Mkuu, hadi sasa kuna mpasuko mkubwa ndani ya muungano, usiuongeze hapa tafadhali. Wapenzi wa Yanga wanaipenda Yanga si kwa sababu ni ya Bara, inapendwa kwa sababu ni Yanga, hata leo kuna Wazanzibar walikuwa upande wa Yanga.
Angalia kesho Azam atakavyopata sapoti ya wana Jangwani eti amuue Mnayama, suala ambalo halipendezi.
Mimi ni Yanga, hakuna timu naichukia kama Azam, nawaomba wana Yanga wenzangu kesho tuwe upande wa Mnyama hawa dogo wadharirike kadri iwezekanavyo. Azam ndiyo adui namba 1 wa Yanga, hawa ndiyo walitunyima ubingwa wa Bara, hawa hawa ndiyo walisababisha wachezaji wetu kibao kufungiwa, hawa hawa walipochukua kombe la mapinduzi wakaanza kuwabeza Yanga na Simba; jamani Simba siyo adui wa Yanga ni mtani tu tena tangu zamani.
Wakimtoa Mnyama wataanza, ooh! bado Yanga huku tutakuwa tumewapa sapoti. Chonde chonde jamani, tuwatose Azam, kama Yanga atashindwa kuchukua ubingwa heri Bingwa awe Simba kuliko Azam.
KESHO IWE NI SIKU YA KISASI, AZAM WATOKE KWENYE MASHINDANO HAYA KWANZA HAWANA JIPYA, NI WAZUSHI TU.