Ushindi ni ushindi tuu, 'The Winner Takes it All, the looser standing small' ni wimbo wa ABBA.
Lazima tuipongeze CCM kwa ushindi wa kishindo.
Nimehudhuria kampeni na kushuhudia upigaji kura. aminini msiamini, CCM imeshinda sio kwasababu inapendwa sana, bali vijijini bado wamelala, mimi ni Msukuma niliyezaliwa na kukulia mjini. Kitendo na kurudi vijijini na kushuhudia jinsi literacy level ilivyo kubwa kimenisikitisha na kunihuzunisha. Asilimia kubwa ya ndugu zangu hawajui kusoma wala kuandika na hizo kura imebidi wapigiwe.
Hii ignorance level CCM wameitumia to their advantage. Siwatukani Wasukumu, ili tumethibitisha ujinga, sisi sio watu wa fujo ila sio siri Wasukuma wa vijijini, tumelala mno!.
Inahitajika civic education ya ukweli kuwafanya mamilioni ya Watanzania wanaoichagua CCM bila kujua wanachagua nini. Pia kuna sisi tunaoichagua CCM kwa sababu hakuna mbadala. Baada ya kuhudhuria kampeni za Chadema jana pale Katoro, nikasema kama CCM itashinda, basi wanaKatoro ni vichaa au wamelogwa.
Chadema imethibitisha inaweza kuwa chama mbadala, Watanzania waliolala wanazidi kuamka na wale wajinga wanazidi kuelimika.2010 will never be the same, japo sio anguko kuu la CCM, but the going gets tough na mabadiliko yanakuja.
Wenzetu ilio mbali, Geita isikieni hivyo hivyo, ndio wilaya yenye utajiri mkubwa wa dhahabu kuliko wilaya zote. Kwa kifupi ndio wilaya tajiri zaidi Tanzania mzima, lakini watu wake ni masikini wakutupwa!. Nyumba za nyasi ni nyingi kuliko nyumba za bati!.
Watoto wanasura za kutilisha huruma, Wakinamama sura za kukatisha tamaa, kinababa sura za mashaka, dada poa Geita buku, buku mbili, ukitoa dala anataja kuhamia! Unagusa tuu, kwisha hata hujasema!, kama ni kwenu unaweza kulia
Hiyo ndiyo Geita iliyozungukwa na Geita Gold Mine, upande mwingine Bulyanhulu, upande mwingine Buzwagi, upande mwingine Kahama Gold Mine, hivi kuna sababu kweli ya Geita kuzama kwenye lindi la Umasikini?. Yote hayo wameambiwa ni kazi nzuri ya CCM na bado mnawachagua kuyaendeleza kisa
wasukuma ni masikini jeuri, umasikini ni jadi yetu, utajiri hatuujui and you can never miss something you have never had.
Wasukuma bado wamelala, wakiamka, walioamka watalala 2010!.
Naomba nikatishie hapa nisije ishia kulia bure...
Kidumu Chama Cha Mapinduzi ....
Pasco.
Lawama za ndugu zako wa vijijini kutokuwa na elimu hata wewe unahusika,umechangia kwa kiasi kikubwa wao kuwa wajinga, ni watu wachache au mmoja huleta mabadiliko kwenye jamii yake.
kama kweli ni kwenu basi unajitukana mwenyewe.ushauri tengeneza sasa mikakati ya kuwainua jamaa zako usisubiri kundi la kampeni ya Chadema liende ndio nawe uende.fungua NGO ya kuleta maendeleo huko mtafanya Mengi ya maana ,kuliko hata angepatikana mbunge kupitia Chadema au Cuf.kuna watu wengi wa Mwanza wamefanikiwa ukiwa mkweli watakusaidia,upinzani kwa kiasi kikubwa umeanzia Mwanza vijijini na shinyanga kwa kina Cheyo na Danhi Makanga.
watu wa mikoa ya Arusha na Kilimanjaro wanajipanga wenyewe kabla ya kusubiri serikali iwaletee maendeleo.ukiwa unaishi Dar basi unachukua jamaa wa kijijini kwako waje kusoma.Wapemba na wakinga wameinuana kwenye biashara kwa utaratibu huo.
Kingine usibabaike na helkopta iliyokwenda siku tatu kabla ya uchaguzi ilitakiwa MBOWE awepo huko kipindi cha kujiandikisha kupiga kura,sio siku tatu kabla ya uchaguzi.kama mtu amevutiwa na sera zako hawezi kujiandikisha kwani siku za undikishaji zimekwisha.
Mrema alikuwa anapata watu wengi 1995 kwenye mikutano yake lakini sio wapiga kura,watu wakiona kuna mkusanyiko hata wakupigwa risasi kwa watanzania wanajazana.
Busanda kama ni kijijini ikija Helkopta wanakijiji wanafuata helkopta sio chama wala sera ni kama imekuja sinema au wanatizama mpira.
MkamaP amekujibu kuwa kuwa mjini sio uelevu, ukitizama jiji la Dar-es salaam maeneo ya waliokwenda shule hayana ushawishi wa upinzani ni maeneo ya wasiosoma kama MBAGALA ndiko utaona upinzani una nguvu kama vurugu alizopata mkuu wa mkoa bwana Lukuvi toka kwa mwenyekiti wa serikali za mitaa wa CUF.
MBAGALA ikiwa jimbo la Kigamboni ilitoa mbunge pekee wa upinzani Frank Magoba kwa tiketi ya CUF.
Zitto Kabwe jimbo lake ni la kijijini kuliko Geita au Busanda,marehemu Kabuye mbunge wa TLP yeye anawakilisha Bukoba vijijini,Tlp wameshawahi kushika Kilimanjaro vijiji, unaweza kusema watu wa Bukoba na Kilimanjaro wamesoma lakini kwa Zitto KABWE ni kijijini na kunawasio soma wengi.
mfano wa wazi ni kisiwa cha Pemba majimbo yote ya Pemba hakuna CCM na huko hakuna shule nyingi au umjini,wapemba wengi wanaonekana ni washamba kwa waunguja.
Vyama vya siasa vinatakiwa muda kama huu kuwa bukoba vijijini kuanza kujitambulisha,hawafanyi hivyo kwa vile hawana PLAN na hawataki kupoteza pesa zao wanasubiri bado wiki mbili ndio wanapita.
wewe kama mpenzi wa chadema chukua mfano wa MBEYA VIJIJINI ambako Chadema na CUF vilipata wafuasi wengi kule ni MBEYA VIJIJINI sio mjini CUF walipata karibu kura elfu kumi na kitu wakaweka upinzani mkubwa kwa ccm, jee baada ya uchaguzi ule kuna chadema au Cuf wamekwenda tena? au kuna mkakati wa kuona kuwa eneo lile ni rahisi kupatikana kunatakiwa plan ya kurudi mara kwa mara?
hivi kura mlizozipata BUSANDA mtazipoteza kwani hamtakwenda tena hadi uchaguzi wa mwakani mtapiga kampeni ya siku moja,huwezi kushinda.
elewa kuwa 2010 sio rahisi chadema kupata kura zaidi ya hizo kwani MBOWE,ZITTO,SLAA na wengine watakuwa hawana muda wa kukesha kwa wiki kadhaa kwani wao watakuwa na shughuli kwenye majimbo yao.inasikitisha Pasco huna utaratibu wa kuwapitia watu wa kijijini kwenu hadi umekwenda kikazi au kikampeni.
ukianza wewe wenzako watafuata,fanya fund raising ya kujenga shule moja kwenu tutasaidiana hapa hapa JF.kuwaletea maendeleo watu wako sio lazima uwe mbunge,wapo wabunge wanaojua wajibu wao kama MKONO na Ndesamburo kwa wapiga kura wao.