CCM YAPITA KATA YA LANGILO RUVUMA bila kupingwa!

CCM YAPITA KATA YA LANGILO RUVUMA bila kupingwa!

Hivyo vyama vingine havijajinasibu kuchukua nchi 2015; anyways naona jamaa hawana haja na kata wao watakomaa tu na Ikulu mbona hata hiyo nayo ni poa sana kwani kwenye kata kuna ulaji gani

Nchi ya Langilo?
 
Leo ni jumapili; uwe mkweli katika kata ya mianzini CHADEMA hampo makini, hata mgombea mmeokota barabarani ni mtu asiye na hekima, busara wala sifa za uongozi. Haishangazi CHADEMA kuwa na wagombea wasio makini kwa vile viomgozi wenu katika ngazi za chini ni wababaishaji ambao wana historia chafu ndani ya jamii inayowazunguka, HIVYO hawachaguliki

Mafalili, kiongozi nakushukuru kwa taarifa, ila naomba ujue kwamba Mgombea wetu bwana Gozbert ana uwezo zaidi yako, kijana huyu kwa sasa anafanya degree yake ya pili pale Mlimani tena ya sheria, amini usiamini kijana anakuzidi uwezo wa fikra hata kujenga hoja, na kwa kuwa leo mnazindua kampeni na huyo mgombea wenu bw. Athuman..... si umesikia ameanza kupia Mi...k..n, baada ya kujenga hoja anataka huruma. Kiongozi Mafalili kuna kitu CCM mmekipoteza, hamsemi mnaenda kuwafanyia nini watanzania, bali kilio chenu kwa sasa ni Chadema na hapo ndipo mnapoitangaza chadema bila nyie kujua,
 
Katika medani ya ushushu, kauli za wendawazimu au walevi mbwa, ni za muhimu kuliko za maprofesa. Mara nyingi walevi hutoa yale ya ukweli yaliyojaza nyoyo zao tofauti na wanapokuwa wazima katika fahamu zao kamili.

Hivyo, kama ni kweli chama hakijasimamisha mgombea kwenye kata husika, badala ya kumshambulia mleta mada, chukulieni maneno yake kama changamoto na sio kumbeza au kumtukana kwani kufanya hivyo kwa mlevi haisaidii! Maono ya chama ni kwenda hadi ngazi ya chini kabisa ya familia, how comes, kinashindwa kusimamisha mgombea katika ngazi ya juu kama kata?

Kama kimeshindwa kufanya hivyo kwa hivi vi-kata vichache 26; kitaweza kufurukuta katika Uchaguzi Mkuu 2015 ambao utahusisha mamia ya kata na changamoto kibao? Acheni mbwembwe na tambo zisizo na mashiko, fanyieni kazi maneno ya mwendawazimu hata kama aliyeyatoa ni punguani lakini ukweli ni ukweli tu hata kama umetolewa na Shetani.

CC: Tumaini Makene, Dr W. Slaa, Molemo, Ben Saanane, John Mnyika, Tundu Lissu, Mwita Maranya, Michael Aweda

Hakuna mtu anayesema kwamba alichosema Nape hapa sio ukweli. Hilo la kutokuweka mgombea tunalijua na tunadili nalo kichama. Tumetoka mbali na tunamove strategically.

Hapa tunamshangaa Nape kukurupuka asubuhi na taulo kuja kuandika kuhusu CHADEMA, wakati kuna mambo lukuki ya kueneza kuhusu chama chake...
 
Wakuu

Kwanza tunashukuru sana kuwa Msemaji wa CCM, amethibtisha mwenyewe hofu inayotokana na kutokuwa na uhakika wa ushindi kila wanapokutana na CHADEMA katika uchaguzi wowote, eneo lolote, mjini na vijijini.

Kilichotokea ni mtindo wa CCM ambao bila shaka yoyote utafikishwa mwisho muda si mrefu, kwa kasi ya mabadiliko na uasi mkubwa dhidi ya CCM unavyozidi kuongezeka.

Wamemtisha aliyekuwa mgombea wa CHADEMA hadi ameshindwa kurudisha fomu. Kwa sababu tu baba yake na mgombea huyo ni mwanachama wa CCM. Ni staili ile ile ambayo CCM chini ya au kwa maelekezo ya Makamba wametisha wagombea na hata viongozi halali wa wananchi wanaotokana na CHADEMA huko Lushoto.

Kwa taarifa za uhakika tulizonazo ni kwamba CHADEMA na mgombea wake, wanakubalika sana katika kata ya Langido, CCM wakamfuata baba yake ambaye ni mwanachama wao, wakamwambia iwapo atamruhusu mtoto wake aendelee kugombea kisha ashinde uchaguzi huo, watamfungulia kesi ambayo hatatoka. Walisema watamhusisha na vurugu fulani zilizotokea hivi karibuni ambapo wananchi walipinga uchakachuaji uliofanyika kwenye uchaguzi wa mabaraza ya katiba.

Wakaenda mbali kuiambia familia nzima haitakuwa salama. Hivyo wajiandae kwa umaskini, kwa yale watakayofanyiwa.

Ni mambo yale yale yaliyofanyika pia kule Ruaha, ambako Kanali Kinana baada ya kuulizwa swali kuhusu tuhuma za tembo, yeye na msafara wake wakavunja mkutano haraka na kukimbia, wakiwatuhumu wanakijiji kuwa wametumwa na CHADEMA.
Matokeo yake CCM wametumia nguvu kubwa, ikiwemo kumbambikia kesi aliyekuwa mgombea kijiji hicho kwa tiketi ya CHADEMA na hadi sasa yuko gerezani.

Wananchi walipomjazia fomu na kuirejesha kwa msimamizi wa uchaguzi, CCM wakaogopa aibu ya kushindwa na mtu aliye gerezani (kama ilivyotokea Tarime), wakaelekeza isikubaliwe. Hadi leo wananchi wamemkataa mtu wa CCM aliyepitishwa kwa mabavu bila kupingwa.

Ofisi ya Katibu Mkuu, kupitia Kurugenzi ya Kampeni na Uchaguzi, imeshatoa maelekezo kwa hatua za haraka kuchukuliwa.

Ni kata hiyo moja pekee kati ya 26, ambako hadi sasa CHADEMA haina mgombea.

Makene

0688 595831/ 0752 691569
 
Katika hali inayodhihirisha kuwa Chadema wana kufa kwa kasi ya ajabu, wamefikia mahali pa kushindwa kuwa na mgombea wa Udiwani kata ya Langido mkoani Ruvuma kiasi cha kuifanya CCM ipite bila kupingwa na hivyo kuanza na kata moja tayari kati ya kata 26 zinazofanya uchaguzi mdogo.

kama watani hata kusimamisha mgombea tu kwenu inakuwa tabu tena wa kata kweli mko serious kutaka kuaminiwa kukabidhiwa nchi? Hili limenifanya nikumbuke maeneo kibao mwaka 2010 ambayo majimbo na kata hamkusimamisha agombea au mliwatelekeza pale mliposimamisha! Na sasa nasikia nguvu kubwa mnapeleka Arusha!!!!! Mwenye akili na atafisiri hili!

Itawachukua muda kidogo kukomaa!

Nepi nini mawazo yako kuhusiana na hoja ya Mdee dhidi ya Chenge kuhusu mikataba mibovu Serikali iliyoingia chini ya maelekezo yake kama Mwanasheria mkuu wa Serikali?Nini msimamo wako juu ya hili?Tuache Siasa za mipasho na za kitoto badala yake tujadili mambo muhimu na mazito ya Kitaifa mara moja moja sio mbaya.
 
Mkuu Tumaini Makene asante kwa taarifa. Kwa maana hiyo mleta mada anajua haya yote na kwake yeye alikuwa anajua ni sehemu ya kuwaumiza Chadema na ndo maana kalileta hapa mapema likiambatana na madongo kwa Chadema.
 
Last edited by a moderator:
Kama unafikiri chadema itakufa umelewa chang'aa, utakufa wewe na ccm yako kabla hata ya chadema . UMeshasema kata zipo 26,subiria uone kata zingine.!!!!!!!!!!!Wenzio jana wameanza kutaka kujitoa huko Arusha na kule Ifakara. NA siasa zenu za kupita bila kupigwa si ndizo zinazowaponza hata kule ruaha!!!!!!!Najua wewe ni mtoto wa nje cup wa mshikaji lazima umsemee sana Nape:nod: Nchi yenu ipi mnayoijenga? baraka ya kupakazia watu ugaidi,kurekebisha matokeo ya mitihani mliowaferisha wenyewe,baraka ya kuongeza deni la taifa kila kukicha,baraka ya kumfanya RIZ bilionea wa mabilionea wote,baraka ya kuchukua ardhi yote ya watanzania,baraka ya kuwa nchi ya 3 ombaomba sugu duniani,baraka ya kusafirisha twiga warefu kama nini kwenye mitege ulaya na uarabuni na subirini tu muone baada ya miaka kumi hakuna mtalii atakayekuja tanzania
Kuna maeneo ukitaja chadema,waweza pigwa kama mbwa mwizi,hawataki hata kuisikia.
 
Nape usishangilie ujinga,usidhani watu wote ni wajinga siku zote,kinachofanywa na CCM sio cha kushagilia,hiyo sio democrasia,kufurahia kuiua Democrasia ni uhaini huitakii mema CCM wala Tanzania,kilichotekea ni mbinu chafu za CCM zikichangiwa na umasikini na kukosa elimu ya Uraia,Kijana aliyeandaliwa CCM ikamtishia kumwua,aliyepatikana dakika za majeruhi naye akafanya uzembe nadhani kwa kujua anachokifanya form zake hazikukamilishwa vizuri,kunataalifa za CCM kuwanunua viongozi wa CHADEMA wilaya lkn mbinu zote hizi zinafahamika na mwishop hazitafanya kazi tena.




Katika hali inayodhihirisha kuwa Chadema wana kufa kwa kasi ya ajabu, wamefikia mahali pa kushindwa kuwa na mgombea wa Udiwani kata ya Langido mkoani Ruvuma kiasi cha kuifanya CCM ipite bila kupingwa na hivyo kuanza na kata moja tayari kati ya kata 26 zinazofanya uchaguzi mdogo.

kama watani hata kusimamisha mgombea tu kwenu inakuwa tabu tena wa kata kweli mko serious kutaka kuaminiwa kukabidhiwa nchi? Hili limenifanya nikumbuke maeneo kibao mwaka 2010 ambayo majimbo na kata hamkusimamisha agombea au mliwatelekeza pale mliposimamisha! Na sasa nasikia nguvu kubwa mnapeleka Arusha!!!!! Mwenye akili na atafisiri hili!

Itawachukua muda kidogo kukomaa!
 
Katika hali inayodhihirisha kuwa Chadema wana kufa kwa kasi ya ajabu, wamefikia mahali pa kushindwa kuwa na mgombea wa Udiwani kata ya Langido mkoani Ruvuma kiasi cha kuifanya CCM ipite bila kupingwa na hivyo kuanza na kata moja tayari kati ya kata 26 zinazofanya uchaguzi mdogo.

kama watani hata kusimamisha mgombea tu kwenu inakuwa tabu tena wa kata kweli mko serious kutaka kuaminiwa kukabidhiwa nchi? Hili limenifanya nikumbuke maeneo kibao mwaka 2010 ambayo majimbo na kata hamkusimamisha agombea au mliwatelekeza pale mliposimamisha! Na sasa nasikia nguvu kubwa mnapeleka Arusha!!!!! Mwenye akili na atafisiri hili!

Itawachukua muda kidogo kukomaa!

Nape: Thread kama hii inastahili kuletwa hapa na mwandishi wa gazeti la Uhuru au Mzalendo na siyo Katibu Mwenezi wa CCM!!! Mbona unahangaika sana na CDM kila kukicha, mbona viti mnavyo poteza huwa huzungumzii?
You need to grow up and know your responsibility, otherwise unaipeleka CCM pabaya, unapoteza credibility na mwishowe utakuja kuondolewa kwenye nafasi hiyo kama mbwa mwizi!!!
 
Hata hivyo mumshukuru Nape Nnauye anawakumbusha. Pili kwa upeo wangu ameona kuwa CHADEMA ni chama pekee kwa Tanzania kinachowapa changamoto za kutosha. Atleast kwa sasa una wa accredit wapinzani wenu wakuu (CHADEMA) Hongera Nape Nnauye. Hivi ndivyo unavyotakiwa kuishi na wenzio wa upinzani ktk kufuatilia maslahi ya kweli.
 
Last edited by a moderator:
Amekijenga? Sasa inakuaje hata mgombea wa ngazi ya kata mmeshindwa kumuweka?

Alichokifanya mwezi wa kwanza ma minyororo kule bumbuli inahitati kamusi ndio uelewe au? Lakini usijali mpwa wangu hawa kunguni ni wa msimu tu.
 
Wakuu

Kwanza tunashukuru sana kuwa Msemaji wa CCM, amethibtisha mwenyewe hofu inayotokana na kutokuwa na uhakika wa ushindi kila wanapokutana na CHADEMA katika uchaguzi wowote, eneo lolote, mjini na vijijini.

Kilichotokea ni mtindo wa CCM ambao bila shaka yoyote utafikishwa mwisho muda si mrefu, kwa kasi ya mabadiliko na uasi mkubwa dhidi ya CCM unavyozidi kuongezeka.

Wamemtisha aliyekuwa mgombea wa CHADEMA hadi ameshindwa kurudisha fomu. Kwa sababu tu baba yake na mgombea huyo ni mwanachama wa CCM. Ni staili ile ile ambayo CCM chini ya au kwa maelekezo ya Makamba wametisha wagombea na hata viongozi halali wa wananchi wanaotokana na CHADEMA huko Lushoto.

Kwa taarifa za uhakika tulizonazo ni kwamba CHADEMA na mgombea wake, wanakubalika sana katika kata ya Langido, CCM wakamfuata baba yake ambaye ni mwanachama wao, wakamwambia iwapo atamruhusu mtoto wake aendelee kugombea kisha ashinde uchaguzi huo, watamfungulia kesi ambayo hatatoka. Walisema watamhusisha na vurugu fulani zilizotokea hivi karibuni ambapo wananchi walipinga uchakachuaji uliofanyika kwenye uchaguzi wa mabaraza ya katiba.

Wakaenda mbali kuiambia familia nzima haitakuwa salama. Hivyo wajiandae kwa umaskini, kwa yale watakayofanyiwa.

Ni mambo yale yale yaliyofanyika pia kule Ruaha, ambako Kanali Kinana baada ya kuulizwa swali kuhusu tuhuma za tembo, yeye na msafara wake wakavunja mkutano haraka na kukimbia, wakiwatuhumu wanakijiji kuwa wametumwa na CHADEMA.
Matokeo yake CCM wametumia nguvu kubwa, ikiwemo kumbambikia kesi aliyekuwa mgombea kijiji hicho kwa tiketi ya CHADEMA na hadi sasa yuko gerezani.

Wananchi walipomjazia fomu na kuirejesha kwa msimamizi wa uchaguzi, CCM wakaogopa aibu ya kushindwa na mtu aliye gerezani (kama ilivyotokea Tarime), wakaelekeza isikubaliwe. Hadi leo wananchi wamemkataa mtu wa CCM aliyepitishwa kwa mabavu bila kupingwa.

Ofisi ya Katibu Mkuu, kupitia Kurugenzi ya Kampeni na Uchaguzi, imeshatoa maelekezo kwa hatua za haraka kuchukuliwa.

Ni kata hiyo moja pekee kati ya 26, ambako hadi sasa CHADEMA haina mgombea.

Makene

0688 595831/ 0752 691569
Asante sana kwa taarifa japokuwa imechelewa kidogo kwa sisi wapenzi wa Chadema humu mtandaoni. Lakini kuna mambo kadhaa ya kuuliza na kushauri.
1/Katika hili kuna namna yoyote kisheria kureverse situation?

2/Kwanini CHADEMA ikaligundua hili baada ya muda wa mwisho wa kurudisha form na sio kabla?

3/Mwanachama akishateuliwa na CHADEMA anakuwa ni mgombea wa chama na sio binafsi, ni vipi hili mkaruhusu mtu binafsi akajiamulia kutorudisha fomu na chama kikakaa kimya?

4/Hila kama hizi zimeshatokea mara nyingi na zitaendelea kutokea sana mpaka kufikia 2015, CHADEMA imejiandaaje katika hili kuanzia nafasi ya Kijiji, kitongoji, kata, Ubunge na Urais?

5/Je CHADEMA haina utaratibu wowote wa kuwa na reserve ya watu wa kugombea kama itatokea aliyeteuliwa kalaghaiwa kabla ya muda wa mwisho wa kurudisha fomu?

6/Sasa CHADEMA imejiandaa vipi na wagombea watakaojitoa(Kwa kuwa wamehongwa au kutishwa na CCM) wakati yatari wameshapitishwa na tume ya Uchaguzi?

7/Chadema imejipanga vipi na hila kama za 'Chitambala 2009' za mgombea kuondolewa kwenye Uchaguzi kwa sababu tu kuna makosa ya kisheria kwenye form za kugombea?
 
Kuna maeneo ukitaja chadema,waweza pigwa kama mbwa mwizi,hawataki hata kuisikia.
Acha uongo na Uzushi.
Wapi hapa Tanzania kuna kitu hicho?
Ninachokifahamu huwezi ukajitambulisha kama mwanaCCM na ukapata huduma yoyote nzuri hapa Arusha mjini.
 
Mkuu Nape, usijiangaishe na CHADEMA hawa tuachie sisi kwani tuna wamudu, mbona wepesi tu hawa, kuna wazalendo kama Ritz, ZeMarcopolo, HAMY-D, CHAMVIGA, Rejao na wengine wengi tu wanatoa elimu ya uraia humu JF.

Wewe jikite na kuimarisha itikadi ya chama taifa, kwani tangu Dr Slaa alivyo toka nduki kufanya majadiliano pale ITV kichwa chake hakitulii kabisa, ushahidi ni kwa wale walio kuwa Babati.
 
Last edited by a moderator:
chadema ikifa ili iweje uendelee na mambo yenu yale ya bungeni ndiooooo....miaka 50 bado tunazunumzia maji hakuna wakai miti na maziwa makuu tunayo acha hizo bana angalia ndugu zako wanavyoteseka dawa hakuna,form one hawajui kusoma wala kuandika ustuleteee hizo banaaaaaaaa.........
ile kasi yako kuzunguka nchi nzima ya kuwaondoa mafisadi imeshia wapi?
 
Wakuu

Kwanza tunashukuru sana kuwa Msemaji wa CCM, amethibtisha mwenyewe hofu inayotokana na kutokuwa na uhakika wa ushindi kila wanapokutana na CHADEMA katika uchaguzi wowote, eneo lolote, mjini na vijijini.

Kilichotokea ni mtindo wa CCM ambao bila shaka yoyote utafikishwa mwisho muda si mrefu, kwa kasi ya mabadiliko na uasi mkubwa dhidi ya CCM unavyozidi kuongezeka.

Wamemtisha aliyekuwa mgombea wa CHADEMA hadi ameshindwa kurudisha fomu. Kwa sababu tu baba yake na mgombea huyo ni mwanachama wa CCM. Ni staili ile ile ambayo CCM chini ya au kwa maelekezo ya Makamba wametisha wagombea na hata viongozi halali wa wananchi wanaotokana na CHADEMA huko Lushoto.

Kwa taarifa za uhakika tulizonazo ni kwamba CHADEMA na mgombea wake, wanakubalika sana katika kata ya Langido, CCM wakamfuata baba yake ambaye ni mwanachama wao, wakamwambia iwapo atamruhusu mtoto wake aendelee kugombea kisha ashinde uchaguzi huo, watamfungulia kesi ambayo hatatoka. Walisema watamhusisha na vurugu fulani zilizotokea hivi karibuni ambapo wananchi walipinga uchakachuaji uliofanyika kwenye uchaguzi wa mabaraza ya katiba.

Wakaenda mbali kuiambia familia nzima haitakuwa salama. Hivyo wajiandae kwa umaskini, kwa yale watakayofanyiwa.

Ni mambo yale yale yaliyofanyika pia kule Ruaha, ambako Kanali Kinana baada ya kuulizwa swali kuhusu tuhuma za tembo, yeye na msafara wake wakavunja mkutano haraka na kukimbia, wakiwatuhumu wanakijiji kuwa wametumwa na CHADEMA.
Matokeo yake CCM wametumia nguvu kubwa, ikiwemo kumbambikia kesi aliyekuwa mgombea kijiji hicho kwa tiketi ya CHADEMA na hadi sasa yuko gerezani.

Wananchi walipomjazia fomu na kuirejesha kwa msimamizi wa uchaguzi, CCM wakaogopa aibu ya kushindwa na mtu aliye gerezani (kama ilivyotokea Tarime), wakaelekeza isikubaliwe. Hadi leo wananchi wamemkataa mtu wa CCM aliyepitishwa kwa mabavu bila kupingwa.

Ofisi ya Katibu Mkuu, kupitia Kurugenzi ya Kampeni na Uchaguzi, imeshatoa maelekezo kwa hatua za haraka kuchukuliwa.

Ni kata hiyo moja pekee kati ya 26, ambako hadi sasa CHADEMA haina mgombea.

Makene

0688 595831/ 0752 691569

Makosa yote ya chadema wa kulaumiwa ni CCM.

Mnapompendeza mtu kugombea uongozi ina maana mmeridhika kuwa anaweza kuwa kiongozi mzuri. Je, ni nini chadema imefanya ili kupendekeza mgombea mzuri?

Hii yote ni ishara tosha kuwa chadema haina uwezo wa kushika dola, kwa sababu ni chama kisichoweza kubeba responsibility ya maamuzi yake...

Unazungumzia chadema kukosa mgombea lakini unaitaja CCM mara nyingi zaidi kuliko chadema!!!
 
Mimi nasubiri kauli ya viongozi wa chedema kwanza kwa nini kata hiyo hawakuweka mgombea from their statement nitachangia na kujenga hoja mimi simuamini Nape, ni vuvuzela tu hilo!!
 
ba hana muda atakufa.kiona simba anashangaa kukuta mzoga bila mwenyewe jua huyo sima
 
Katika hali inayodhihirisha kuwa Chadema wana kufa kwa kasi ya ajabu, wamefikia mahali pa kushindwa kuwa na mgombea wa Udiwani kata ya Langido mkoani Ruvuma kiasi cha kuifanya CCM ipite bila kupingwa na hivyo kuanza na kata moja tayari kati ya kata 26 zinazofanya uchaguzi mdogo.

kama watani hata kusimamisha mgombea tu kwenu inakuwa tabu tena wa kata kweli mko serious kutaka kuaminiwa kukabidhiwa nchi? Hili limenifanya nikumbuke maeneo kibao mwaka 2010 ambayo majimbo na kata hamkusimamisha agombea au mliwatelekeza pale mliposimamisha! Na sasa nasikia nguvu kubwa mnapeleka Arusha!!!!! Mwenye akili na atafisiri hili!

Itawachukua muda kidogo kukomaa!

Kwani wanaokabidhiwa nchi wanamapembe? nyie mbona mmkabidhiwa nchi imewashinda? wewe nawe kwa kuwa tu baba yako naye alikuwa kiongozi ndo ushukuru hivyo lakini si kwa uwezo wako mwenyewe. Huna uwezo wowote, wewe ni tofauti na kina Myika, Zito ambao ni kwa akili zao na uwezo wao. lakini wewe huwezi kutuambia lolote. Yahani uko hapa unafurahia hata kushinda udiwani? Mbona tukipita huko kufanya mikutano mnasema wachochezi na waleta vurugu? Kumbe lengo lenu msipingwe. Hamuuwezi ushindani nyie na wewe ushukuru baba yako alikuwa kiongozi la sivyo ungekuwa unachuuza korosho kule kwenu.
 
Back
Top Bottom