku uraiani mnamganga umbea na story za kina kajala na harmonize tuu!? Na ubishi simba na yanga jioni mnarud kwenu kula na kulala salama

haya niambie tangu lisu yupo gerezani wewe binafsi ni harakati gani umeifanya ili kubadilisha mfumo kandamizi ulipo sasa Au kuwatetea hao unao waita wananchi ? Ni kipi ulicho fanya hadi sasa ambacho kimeleta mabadiliko yeyote na Ambacho kinaunga mkono jitihata za lissu.? Au unalaumu huku unapiga mvinyo na kitimoto hapo bar kwa starehe zako.
 
Mapamano yaendeleee hakuna kurudi nyuma,kuwe kumetulia tu kwa muda, tunaamsha tena
Labda wameshaandaa mipango kwamba hata wakimuachia basi hatokuwa na madhara kma awali. Mbogamboga wanachowaza ni kutawala milele isitokee rais flani chama kimemfia mikononi mwake so, kila nguvu itatumika kuhakikisha chama kinasalia madarakani hadi pale kijiti kitakapopokelewa na mwingine.
 
Ni mada ya kichokonozi tu; haina lolote jipya..

Mtu ukitaka kupima upepo, anzisha mada ya kichokonozi kama hii.

Sasa wasomaji tukikubali kuwa "CHADEMA imewasaliti watanzania"..., halafu iweje? Tufurahi pamoja na hao wanaotukandamiza?

"CHADEMA imewasaliti watanzania"!
Kwa kufanya nini?
Wametangaza kuwa wanakubaliana na matakwa ya hao waovu waliopo madarakani kwa kutumia mabavu?

Uelewa wa kilichosemwa na hicho chama wa huyo mleta mada, ndicho kipimo sahihi cha kutuonyesha sisi wote kwamba "CHADEMA imewasaliti watanzania"?
😀😀😀😀Yawezekana kweli jamaa wanapima upepo. Wanafanya utafiti mdogo kuona kama bado chama kinakubalika hata baada ya madhira yote kabla na baada ya Uchaguzi. Wajue tu ngoma bado ngumu na inaendelea kuwa ngumu cause shida si chadema, kwa sasa shida ni mbogamboga wenyewe wanavyojichanganya wakifikiri WaTz ni walewale wa siku zote.WAKATI NI UKUTA!
 
Alisema yuko tayari kwa mazungumzo akiwa huru na Chadema kufutiwa kesi zote, sasa hapo kasaliti nini? Kwa sababu kwa hali tuliyofikia hatuwezi kukwepa mazungumzo kabisa unless tungekuwa na majeshi na sisi tungesema mtanziko huu umalizwe kwenye uwanja wa mapambano. CCM wamepora uchaguzi kwa kutumia majeshi yake na kujisimika tena madarakani sasa utashindana nao vipi bila kukaa mezani? Nafikiri umekurupuka laa siyo wewe ni mccm mhafidhina.
Hata Huko kwenye majeshi yenye nguvu za kila aina bado wanasisitiza wafanye maridhiano !
 
Cha ajabu wewe unaye mlaumu lissu huna hata kovu la fimbo, nanl huyo unaye mlaumu amekuwa na kesi zaidi 100 mahakamani kwa upinzani wake, amepigwa mara nyingi na kudhalilishwa na vyombo vya dola sababu ya upinzani wake, amepigwa risasi zaidi ya 10 mwilini mwake hadi kumpa kilema cha maisha sababu ya upinzani wake , amewekwa jela kwa zaidi ya mwaka sababu ya upinzani wake ,

Halafu wewe upo tuu umekaa nyuma ya keyboard mzima wa afya huijui jela wa mahakama, huzijui risasi wala mabomu unaenjoy tu na familia yako mwenzako ana mwaka haijui familia yake wala mke na watoto wake,halafu pamoja na hayo bado unalaumu na wakati msimamo wake upo bayana na ameusema wazi hata ya hivyo anao watetea ndio nyie mnajua kelele za mitandaoni tu hamtoi ushirikiano kwa vitendo,

Mimi nasema kwa aliyo yapitia kwa ajili ya hawa watanzania vilaza kama atabadilisha misiamamo sina deni nae kaumizwa sana kwa ajili ya kutetea mang'ombe yasiyo jitambua kama wewe yanayo jua kulaumu mtandaoni halafu field hayaendi

Wewe ukapimwe akili si bure una matatizo mengi na mengine ya akili na huna utu wala huruma
Simfurahii wala simchukii Lissu, na ningependa atoke gerezani haraka. Hata hivyo, tukitafakari kwa utulivu bila hisia, suala la maridhiano lilipaswa kufanyika kabla ya uchaguzi wa Oktoba 29; huo ndio uliokuwa msimamo wa CHADEMA na baadhi ya Watanzania.

Badala yake, kuliripotiwa matukio mabaya yaliyosababisha vifo na madhara makubwa, huku serikali ikiendelea kubaki madarakani.

Baada ya matukio hayo, kuanzisha mazungumzo kunaibua maswali, je, wale waliokataa mazungumzo kabla ya uchaguzi sasa watayakubali baada ya hali kubadilika?

Ninasisitiza kuwa naheshimu Lissu, lakini siweki imani yangu yote kwa wanasiasa.
 
Back
Top Bottom