CCM YAPITA KATA YA LANGILO RUVUMA bila kupingwa!

CCM YAPITA KATA YA LANGILO RUVUMA bila kupingwa!

Hapa si kumbeza Nape ,swali ni kwa nn hatuna mgombea kwenye hiyo kata,hatuwezi kuendelea kujifariji kwa uzembe wa namna hii na baadae tuanze kutafuta sababu,ikumbukwe chama kimepuuzia matokeo ya awali (kushindwa) kwa wanachama wetu kwenye uchaguzi wa mabaraza ya katiba,kwa mtu yeyote mkweli na anayefikiria kwa kina uchaguzi ule ulikuwa kipimo cha uchaguzi wa serikali za mitaa 2014 na tulichovuna ndicho hicho tutakachovuna hapo mwakani iwapo juhudi za makusudi hazitachukuliwa.Rai yangu Chadema ihimize uchaguzi wa ndani ya chama watu wenye moyo wa kufanya kazi wapatikane na tuachane na hawa wanaofanya kazi kwa mazoea.J2 njema.

Naunga mkono hoja huu ni upuzi usio kubalika waje hapa waseme kwanini hawajasimamisha mtu. Unless watuambie mgombea amenunuliwa na kuna hila hapo tutawaelewa na hata hiyo haitoshi kwani kwa vyovyote hila zina julikana sasa inakuwaje hawajajiandaa kwa hizi hila?
 
Chadema, Chadema, Chadema... Nape we ni muenezi wa CCM.. Why should all your speeches start with Chadema? Kuna vyama vingine 18 ambavyo vilikuwa na mandate ya kuweka mgombea huko... Lakini asubuhi yote hii umekurupuka kitandani kuja kuandika kuhusu CDM. Kweli wamekushika pabaya...
Hivyo vyama vingine havijajinasibu kuchukua nchi 2015; anyways naona jamaa hawana haja na kata wao watakomaa tu na Ikulu mbona hata hiyo nayo ni poa sana kwani kwenye kata kuna ulaji gani
 
Katika hali inayodhihirisha Nape Nauye anaiogopa sana chadema nikutokufikiria kuwa Tanzania kunavyama vingine vya upinzani....mkuu NCCR hauijui? au CUF umeisahau? Vipi kuhusu TLP? Na kile chama chenye bendera nyingi kuliko idadi ya wanachama (ADC) haukitambui? au hivi vyote havijaweka wagombea? Kama havijaweka wagombea mbona hauvisemi?.....bwana mdogo Nape kitu kikubwa ambacho mwenyezi Mungu ametunyima binadamu nikutokuijua kesho yetu suala linalotufanya tuamini kwamba nchi hii itakuwa chini ya ccm milele....Naomba nikutakie jumapili njema!
 
Ngoja "Vibaraka wenu", tume ya uchaguzi wawaandikishe damu hii iliyo na kiu ya kuwang'oa ndipo Nape uje na Kabaang yako hapa! Labda muwaambie wasifanye usajiri tena kwenye daftali la wapiga kura kama mlivyowaambia wasiitishe uchaguzi kwenye kata aliyoiacha Mawazo kule Arusha.
 
Naunga mkono hoja huu ni upuzi usio kubalika waje hapa waseme kwanini hawajasimamisha mtu. Unless watuambie mgombea amenunuliwa na kuna hila hapo tutawaelewa na hata hiyo haitoshi kwani kwa vyovyote hila zina julikana sasa inakuwaje hawajajiandaa kwa hizi hila?
Kuna hali ya kuridhika na kujiaminisha kuwa shughuli ya ukombozi tayari imetimia na kusahau kuwa kilichowadia ni saa ya ukombozi! Bado kuna milima na mabonde nani atakuwa tayari kwenda jela baada ya kuachia madaraka kirahisi hivyo? Nani atakubali kufilisiwa na kuishi kwenye umasikini anaousoma kwenye vitabu na kuangalia kwenye film? Ukweli ni kwamba akina Ridhiwan na Lowasa wapo tayari kutoa kila walichonacho na kuanza upya lakini wakiwa ndani ya mikono salama ya Chama cha Mapinduzi.Dr Slaa anajua vyema haya yote wasiwasi wangu ni hizi kurugenzi zinazomzunguka.
 
duh kweli magamba tumewakamata vibaya, jamaa halali akiiwaza chadema!
 
Hizo ni ishara za mwanzo tu na bado tutawanyamazisha mwaka huu.
 
CHADEMA UKIWATOA ZITTO,SLAA,MBOWE, TUNDU,MNYIKA,MDEE, UMEKIMALIZA KABISA. 2015 kitaanguka anguko 5a aibu sana.
 
Nampenda huyu Nepi ninayo kwa sababu amekijenga sana chama chetu CDM hivi mnadhan bila ya kuropoka ropoka huyu bui bui cc kama cc cdm tungekua wapi 4now? Yaan anakijenga chama chetu vere weli halafu anabomoa kwao akhsante permpas

Amekijenga? Sasa inakuaje hata mgombea wa ngazi ya kata mmeshindwa kumuweka?
 
Hapa si kumbeza Nape ,swali ni kwa nn hatuna mgombea kwenye hiyo kata,hatuwezi kuendelea kujifariji kwa uzembe wa namna hii na baadae tuanze kutafuta sababu,ikumbukwe chama kimepuuzia matokeo ya awali (kushindwa) kwa wanachama wetu kwenye uchaguzi wa mabaraza ya katiba,kwa mtu yeyote mkweli na anayefikiria kwa kina uchaguzi ule ulikuwa kipimo cha uchaguzi wa serikali za mitaa 2014 na tulichovuna ndicho hicho tutakachovuna hapo mwakani iwapo juhudi za makusudi hazitachukuliwa.Rai yangu Chadema ihimize uchaguzi wa ndani ya chama watu wenye moyo wa kufanya kazi wapatikane na tuachane na hawa wanaofanya kazi kwa mazoea.J2 njema.
Mkuu acha kuropoka ujinga hapa JF.
Kwanini unataka kuchanganya maji taka na maji safi kwenye chombo kimoja?

Kila mtu mdadisi anajua Chaguzi za mabaraza ya Katiba zilikuwa ni Uchafu mtupu.
Hata kama wagombea wa CHADEMA wangekuwa ni Mitume wa Mungu na wapiga kura wengi wangekuwa ni Malaika wa Mungu, bado CHADEMA ingeshindwa tu. Na ingeshindwa sio kwa sababu ya wingi wa kura bali kutokana na kanuni na mfumo wa uendeshaji wa chaguzi zile zilipangwa makusudi kabisa kuifanikisha CCM.

*Turudi kwenye mada, Swali je ni kweli CHADEMA wameshindwa kusimamisha mgombea huko Ruvuma, na kama ni Kweli kuna sababu gani ya msingi kushindwa kufanya hivyo?
Viongozi na Wasemaji wa CHADEMA tunataka watupe majibu hapa hapa JF tena sasa.
 
Halafu nimesikia mnawachombeza wazee wa watu kwa lazima kugombea w/viti wa vijiji hata ukitokea wametoa udhuru kuwa hawawezi soma au kuandika.
 
Mimi sishangzwi na hilo.

Kama mnakumbuka rasimu ya sera ya majimbo ya chadema aliyoileta Mnyika hapa JF mkoa wa Ruvuma ulisahauliwa. zanzibar na Tanga zikafanywa kuwa kitu kimoja kinachoitwa "Tanga na visiwa vyake"!!!!!!!!!

Tulipomuuliza alisema hiyo ni rasimu sifuri na kwamba rasimu kamili itakumbuka mikoa yote!

Kuusahau mkoa kwenye mipango ya chama sio dalili nzuri...
 
hamkawii kumtagazia polisi kama lile saga la morogoro
 
Mkuu acha kuropoka ujinga hapa JF.
Kwanini unataka kuchanganya maji taka na maji safi kwenye chombo kimoja?

Kila mtu mdadisi anajua Chaguzi za mabaraza ya Katiba zilikuwa ni Uchafu mtupu.
Hata kama wagombea wa CHADEMA wangekuwa ni Mitume wa Mungu na wapiga kura wengi wangekuwa ni Malaika wa Mungu, bado CHADEMA ingeshindwa tu. Na ingeshindwa sio kwa sababu ya wingi wa kura bali kutokana na kanuni na mfumo wa uendeshaji wa chaguzi zile zilipangwa makusudi kabisa kuifanikisha CCM.

*Turudi kwenye mada, Swali je ni kweli CHADEMA wameshindwa kusimamisha mgombea huko Ruvuma, na kama ni Kweli kuna sababu gani ya msingi kushindwa kufanya hivyo?
Viongozi na Wasemaji wa CHADEMA tunataka watupe majibu hapa hapa JF tena sasa.

Thats means mmeshakata tamaa kuingia ikulu kwa sababu ulizozitoa, poleni sana.
 
Kama kweli cdm wanaweka nguvu arusha pekeee basi hawana nia ya kweli kwa watanzania, inaweza kuwa YOTE DUGU MOJA

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Mkuu acha kuropoka ujinga hapa JF.
Kwanini unataka kuchanganya maji taka na maji safi kwenye chombo kimoja?

Kila mtu mdadisi anajua Chaguzi za mabaraza ya Katiba zilikuwa ni Uchafu mtupu.
Hata kama wagombea wa CHADEMA wangekuwa ni Mitume wa Mungu na wapiga kura wengi wangekuwa ni Malaika wa Mungu, bado CHADEMA ingeshindwa tu. Na ingeshindwa sio kwa sababu ya wingi wa kura bali kutokana na kanuni na mfumo wa uendeshaji wa chaguzi zile zilipangwa makusudi kabisa kuifanikisha CCM.

*Turudi kwenye mada, Swali je ni kweli CHADEMA wameshindwa kusimamisha mgombea huko Ruvuma, na kama ni Kweli kuna sababu gani ya msingi kushindwa kufanya hivyo?
Viongozi na Wasemaji wa CHADEMA tunataka watupe majibu hapa hapa JF tena sasa.
Mkuu,bahati mbaya sana siuelewi vizuri ushiriki wako ktk siasa zetu ,lakini nikukumbushe tu jambo moja juu ya uchaguzi wa mabaraza ya katiba ni ulikuwa ukiwashirikisha wananchi wa mtaa/kitongoji husika,sahau juu ya uchakachuzi uliochukuwa nafasi yake kwenye ngazi ya kata,kwetu sisi ambao huwa tunapenda kufanya utafiti hata kwa vitu vidogo vinavyotuzunguka ni kuwa wagombea wetu wengi ngazi hiyo chini kabisa walishindwa na sababu kubwa ni sisi kama chama hatukuwa tumejipanga vema.Kuhusu mada husika majibu ya aina yoyote toka kwa viongozi wetu hayawezi kusaidia lolote kumbuka kitendo cha kutoweka mgombea ni sawa nakujihukumu kifungo cha miaka 5 so haindoi wahusika kuwajibika.Uliwahi kusikia kisa cha mfalme Daudi baada ya kujichukulia mke wa mtwana wake? Pamoja na kujuta kwa kuyararua mavazi yake ya kifalme na kuvaa marapurapu ya magunia huku akijipaka majivu mwili mzima na kutoa toba kwa muumba wake bado hakukwepa adhabu ya Mungu.
 
tatizo la watu wa CCM wanapenda sana kujivika vyeo sio vyao
Kama hapa Rejao anamjibia Nape kwani wewe ndie msemaji wake?
usiwe sawa na wabunge wanaojivika uwaziri wawapo bungeni kujibu hoja za wenzao.
Swali langu mlengwa ni Nape au mleta mada na sio wana CCM wote tafadhali.
eti CCM ni washindi na wataendelea kuwa washindi daima, hapo mwajidanganya
msidhani 2015 mtaiba tena kura kama 2010.
Mataifa ya nje yanasuport CCM ili waweze kuiba zaidi rasilimali zetu.
hakuna Mtanzania alielala tena atakaekubali kuibiwa kura, patachimbika aisee
be informed.

Ametoa tu taarifa na siyo kutangaza ushindi. Ni jukumu lake kufanya hivyo. BTW, hata atangaze nani, hali halisi haibadiliki! CCM ni washindi, na wataendelea kuwa hivyo daima!
 
Hoja mufilisi kabisa, yaani wewe unataka kumhubiri Mungu bila kumtaja shetani?!!!! Injili gani hiyo?

Mkuu naona na wewe unaingia kwenye mambo ya plagiarism... hahahaaa. Maana hiyo hoja ya kumtaja shetani umeikopa CHADEMA halafu hutaki kuonyesha reference!!! Tafuta yako katibu mwenezi... au ndo mwendelezo wa kueneza CHADEMA?

Kwa bahati mbaya CDM hawajaweka mgombea huko kwa sababu hujawahi kwenda huko. Najua siku si nyingi utaenda huko kushangilia 'ushindi', na hapo utatusaidia kuihubiri CDM. Probably 2015 CDM huko wataweka mgombea maana utakuwa umeieneza vya kutosha...
 
Katika hali inayodhihirisha Nape Nauye anaiogopa sana chadema nikutokufikiria kuwa Tanzania kunavyama vingine vya upinzani....mkuu NCCR hauijui? au CUF umeisahau? Vipi kuhusu TLP? Na kile chama chenye bendera nyingi kuliko idadi ya wanachama (ADC) haukitambui? au hivi vyote havijaweka wagombea? Kama havijaweka wagombea mbona hauvisemi?.....bwana mdogo Nape kitu kikubwa ambacho mwenyezi Mungu ametunyima binadamu nikutokuijua kesho yetu suala linalotufanya tuamini kwamba nchi hii itakuwa chini ya ccm milele....Naomba nikutakie jumapili njema!


Katika medani ya ushushu, kauli za wendawazimu au walevi mbwa, ni za muhimu kuliko za maprofesa. Mara nyingi walevi hutoa yale ya ukweli yaliyojaza nyoyo zao tofauti na wanapokuwa wazima katika fahamu zao kamili.

Hivyo, kama ni kweli chama hakijasimamisha mgombea kwenye kata husika, badala ya kumshambulia mleta mada, chukulieni maneno yake kama changamoto na sio kumbeza au kumtukana kwani kufanya hivyo kwa mlevi haisaidii! Maono ya chama ni kwenda hadi ngazi ya chini kabisa ya familia, how comes, kinashindwa kusimamisha mgombea katika ngazi ya juu kama kata?

Kama kimeshindwa kufanya hivyo kwa hivi vi-kata vichache 26; kitaweza kufurukuta katika Uchaguzi Mkuu 2015 ambao utahusisha mamia ya kata na changamoto kibao? Acheni mbwembwe na tambo zisizo na mashiko, fanyieni kazi maneno ya mwendawazimu hata kama aliyeyatoa ni punguani lakini ukweli ni ukweli tu hata kama umetolewa na Shetani.

CC: Tumaini Makene, Dr W. Slaa, Molemo, Ben Saanane, John Mnyika, Tundu Lissu, Mwita Maranya, Michael Aweda
 
Back
Top Bottom