Rashda Zunde
JF-Expert Member
- May 28, 2022
- 291
- 281
Leo tarehe 26 Julai 2025, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimefanya Mkutano Mkuu wake wa Taifa kwa njia ya mtandao, kikihusisha takriban wajumbe 2,000 kutoka maeneo mbalimbali ya nchi. Taarifa kutoka ndani ya chama zinadai kuwa huu ni mkutano wa kwanza barani Afrika wa aina hiyo kufanywa kwa njia ya kidijitali kwa mafanikio.
Mkutano huo umeongozwa na Mwenyekiti wa CCM ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Tukio hili linatajwa kuwa ni utekelezaji wa hatua za kidijitali ambazo zimekuwa zikipigiwa chapuo katika ngazi ya kimataifa, hususan kupitia itifaki za Umoja wa Mataifa kuhusu ushirikiano wa kidijitali.
Kwa waliokuwa wakifuatilia maendeleo ya TEHAMA nchini, tukio hili si la kushangaza. Katika kipindi cha miaka michache iliyopita, kumekuwa na ongezeko kubwa la:
Mkutano huo umeongozwa na Mwenyekiti wa CCM ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Tukio hili linatajwa kuwa ni utekelezaji wa hatua za kidijitali ambazo zimekuwa zikipigiwa chapuo katika ngazi ya kimataifa, hususan kupitia itifaki za Umoja wa Mataifa kuhusu ushirikiano wa kidijitali.
Kwa waliokuwa wakifuatilia maendeleo ya TEHAMA nchini, tukio hili si la kushangaza. Katika kipindi cha miaka michache iliyopita, kumekuwa na ongezeko kubwa la:
- Matumizi ya huduma za kifedha kupitia simu (mobile money)
- Upatikanaji wa intaneti hadi maeneo ya vijijini
- Huduma za serikali kupitia mifumo ya mtandao (e-government)
- Uwekezaji kwenye startups na vituo vya ubunifu (innovation hubs)