CCM yanguruma Busanda; Wapinzani chali!

CCM yanguruma Busanda; Wapinzani chali!

Nakuomba uendelee kuniaminia kwa sababu ni hakika bila mashaka mimi sio mshabiki wa chama chochote bali ni pro-democracy ambaye ningependa kuona upinzani unashinda ili kuongeza wigo wa demokrasia ndani ya bunge

Pasco

Mwanzoni nilikuwa sijakuelewa ndo maana nilitaka tofautiana na wewe ....nimekukubali umejitahidi kutufikishia yale yaliyojili bila ushabiki..sipendi bunge la upande mmoja, wabunge ambao wako bungeni bila kujua wanafanya nini nadhani ni wakati wakupisha wenye kuleta changamoto! Busanda wameonyesha kuwa kampeni za kuwaelimisha wapiga kura zitazaa matunda mazuri 2010.

Pamoja na yote nawapongeza wanaCCM Busanda Kuchangua Sanda

Masa
 
Kushinda mmeshinda,lakini cha moto mmekiona.Kwa ufupi niwape hongera CHADEMA kwani ni chama ambacho kinakuwa kwa haraka,na CCM kimedumaa.Big up viongozi wa CHADEMA.

Mimi nafikiri kuwasifia na kuwapaka mafuta kwa mgongo wa chupa.

Mtoto kuwa wa kwanza kwa darasa la wajinga na ukampa sifa ni kumpoteza kabisa mtoto huyo.

CHADEMA waachane na makao makuu waende huko wakajidhatiti alichowashauri marehemu wakifanyie kazi.

Jamani hebu tutumie kalogic kadogo hivi utaipa tenda kampuni ambayo hata hard adress haina.? CHADEMA watapewa je ushindi huko ambako wenda wilaya nzima wana ofsi moja ama hakuna kabisa?
 
hata mie mwana CCM mzee....tupongezane...lakini wakuu wanamtandano wenzangu tukumbukane kwenye kugawana vyeo......FMES,kibunango sasa nguvu tuzihamishie biharamulo.....

Kama CCM mnataka aibu muwekeni Yo Yo kwenye mtandao wenu....jamaa atakuwa busy na kuuza siri zenu kwa mashori!
 
Kama CCM mnataka aibu muwekeni Yo Yo kwenye mtandao wenu....jamaa atakuwa busy na kuuza siri zenu kwa mashori!
aaaah shem unanivua ngua hadharani......mkuu wewe si unaona wanaojiita manguli wa ChADEMA hapa JF tuluvyowatoa jasho.....nakuambia siasa sio kukandamiza keyboard na kuungurumisha helkopta......CCm daima
 
Binafsi kwa matokeo haya bado naona tumeshinda pamoja na kwamba Magesa haendi bungeni. Hakuna mtu atakayebisha kuwa operasheni sangara imefanya kazi, na kwamba CHADEMA really is becoming an alternative party and a government in waiting. Siku za CCM zinahesabika, sio chadema walioamua hivi ni wananchi wenyewe.

Hili pia ni jibu kwa tafiti tata za REDET. Sasa wajiulize hizi data ambazo wamekuwa wakitoa zikionyesha kwamba CCM bado wanakubalika sana hasa vijijini hao research assistants wao huwa wanazitoa wapi? Hawa ma-RAs wa REDET wanaendaga field kweli au hujaza dodoso wenyewe?

Na mwisho hili liwe ni jibu kwa ndugu zetu CUF kwamba wananchi wameshaamua kuwa huku bara mbadala wa CCM ni CHADEMA. Wakiendelea kulifumbua macho hili wananchi watawaweka katika kapu moja na CCM na athari zake hazitaishia bara, bali zitateremka hadi visiwani.

Kitila Mkumbo,
Unasubiri nini ndugu yangu kuingia uwanjani? Nakumbuka uongozi wako mzuri kabisa pale UDSM ukiwa rais wa DARUSO in the 90s. Mimi binafsi I say you can be a good president of this country kuliko Zitto mzee wa Dowans. Kwa uhakika sina imani na Zitto tena hata afanyeje. Ndo maana hata Biblia inasema chumvi ikiwaimeharika itatiwa nini hata ikolee? Mkumbo inabidi jina lako lianze kusikika kuanzia Bungeni on the way to the presidentail post. Hili ni ombi langu maalum kwako.
 
Ccm kura 29.000 chadema 21,000 bado matokeo ya vituo 8

Wananchi 21,000 si wa kubeza,ni hatua.....Ina maana mabadiliko ni lazima. Kuna mtu mwenye data za matokeo ya uchaguzi uliopita Busanda ili tuweze kufanya comparisons? Itakuwa vyema ili kabla ya wana chadema kujifariji ni muhimu kuweka concrete data to prove so.
 
Binafsi kwa matokeo haya bado naona tumeshinda pamoja na kwamba Magesa haendi bungeni
mkuu KM hizi ni ndoto za alinacha nyie CHADEMA niwaambie ukweli mambo yenu ni kama zimamoto jiimarisheni kwanza vijijini uuze sera pelekeni helkopta siku zote vijijini sio wakati wa uchagusi ndio mnaungurumisha......

Hakuna mtu atakayebisha kuwa operasheni sangara imefanya kazi, na kwamba CHADEMA really is becoming an alternative party and a government in waiting. Siku za CCM zinahesabika, sio chadema walioamua hivi ni wananchi wenyewe.
mabadiliko yapi operesehni yenu umefanikiwa? mafanikio ongezeni viti bungeni....sasa wcheni kupiga kelele kwenye keyboard ingieni mtaani,wafikie wananchi wasiojua hata kusoma uuze sera zenu labda mtaikaribia ccm....
 
Guys!!! for once we have to be true.... aliyechangia chachu ya yote ni magufulu

Can we have a little repsect to JOHN POMBE MAGUFULI.... wa ndani mnanisoma vilivyo!!!!!

Kwani Magufuli naye alienda huko Busanda kwenye kampeni? Mbona sijamsikia? Au unazungumzia utendaji wake wa kazi?
 
Mimi nafikiri kuwasifia na kuwapaka mafuta kwa mgongo wa chupa.

Mtoto kuwa wa kwanza kwa darasa la wajinga na ukampa sifa ni kumpoteza kabisa mtoto huyo.

CHADEMA waachane na makao makuu waende huko wakajidhatiti alichowashauri marehemu wakifanyie kazi.

Jamani hebu tutumie kalogic kadogo hivi utaipa tenda kampuni ambayo hata hard adress haina.? CHADEMA watapewa je ushindi huko ambako wenda wilaya nzima wana ofsi moja ama hakuna kabisa?

ccm wanatumia hela ya tra kulisha matawi ya vijijini
je chadema watatoa wapi hela ya kuwa na matawi mengi vijijini ...
 
Nawapongeza CCM for winning the uchaguzi.... Kama alivyosema Nyerere once, ushindi ni katika grassroot na si vinginevyo!!!!

Pia nawapongeza CHADEMA kwa kutoa upinzani ambao ni wake up call kwa mkoa wa mwanza na hasa wilaya ya geita, it has never been this way before

Wazo la Leo: Kitila rudi nyumbani ufanye kazi, hakuna remote control kwenye siasa, wew tulisota pugu na akina nzowi na najua potentials zoooote ulizonazo

unfortunately, sina kambi maalum kwani mimi ni mhudumu tu!!!


Its LONG ROAD TO THE PROMISED LAND AND mUSA NEVER SAW THE LAND!!!!!!!
 
mkuu KM hizi ni ndoto za alinacha nyie CHADEMA niwaambie ukweli mambo yenu ni kama zimamoto jiimarisheni kwanza vijijini uuze sera pelekeni helkopta siku zote vijijini sio wakati wa uchagusi ndio mnaungurumisha......


mabadiliko yapi operesehni yenu umefanikiwa? mafanikio ongezeni viti bungeni....sasa wcheni kupiga kelele kwenye keyboard ingieni mtaani,wafikie wananchi wasiojua hata kusoma uuze sera zenu labda mtaikaribia ccm....

Cha muhimu tusubiri data za uchaguzi huu vs uliopita ili tuweze kufanya comparisons kuona kama wamepiga hatua ama la,si vyema kuzipuuzia juhudi na nia njema za wazalendo.
Kwa mfano mimi sijui kama uchaguzi uliopita wa 2005 kama chadema walishinda hata maeneo ya mjini nk. Idadi ya wapiga kura,ili tuweze kufanya analysis inayoeleweka na convincing.. Moto wowote ule kabla haujatapakaa huwa na chanzo, kama moto wa vita ya ufisadi umepata chanzo,si vyema kupuuza kwani inategemea na juhudi za kuusambaza moto huo. Lakini kabla ya kusambaa ni lazima kuwe na chanzo,binafsi naamini kuwa sasa ni kazi za hao waliopo huko mijini kwenda huko vijijini kusambaza moto huo kwa ndugu zao waliowaacha huko.
 
kweli wasukuma hawaoni umasikini.....siku wakijua kwamba kura yao kwa sisiemu ndo inawafanya wawe masikini, basi chama dume kiatanguka..... wananunuliwa kirahisi mno, wanawake ni chumvi ya mawe , wanaume gogno, vijana soda na ahadi hewa....mpaka miaka miatano tena!!!!
 
kweli wasukuma hawaoni umasikini.....siku wakijua kwamba kura yao kwa sisiemu ndo inawafanya wawe masikini, basi chama dume kiatanguka..... wananunuliwa kirahisi mno, wanawake ni chumvi ya mawe , wanaume gogno, vijana soda na ahadi hewa....mpaka miaka miatano tena!!!!
hao chadema kwenye majimbo yao wamefanya nini la maana? jimbo kama la Zitto kabwe.........mbunge yuko dar muda woote ana tofauti gani na muungwana....wapinzani wajipange upya...
 
It all comes back to what I said before... vyama vya Upinzani bila kuunda umoja hawawezi kumshinda CCM.. Hili ndilo funzo.. swala la kupongeza Chadema kwa jitihada na kadhalika halina nafasi ktk fainali..ni makosa kufungwa goli hata moja watu wakachukua kikombe, ikiwa sababu imetokana na mapungufu ambayo tunayafahamu..
Wananchi wa Busanda wanapoteza mwakilishi wa haki kwa sababu ya udhaifu wa vyama vyetu..
 
Kulingana na historia ya nchi yetu kisisasa na ninavyoona matokeo haya ya Busanda, ninaendelea kuamini imani kuwa Tanzania bado ni sikio la kufa.
 
Kwa mujibu wa tovuti ya chadema kuhusiana na uchaguzi wa ubunge jimbo la Busanda 2005, sijaweza kuona alizopata mgombea wa ccm plus total votes,lakini kuna hatua,mgombea wao alipata kura zifuatazo...

Busanda alisimamishwa ISMAIL, Manyanya Chalahani kura 3,1070 ambazo ni asilimia .351%
 
It all comes back to what I said before... vyama vya Upinzani bila kuunda umoja hawawezi kumshinda CCM.. Hili ndilo funzo.. swala la kupongeza Chadema kwa jitihada na kadhalika halina nafasi ktk fainali..ni makosa kufungwa goli hata moja watu wakachukua kikombe, ikiwa sababu imetokana na mapungufu ambayo tunayafahamu..
Wananchi wa Busanda wanapoteza mwakilishi wa haki kwa sababu ya udhaifu wa vyama vyetu..
Ni kweli nilisema mahali kama Wanabusanda wanachagua mtu, Magesa ndiye angekuwa mbunge, kwa vile wanachagua vyama, mgombea wa CCM ni bomu ila CCM imembeba, CCM imshukuru sana Mzee Malecela busara zimeokoa, Mama Kilango aliyetoa maneno makali ya kuzaliwa na mwanamke, John Pombe Magufuli aliyepiga kampeni kwa Kisukuma lugha ambayo wanaielewa na Mhe. Dialo ambaye TV yake na Radio yake vimeibeba CCM.
Japo mshindi wa CCM ni bomu, Mama Anne Kilango ameahidi kumlea ili awe kama yeye, ukibebwa, bebeka, asipobebeka, 2010 Busanda inaondoka CCM.
 
Back
Top Bottom