CHADEMA imewasaliti Watanzania

CHADEMA imewasaliti Watanzania

Wewe ni mpuuzi, unayefaa kupuuzwa.
Useless bitch!

Lissu amekwambia anataka uhuru wake kwa kutumia damu ya waTanzania? Hivi kichwani zinakutosha kweli wewe?

Nilitaka nikuache uendelee na upumbavu wako; lakini sasa nimeamua kuwa nawe.
Acha matusi na ujibu hoja. Hapa nazungumzia kauli ya Lissu mwenyewe kupitia kwa wakili wake, Kisabo: ‘kesi zote zinazomkabili yeye na chama zifutwe… na kwamba yuko tayari kwa mazungumzo.’ Sentensi hii inaacha maswali mengi na, kwa mtazamo wangu, inaashiria uwezekano wa usaliti. Ninamuheshimu Tundu Lissu, lakini sina imani kamili na wanasiasa. Endapo atajaribu kutumia muktadha uliopo kwa maslahi yake ya kisiasa, tutamkosoa vikali, kama tulivyofanya kwa Mbowe.

1000393919.jpg
 
Acha matusi na ujibu hoja. Hapa nazungumzia kauli ya Lissu mwenyewe kupitia kwa wakili wake, Kisabo: ‘kesi zote zinazomkabili yeye na chama zifutwe… na kwamba yuko tayari kwa mazungumzo.’ Sentensi hii inaacha maswali mengi na, kwa mtazamo wangu, inaashiria uwezekano wa usaliti. Ninamuheshimu Tundu Lissu, lakini sina imani kamili na wanasiasa. Endapo atajaribu kutumia muktadha uliopo kwa maslahi yake ya kisiasa, tutamkosoa vikali, kama tulivyofanya kwa Mbowe.

View attachment 3574614
Maana yake ni nini hii?

Wewe hujui kwamba kesi ya uhaini ni ni ya kutungwa? Hilo hulijui

Wala huna uelewa wowote kwamba kesi zote zinazokikabili chama ni kesi za kipuuzi tu; hili nalo hulijui?

Na wala humnna akili ya kukuonyesha kuwa pamoja na kesi kuwa FEKI; lakini bado uendeshaji wa kesi hizo nao ni wa kipuuzi?

Yote haya wewe huyajui?
 
Lissu anataka aachiwe huru kisha awe tayari kufanya mazungumzo. Hii ina maana gani? Je, tutampa uhuru kwa sharti la kufanya mazungumzo na sisi? Swali ni: anataka kufanya mazungumzo na nani hasa?
Tundu Lissu hajaomba kufanya mazungumzo. Swala la mazungumzo na maridhiano linawahusu wahalifu, ndio wanaolipigia kelele kila mara ili wajisafishe.

Kwa hiyo unapaswa kuwauliza hao unaowafanyia kazi hapa, wao wanataka hayo mazungumzo na maridhiano na nani; na kwa sababu zipi hasa?
 
Maana yake ni nini hii?

Wewe hujui kwamba kesi ya uhaini ni ni ya kutungwa? Hilo hulijui

Wala huna uelewa wowote kwamba kesi zote zinazokikabili chama ni kesi za kipuuzi tu; hili nalo hulijui?

Na wala humnna akili ya kukuonyesha kuwa pamoja na kesi kuwa FEKI; lakini bado uendeshaji wa kesi hizo nao ni wa kipuuzi?

Yote haya wewe huyajui?
Hayo yote nayajua, lakini hoja ya kusema kwamba aachiwe huru kisha awe tayari kwa mazungumzo inaacha maswali mengi na inaonekana kama inaashiria usaliti. Inamaanisha kuwa uhuru wake unatolewa kwa masharti kutoka kwa wanaodaiwa kuwa wahalifu, yaani ‘tutakuacha huru halafu tuongee.’ Swali ni: anazungumza na nani hasa, na mazungumzo hayo yanahusu nini? Je, anataka kufanya mazungumzo na watu wanaotuhumiwa kwa mauaji?.
 
Tundu Lissu hajaomba kufanya mazungumzo. Swala la mazungumzo na maridhiano linawahusu wahalifu, ndio wanaolipigia kelele kila mara ili wajisafishe.

Kwa hiyo unapaswa kuwauliza hao unaowafanyia kazi hapa, wao wanataka hayo mazungumzo na maridhiano na nani; na kwa sababu zipi hasa?
Hii statement ni ya nani Lissu au Samia!? "........na kwamba yuko tayari kwa mazungumzo."
 
Iwapo jambo hili ni kweli, basi ni wazi kwamba CHADEMA imewasaliti Watanzania.
View attachment 3574549ma
Watu ambao hawapo jela hawana haki ya kuwaita watu walio jela wasaliti.

Labda ikiwa mtu A aliye jela akapewa nafasi ya kutoka kwa masharti, akakataa, halafu mtu B aliye jela akapewa masharti hayohayo ya kutoka, akakubali, hapo mtu A anaweza kumuita mtu B msaliti.

Lakini wewe mtu uko nje unamuita mtu aliyefungwa jela msaliti hata haya huoni?

Pia, mtu kusema yuko tayari kufanya mazungumzo kuna usaliti gani hapo wakati kukubali mazungumzo si kukubali jambo lokote zaidi ya mazungumzo?

Mnajuaje kwenye mazungumzo Lissu atasemaje?

Mnajuaje kwenye mazungumzo Lissu hawezi kuwabana vizuri?
 
Unafanya mazungumzo na wahalifu!?
Kuna mahali popote alipotaja anafanya mazungumzo na nani; au hizi ni akili zako zinazokufanya kutunga mambo ya kufikirika ndiyo yawe mawazo ya Tundu Lissu?

Unahangaika hapa na mada isiyokuwa na kichwa wala miguu; kwa kufikiri tu na kuweka maana yako katika hayo aliyosema Tundu Lissu?

Unataka tuchukulie uelewa wako mbovu ndio uwe tafsiri ya aliyosema Lissu?
 
Hayo yote nayajua, lakini hoja ya kusema kwamba aachiwe huru kisha awe tayari kwa mazungumzo inaacha maswali mengi na inaonekana kama inaashiria usaliti. Inamaanisha kuwa uhuru wake unatolewa kwa masharti kutoka kwa wanaodaiwa kuwa wahalifu, yaani ‘tutakuacha huru halafu tuongee.’ Swali ni: anazungumza na nani hasa, na mazungumzo hayo yanahusu nini? Je, anataka kufanya mazungumzo na watu wanaotuhumiwa kwa mauaji?.
Sasa kama wewe unayo maswali hayo uliyouliza hapa, unaanzia wapi kumpa sifa ya usaliti wakati huna majibu juu ya hayo maswali unayouliza wewe?

Kama unajuwa Kesi zinazomkabili Tundu Lissu na CHADEMA ni za kutungwa tu; kwa ni ni sasa uone ajabu yeye akisema aachiwe huru?
Mbona unajichanganya kiasi hiki!
 
Lissu anataka aachiwe huru kisha awe tayari kufanya mazungumzo. Hii ina maana gani? Je, tutampa uhuru kwa sharti la kufanya mazungumzo na sisi? Swali ni: anataka kufanya mazungumzo na nani hasa?
Sasa afanye nini unataka? Maybe una idea nzuri, tell us about it
 
Hii statement ni ya nani Lissu au Samia!? "........na kwamba yuko tayari kwa mazungumzo."
Kwani hujui anayetaka mazungumzo ya maridhiano ni nani?

Umemuuliza Lissu hayo mazungumzo anayoyataja ni hayo hayo anayofikiri Samia?.

Utaleta vipi mada hapa wakati hata hujui kinachosemwa na huyo unayemzushia usaliti?
 
Mkuu Lisu huyo asingekuwa bahati yake basi ni zaidi ya oct29. Jamaa bado anatembea na risasi mwilini. Tukio la oct29 Lisu lilishampata nyuma zaidi na bado karudi anapambania hadi kesi ya uhaini kapewa. Unataka afanye nini? Unamdai nini? Sidhani kma majeruhi waliopigwa risasi oct29 wanaweza kurudi kupambana tena kma TL alivyofanya. Lisu aliweza kuacha hizi mambo na shavu likawa dodo zaidi. Usimlaumu mtu alikuwa jela yeye na makamu wake ni wamesimuliwa tu kilichotokea.
Mapamano yaendeleee hakuna kurudi nyuma,kuwe kumetulia tu kwa muda, tunaamsha tena
 
Wewe uliingia? Mambo huwa yanaenda kwa hatua, nadhani ni muda jamaa apumzike awe anatoa ushauri. Huenda wewe au mwingine umefika muda wako wa kwenda kufikisha hayo makwazo. Sio lazima hata uwe mwanasiasa, unaweza kufanya kwa namna yako. Andika hata vitabu, tengeneza content n.k
Mimi ni mmoja wa watu wa mwanzo kabisa kuona vifo ndio maana nipo hai, nimepoteza ndugu na marafiki, huo muda umefika lini? Nilishakuwepo.
 
Nakubaliana nawe kabisa kwamba Lissu ni shujaa katika harakati za kupigania haki na demokrasia nchini Tanzania. Hata hivyo, hatua anayopanga kuchukua inaweza kuathiri sifa na heshima yake. Aidha, tukumbuke kuwa Watanzania wengi wamepoteza maisha wakipigania haki katika nchi hii; hivyo si vyema kutumia vifo vyao kwa manufaa ya kisiasa. Nina imani kwamba hatafanya hivyo
Let's not jump into conclusion, tusubiri muda ndiyo utaongea.
 
Watanzania hawakuandamana kwa ajili ya CHADEMA au chama chochote cha siasa, mazungumzo siyo kwa ajili ya CHADEMA.
Sasa kwanini CCM wanaishinikiza CHADEMA kwenye meza ya reconciliations? Kibaya zaidi hata hivyo vyama vingine wala hawavizungumzii kwenye hayo maridhiano yao.
 
Back
Top Bottom